Salam wanaJf
Wanandoa mnawezaje kuishi na wenzi wenu kwa muda mrefu, mwenzi ambaye amekuzwa kwao huko, mpo tofauti kitabia na makuzi, mnawezaje kuvumiliana. Nimeuliza hili jambo ili ambao bado hatujaoa tusije wachoka wake zetu tukawafukuza bure.
Ilikuwa ni siku moja nimeweka appointment na mwanadada mmoja kuwa atakuja kushinda weekend nyumbani kwangu (nimepanga), mawasiliano yalikwenda vizuri mpaka alipofika, tulikaa vizuri ila baada ya muda nikaanza kuhisi kero, maana kuna mambo alikuwa anafanya mimi sipendelei kabisa.
Nilipokuwa nakula naye nilihisi siko sawa maana mwenzangu anatafuna bila kufumba mdomo, halafu anatafuna kwa sauti( siipendi hii tabia).
Mpangilio wa vitu ndani utabadilishwa uwe kama anavyotaka yeye, hapa nikachoka kabisa, yaani utaratibu wa maisha unabadilika kabisa.
Asubuhi tumeamka nasikia mtu ana vuta makohozi kwenye koromeo cha ajabu hamalizi, kumbe huwa ni utaratibu wake kila akitaka kuswaki, nikajikaza.
Kwa kuwa alikuwa ni girlfriend nilivumilia muda ulipokwisha aliondoka.
Hivi mnaishije wanandoa bila kuchukizana na keroa kutoka kwa wenzi wenu? na sisi mabachela tujifunze kutoka kwenu?
Mimi ninahisi hii amani na furaha niliyonayo itaisha siku hiyo hiyo nitakapooa maana yataka moyo.