Mlipuko watokea Ubungo-TANESCO, umeme wakatika!

Mlipuko watokea Ubungo-TANESCO, umeme wakatika!

Hawa ccm wajanja sana. Ili tusahau katiba, wanatuletea breaking news. Ikipita hii kama issue ya katiba itakuwa haijakaa vizuri kwao watagongesha hata treni hawa.
Im just thinking loud.

wameanza na tusker challenge cup na tunalichukua katiba inasahaulika.nukta
 
kumbe na wewe huwa ukijisahau unachangia mada. Nimezoea kukuona kule kwenye mambo yako yale.

Anyway, kila lenye mwanzo lina mwisho. Hili swala la umeme lipo mbioni kutatuliwa.

naona umechukua nafasi ya badra masoud.nukta
 
Samahani
VOICE FROM DARKNESS!
kwa kuwa mlijua mtahojiwa juu ya ahadi ya PM Na Ngeleja bungeni wakati hamjaitimiza..Mnatuletea sinema? Vinjiti vyetu vinakufa kwenye incubators,nyama zinaoza kwenye friji.mnaekti kulipua transformer kutudivert akili zetu eh! Hapa mmenoa.hata ****** alisema za mbayuwayu changanya na za kwako.anaebisha aseme kisa kwa nini kibaka asifie uraiani kwenye wananchi wenye hasira kali akafie polisi post? I mean transformer kulipukia pale power plant ni uzembe au hujuma!
 
Nchi hii banaa baada ya kuona mjadala wa Katiba umepamba moto sasa wakamua kudiverge kwenye umeme hii ishu ya transformer imekaa kiusanii zaidi ukiongea na Tanesco wanakwambia ohoo tunarekebisha kuna baadhi ya maeneo hayana umeme tokea jana.
 
Kazi Ya Kikwete na Usalama wa Taifa hawana pakutokea ni kweli transformer halijalipuka nadhani wakati umefika kuwaonyesha kwamba wananchi nfio wenye nchi
 
Mi nilikua nakatiza pale daraja la rivasaidi, nimeona kwa macho yangu moto mkubwa ukiwaka kwenye eneo la gridi ya taifa. Kama isingalikua jitihada za kampuni binafsi ya ulinzi ya knight support basi hali ingekua mbaya sana kwani zimamoto ya jiji ilichelewa sana kufika eneo la tukio.

Taarifa zinadai kuwa hadi sasa jamaa wanahangaika kusolve tatizo lakini inaonekana kuwa huenda tukjasubiri kwa zaidi ya saa 24 hadi 48 kuweza kupata umeme.
 
Hilo nalo linawezekana, Lakini tutajua ukweli wake muda si mrefu.

Hakuna siri ya watu wawili labda mwingine awe amekufa.
 
Tshs Millioni 900 zahitajika kununua kifaa kilichoharibika ktk mlipuko wa mtambo wa TANESCO:

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco, Sophia Mgonja aliwaambia waandishi wa habari kwamba: "Hadi sasa hatujui chanzo na wala athari zake. Umememe umekatika jiji zima na hatuwezi kurudisha hadi tutakapofanya uchunguzi kuona kiwango cha uharibifu."

Alisema kifaa hicho kilichoungua kinachokadiriwa kuwa na thamani ya Dola za Marekani 500,000 (takriban Sh 900milioni) hakitengenezeki na badala yake kinatakiwa kuagizwa kingine.

Mgonja alisema mbali ya kifaa hicho vingine kama ‘Control Cable' pamoja na vikombe vya kwenye nguzo ambavyo vilikuwa havionekani kutokana na kufunikwa kwa moshi huenda navyo vimeteketea."Kuanzia sasa mafundi wanaanza kazi ya kuchunguza chanzo cha tukio hilo lakini pia kuona namna tunavyoweza kurudisha umeme kwa wakazi wa jiji la Dar es Salaam".

Source: Mtambo Tanesco waungua
 
umeme kwetu umekatika saa 12;30 baada ya kuwaka kwa masaa 3 sijui transfotmer imelipuka tena?
 
Me nilivyosikia habari hizi nikahisi foul play. Haya magamba yako radhi kufanya chochote ili ku-justify their incompetence. Watasema ahadi zimetekelezwa, lakini si mmsikia mlipuko SONGAS, ndo maani bado kuna problems.
 
Samahani
VOICE FROM DARKNESS!
kwa kuwa mlijua mtahojiwa juu ya ahadi ya PM Na Ngeleja bungeni wakati hamjaitimiza..Mnatuletea sinema? Vinjiti vyetu vinakufa kwenye incubators,nyama zinaoza kwenye friji.mnaekti kulipua transformer kutudivert akili zetu eh! Hapa mmenoa.hata ****** alisema za mbayuwayu changanya na za kwako.anaebisha aseme kisa kwa nini kibaka asifie uraiani kwenye wananchi wenye hasira kali akafie polisi post? I mean transformer kulipukia pale power plant ni uzembe au hujuma!

hizi ni hujuma ndugu yangu hamna kulipuka wala nini
 
Tshs Millioni 900 zahitajika kununua kifaa kilichoharibika ktk mlipuko wa mtambo wa TANESCO:


hapo waheshimiwa washaweka chao, maana wanajua ni emergency lazima hiyo pesa ipatikane. Late night umeme ulirudi ..sijui walitumia means gani maana haikupita 2hrs wakalamba tena.
 
Back
Top Bottom