Mlipuko tena Arusha, jeshi la Polisi watuhumiwa

Mlipuko tena Arusha, jeshi la Polisi watuhumiwa

Serikali yetu inaendeshwa kwa kafara ya damu za raia, hapo jk anataka damu imwagike kwa wingi kabla hajamaliza mda wake,.
Wanaomwaga damu ya watz ni chadema. Waliua morogoro, arusha, iringa - mwangosi na bado wanaendelea.
 
Kwa hiyo unataka kutuambia polisi wetu ni vichaa au?

Hapo gongo haijaruhusiwa mnapost vitu kama hivi ikiruhusiwa itakuwaje?

Mzee embu acha utani kwenye hoja kama hizi,kama huwezi jibu kwa hoja then better ukae kimya mana tunaongelea maisha ya waTanzania.

Tafadhali kwa hilo
 
Wakati ulipochakachua rambirambi za Mwangosi ulilewa gongo?
Wewe mfuasi wa slaa ndio mlevi wa gongo. Hapo umeharibikiwa ubongo haijahalalishwa, siku slaa akiihalalisha utaanza kuongea peke yako barabarani
 
Kabla hamjampa Mbunge zuzu kama lema nafasi haya yalikuwa yanatokea huko??yan nikiunganisha dots naona huyu pimbi ameigharim sana arusha,2015 chama chenu kisimamishe mtu mwenye weledi wa uongoz bora na sio kuleta wahun wahun wasio jitambua,Arusha mji mkubwa huo,hauwez ongozwa na akili ndogo hata siku moja,mbona moshi kwa mzee ndesa na hai kwa mbowe kuko salama tuh??hatuskii machafuko kama hayo,,Arusha achene ujinga msifanye makosa kama hayo 2015,sisemi muichague CCM la hasha,ila nasema chama chenu kisimamishe mgombea anaejitambua,sio hyu mnaemuita Min Kabaang,,,!

unataka kusema arumeru lema ndiye anayeongoza?
 
Habari ni za kweli nasikiliza Wapo radio sasa hivi anaeweza kufungulia radio atapata hiyo habar, sasa hawa polisi wetu wana mtindio wa ubongo au hao waumini walikua na maandamano wakambiwa waondoke wakakaidi amri?
 
Sera dhalimu za mbunge wa arusha mjini

Hii kali, mbunge wa arusha mjini ana sera zake binafsi kuongoza jimbo la arusha mjini? Anatekeleza sera zake serikali ya CCM inamtazama tu? Anatoa order polisi wakalipue wapi serikali kimya! Kwa nini? Lema atasingiziwa kwa mengi arusha mjini lakini hiyo haiwezi kuondoa ukweli wa udhaifu wa serikali ya CCM. Propagandists mtapiga porojooooo lakini wananchi wanajua ukweli wa mambo na wataendelea kusimamia kwenye ukweli.
 
Kwa hiyo unataka kutuambia polisi wetu ni vichaa au?

Hapo gongo haijaruhusiwa mnapost vitu kama hivi ikiruhusiwa itakuwaje?

Mkuu nasikia umekuwa nominated ku kolekt rambi rambi kwa ajili ya Marehemu Mgimwa.
Ya kweli haya, if YES tutegemee nini aisee?
 
Sass hili Ni jeshi la kulinda usalama WA raia au kuua raia?

[h=3]MLIPUKO TENA ARUSHA, JESHI LA POLISI WATUHUMIWA[/h]

Taarifa ambazo zimetufikia kupitia kituo cha WAPO Radio FM zinaeleza kwamba kuna bomu limelipuliwa kwenye kanisa katoliki la Mtakatifu Karoli, Ruanga huko USA River jijini Arusha, ambapo wanakwaya takriban 6 wamejeruhiwa.


Kwa mujibu wa taarifa hizo ambazo zimetufikia, zinaeleza kwamba watuhumiwa ni jeshi la Polisi, na kwamba walirusha kitu kinachosadikiwa kuwa bomu - lililojeruhi 6, ambapo 4 kati yao wameruhusiwa baada ya matibabu kwenye hospitali ya Mission na ya Wilaya ya Arumeru.


Majira ya saa sita na nusu, waumini walidai kuona gari la polisi likipita kwa kasi, na lilipowakaribia walistuka mlipuko ukiwarusha pembeni, ambapo walijikuta na majeraha na usoni, mapajani na maeneo mbalimbali ya mwili. Kisha baada ya hapo gari ilisogea mbele na kuanza kurusha mabomu kwa watu wowote iliokutana nao.


Hadi sasa inaelezwa kuwa uchunguzi umeshaanza kufanyika, huku Kamanda Liberatus Sabas akikataa kuzungumzia zaidi suala hilo. Alipotafutwa na WAPO Radio FM, hakueleza kwa kina, lakini akasema kuwa sio suala la kwaya kama ambavyo imeelezwa, bali ni wakinadada wawili na kwamba hawezi kuzungumza zaidi, bali kesho (Ijumaa) atatoa taarifa rasmi na iliyo kamili kwa vyombo vya habari.


Alipoulizwa kuwa kama ni kweli jeshi la Polisi linatuhumiwa kuhusika, alisema kuwa atazungumza kesho kuhusiana na tukio hilo. Tukio hili limetokea ikiwa ni siku mbili zimepita tokea kuapishwa kwa Inspekta Jenerali wa Polisi mpya, Ernest Mangu ambaye amechukua nafasi ya IJP Said Mwema aliyestaafu.

Source: Gospel Kitaa.
 
Mungu atusaidie,,na udhalimu huu ukashindwe,,Tanzania itasimama imara,,na kamwe haitateteleka kwa matendo haya ya kigaidi.
 
Kwa hiyo unataka kutuambia polisi wetu ni vichaa au?

Hapo gongo haijaruhusiwa mnapost vitu kama hivi ikiruhusiwa itakuwaje?
mkuu si umesikia wananchi wamewaua watu watano waliokula hera za rambirambi utakapokuja Tanzania uwe na tahadhari.
 
Kwa hiyo unataka kutuambia polisi wetu ni vichaa au?

Hapo gongo haijaruhusiwa mnapost vitu kama hivi ikiruhusiwa
itakuwaje?[/QUOTE
......unauliza majibu? Kwani we unadhania Polisi wetu sio vichaa?
jiangalie wewe kama mfano wa polisi wetu uliyetimuliwa kwa wizi kisha
utajua kama ni wazima au la!
 
[h=3]MLIPUKO TENA ARUSHA, JESHI LA POLISI WATUHUMIWA[/h]

Taarifa ambazo zimetufikia kupitia kituo cha WAPO Radio FM zinaeleza kwamba kuna bomu limelipuliwa kwenye kanisa katoliki la Mtakatifu Karoli, Ruanga huko USA River jijini Arusha, ambapo wanakwaya takriban 6 wamejeruhiwa.


Kwa mujibu wa taarifa hizo ambazo zimetufikia, zinaeleza kwamba watuhumiwa ni jeshi la Polisi, na kwamba walirusha kitu kinachosadikiwa kuwa bomu - lililojeruhi 6, ambapo 4 kati yao wameruhusiwa baada ya matibabu kwenye hospitali ya Mission na ya Wilaya ya Arumeru.


Majira ya saa sita na nusu, waumini walidai kuona gari la polisi likipita kwa kasi, na lilipowakaribia walistuka mlipuko ukiwarusha pembeni, ambapo walijikuta na majeraha na usoni, mapajani na maeneo mbalimbali ya mwili. Kisha baada ya hapo gari ilisogea mbele na kuanza kurusha mabomu kwa watu wowote iliokutana nao.


Hadi sasa inaelezwa kuwa uchunguzi umeshaanza kufanyika, huku Kamanda Liberatus Sabas akikataa kuzungumzia zaidi suala hilo. Alipotafutwa na WAPO Radio FM, hakueleza kwa kina, lakini akasema kuwa sio suala la kwaya kama ambavyo imeelezwa, bali ni wakinadada wawili na kwamba hawezi kuzungumza zaidi, bali kesho (Ijumaa) atatoa taarifa rasmi na iliyo kamili kwa vyombo vya habari.


Alipoulizwa kuwa kama ni kweli jeshi la Polisi linatuhumiwa kuhusika, alisema kuwa atazungumza kesho kuhusiana na tukio hilo. Tukio hili limetokea ikiwa ni siku mbili zimepita tokea kuapishwa kwa Inspekta Jenerali wa Polisi mpya, Ernest Mangu ambaye amechukua nafasi ya IJP Said Mwema aliyestaafu.

Source: Gospel Kitaa.

Nawapigwe tu!
 
Nini Gongo? Colorado (USA) wameanza kuuza bangi rasmi kihalali toka jana
Watu wanajadili kwa mshtuko wewe unachafua
Issue ni kutafuta ukweli wa habari na sio kukashifu

Sasa hao wavuta bangi wanatuhusu nini sisi huku bongo!?

Au kwa sababu wazungu basi hata mavi yao mali!
Kule ni colorado na huku ni bongoland!!

Wacha kuwa mtumwa wa kiakili wewe! Hapa bado tunapigania CDM wapigwe chini 2014 ili hio GONGO isihalalishwe!
Halafu we unataka kutuletea habari ya bangi tena!!?

Huna adabu kabisa we kijana!

Wakati ule wa sungusungu mtu kama wewe tunapiga mikwaju ya viganja siku nyingine usiweze kuandika utumbo wa namna hii.
 
Hao ndo polisi ccm eti wanatekeleza kauli ya mzee kwamba kama hawatii sheria bila shurutg kong'ota
 
Kwa hiyo unataka kutuambia polisi wetu ni vichaa au?

Hapo gongo haijaruhusiwa mnapost vitu kama hivi ikiruhusiwa itakuwaje?
Mwagito, sijakuelewa, unamlaumu mleta uzi au source yake? Kasema Wapo radio ndio wame-report hivyo! Hebu soma tena uzi!
 
Back
Top Bottom