Mlioko kwenye ndoa mnashindaje hili jambo?

Mlioko kwenye ndoa mnashindaje hili jambo?

POVU RUKSA WAKUU
ndio maana wazungu wanaruhuusu watoto wao wakifika miaka 16 kuwa na GF na BF,muanze kuzoeana mapema,lkn Bongo mtu una 35 unapata mwanamke ana 30 yaani lazima kusumbuana .Mwanamke kuna vitu hutakiwi kufanya kujichokonoa puani na vidole, sijui unakula huku unaongea,kutafuna vizuri (table manners ni muhimu sana kwa mtoto wa kike),kuwa mbishi,kutema tema mate njiani nk.Kama huwezi kuvumilia inabidi uwe unamwambia kila mara,yaani ukimwambia kitu mara 10 hasipobadilika huyo kimbia babu.
MTOTO WA KIKE UNATAFUNA KAMA JENERETA?,KWACHA KWACHA KWACHA KWACHA KWACHA KWACHA.
hapo kutafuna kwacha kwacha kumeniacha hoi kabisa yani, mi vitabia vya hovyo hunifanya nisitishe mahusiano, sasa table manners ikimshinda mtu, it's obvious na vingine vitamshinda tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo hakukujambia kweli??

Ndoa sio mchezo wa kuigiza ndio maana hutakiwi kukurupuka kwenda hatua hiyo. Uzuri huyo msichana sio pretender kakuonesha upande wake mwingine wa ukweli. Ndoa sio kuishi tu pamoja legally kuna mengi ndan yake kama kuvumiliana mapungufu yenu na kurekebishana makosefu yenu.
 
Mi naona hata wewe pia una matatizo. Wewe umelelewa kwenu na una interest zako na yeye ana zake, sasa yeye kuja kwako siku moja tu atajuaje kipi unakipenda kipi ukipendi? si shids hiyo. Wapenzi wa kweli hukaa pamoja na kuweka katiba ya mapenzi yao kuwa tutaishi hivi, hiki nakipenda hiki sikipendi baada ya hapo mnaanza utelekezaji. Pia hata mtu ukimkataza kitu hawezi kubadikirika dakika moja kama kukoroga sukari katika chai anahitaji muda hivyo uvumilivu ni muhimu sana. Pia hata mkikubaliana usiyoyapenda yote hawezi yafanya siku moja hivyo tegemea atakukwaza tu mbele ya safari. Chamsingi kabisa katika makubaliano unatakiwa uwe fair usiwe wewe dictator
 
sasa mbona unakereka kwa mambo madogo hivi mfano mm huu mwaka 21 mambo yako poa ujuwe mwanamke sawa na Gari ukiliendesha mwendo kasi sawa taratibu sawa. hapa muhim kjmweleza huwa wana sikia sana na kufuata fasta muhim mweleze hili halitakiwi liwe hivi uone siku chache mambo yatakuwa kama upendavyo. wewe mweleze jambo ambalo umeona haliko sawa kama si mkaidi atafuata fasta. usichoke kumwambia unataka nn na afanye nini huwa waminifu kabisa wanawake hufuata tu kama unalo mwambia ni Jema. Fanya hivyo utafurahia maisha na mke ama mpz.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yoote 9 karibu na 10. Namalizia kwa kusema; Mapenzi buanaa. Ukimpenda, hata kama anakohoa ka exhaust ya Prado kuukuu. Hutamsikia. Ila kama umemtamani tu mtoto wa watu, hata akicheua mchuzi wako mchafu, hakika, utampata tatizo.
Acha kuwatamani watoto wa watu, wapende kwa mapenzi ya dhati. Hakuna aliye perfect duniani.
 
ukimpata sahihi kwako mapungufu yake machache utayabeba na yy vilevile atabeba ya kwako haiwezekani mkamatch 100%. kikubwa ubinafsi unauweka kando. vinginevyo hutaingia kwenye ndoa..

mfano. hayo uliyoyaona kwa huyo yanarekebishika vyema mkikaa pamoja wk atagundua hupendi hyo hali hivyo automatic anajirekebisha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na inabidi kabla ya kuingia kwenye mahusiano ujiridhishe na tabia za mwenzi wako, ili ujue unamvumilia au lah, kwa case ya mleta mada baada ya kupata papuchi na kukidhi haja zake ndo akaona madhaifu ya mwenzake

Sent using Jamii Forums mobile app
ahaha hahah tena kala mzigo usiku mzima asbh ndio anaona tabia za ajabu
 
Back
Top Bottom