Hakuna aliye mkamilifu, mrekebishe kwa kile unachoona hayuko sawa. Ukiona hakuelewi, acha kumrekebisha. Elekeza nguvu na akili yako katika kutafuta hela. Ipo siku atakuhoji kwanini umeacha kumsemasema ili ajirekebishe, mjibu una mpango wa kuoa mke mwingine atakayekusikiliza, hivyo umeelekeza nguvu na akili zako katika kujiongezea kipato maana unajua kuhudumia wake wawili lazima uwe fiti kiuchumi. Ishia hapo, halafu mwambie hupendi alivyosuka, asipoenda kubadili hiyo staili ya nywele mara moja, sio mtu huyo, hilo jini.