Tulimumu
JF-Expert Member
- Mar 11, 2013
- 14,395
- 13,272
Baada ya kuanzishwa kwa matangazo ya digitali kumetokea msambaratiko mkubwa sana wa vituo vya televisheni hasa kutokana na kuwa na makampuni tofauti yanayorusha matangazo kwa njia ya digitali. Toka utaratibu huo umeanza vituo tajwa hapo juu vimepotea na sijui vimefungwa au vinarushwa kupitia ving'amuzi vya kampuni gani.
Ushauri kwa serikali: Naiomba serikali iweke utaratibu kuwa makampuni yote yanayorusha matangazo kwa njia ya digitali yahakikishe kuwa kila kampuni linaingiza vituo vyote vya ndani badala ya sasa kwamfano ukiwa na star times na ukataka kuangalia Clouds TV utapaswa kununua tena king'amuzi cha Zuku. Je tutanunua ving'amuzi vingapi? Kwa mtindo ulivyo sasa mtu anaweza akajikuta analazima kununua ving'amuzi vinne au vitano ili aweze kuona channels zote za ndani. Mimi naona tofauti za makampuni haya ingekuwa ni idadi na aina ya channels za nje. Za ndani ziwe kwenye kila king'amuzi!
Ushauri kwa serikali: Naiomba serikali iweke utaratibu kuwa makampuni yote yanayorusha matangazo kwa njia ya digitali yahakikishe kuwa kila kampuni linaingiza vituo vyote vya ndani badala ya sasa kwamfano ukiwa na star times na ukataka kuangalia Clouds TV utapaswa kununua tena king'amuzi cha Zuku. Je tutanunua ving'amuzi vingapi? Kwa mtindo ulivyo sasa mtu anaweza akajikuta analazima kununua ving'amuzi vinne au vitano ili aweze kuona channels zote za ndani. Mimi naona tofauti za makampuni haya ingekuwa ni idadi na aina ya channels za nje. Za ndani ziwe kwenye kila king'amuzi!