Mkwawa High School mpo?

Watu wa language nafkir mnamrem Masatu mzee wa hasira za faru, Shaban ist hukoo! kihava wa history mzee wa shalo! geog mshamrem Mirambo almaarufu Fantamagorian! NELKON nackia kasepeshwa na SENSA ya Taifa dah! ndo lyf wanaa! pamojaa! gawa nyuuz!

Vipi Chuwa yeye bado yupo???
 
Chuwa mie sina hakika sana bt ntakurushieni nkipata news! Ebanae cku hizi full mkeka hadi geti kuu! Walinzi na fence ya seng'eng'e, ila cku hizi ground halitumiki efektive, ma ustaadh wenzgngu mnarememba msikiti wetu, al adhhar, duh 2lipiga sana mkeka pale, viboko kwa wasaliti, ah. Suruali njiwa mmh! Imani we acha tu! Mungu ibariki mkwawaaa! Mmoja aandike songi la shule kama anakumbukaa! 2mit tena wanaa!
 
mbona mnamsahau kaaya? second master around 1993-6
alikuwa anatukana wanafunzi live kwenye parade. aliwahi kusema nyie darasa ......... mtajamba cheche!!!!!! baada ya wanafunzi kukataa kukata kuni za kupikia
 
Kwa wana mkwawa waliomaliza miaka ya mwishoni kabla ya kubadilshwa watakuwa wanamkumbuka mzungu (Mr. Bob) aliyekuwa anafundisha comb za sayansi kwenye inorganic chemistry. Zungu alikuwa haeleweki kabisa class maana anatema ngeli ya kiamerika, raha zaidi akipewa zamu coz mambo ya kukimbizana yanakuwa likizo wiki hiyo.
 
Kuna jamaa mmoja alikuwa anabeba physics kichwani then anakuja kutema class, tabu ni kuelezea ila alikuwa na notes tamu sana. Paper zake ni balaa , jina lake limenitoka kidogo ila somebody like NGOI
 
Mgimwa nafkir bado yupo iringa coz kuna cku nilimit nae town ir. Huyo mchizi wa kizikx nishamnyaka si mista garigo, au cyo! Kakupigisha kisayankrimu pale nini, pia nakumbuka pindi ndo 2najsepesha zea ndo wakampiga kinyota akapanda akawa makamu! Ebwanae mie nmesahau songi la chama la mkwawaa! Mnakumbuka mashndano ya don bosco!!
 
Kuna jamaa mmoja alikuwa anabeba physics kichwani then anakuja kutema class, tabu ni kuelezea ila alikuwa na notes tamu sana. Paper zake ni balaa , jina lake limenitoka kidogo ila somebody like NGOI

Huyo alikuwa anaitwa NGUI, alikuja kutepeta baada ya Kuwa Second Master, shughuli zikawa nyingi akaacha kufundisha Physics. Nakumbuka wakati niko pale kuna mwingereza mmoja ndio alikuwa anafundisha Physics.
 
Haya ile jamii ya tuliosoma mkwawa mpo? ebu tujikumbusheni yaliyotokea skul,yeyote mwenye kumbukumbu ya chocote we mwaga tuu. mimi namkumbuka sana Nelkon na Mzee Chuwa, usisahau mama Uswege!!
 
wee bwana wa miaka hiyo ni wazee na hawajui mambo ya computer nakushangaa wewe upo ktk JF sijui ulisoma nje ya africa?
 
sasa hao ni wazee wengi washafariki hawajui pc, si tunaulizia kina ngui, mtui, mgohamwende, nelkon, chuwa,mama uswege etc
 
teheeee makanyagio duh, mandazi na chai maziwa ya chai'si chai ya maziwa' kwa mzee chuwa
 
sasa hao ni wazee wengi washafariki hawajui pc, si tunaulizia kina ngui, mtui, mgohamwende, nelkon, chuwa,mama uswege etc

realtz77, nakubaliana na wewe. Sisi ambao tuliwakuta kina Mgimwa, Masebo. Wazee wa Makanyagio ndio tupo wengi ndani ya JF nashangaa kuona mtu aliyesoma 1974 yupo.

Wazee wa Shabani West na East tulikuwa tunakimbizana na Ngui sana...
 
Head Master - Mgohamwenda
Second Master - Ngui
Nidhamu - Mgimwa

Kweli mkwawa kulikuwa na Vichwa vya aina yake!!!

Kabla ya Mgohamwende alikuwepo Headmaster mmoja alikuwa anaitwa kwa jina la utani "Dudu". Huyu mtu alikuwa na tatizo la mguu mkisikia anaumwa mguu mjue kuna mwanafunzi anakufa. Lol, ilikuwa ni hatari.

mbona mnamsahau kaaya? second master around 1993-6
alikuwa anatukana wanafunzi live kwenye parade. aliwahi kusema nyie darasa ......... mtajamba cheche!!!!!! baada ya wanafunzi kukataa kukata kuni za kupikia

Yeah kwa wale tuliosoma pale miaka ya 92-94 tunamkumbuka. Nakumbuka kisa kimoja alifukuzana na jamaa mmoja alikuwa anaitwa Kerenge (jamaa mmoja kwa Kikurya), basi akamkamata akaja naye parade akaanza ku-narate story ilivyokuwa na ile sauti yake ya kuvuta wacha wanafunzi tucheke, ilikuwa kama igizo fulani vile.

Burudani kubwa ilikuwa Mkwa vs Haliendi (Highland) katika soccer.

Yeah enzi zetu hiyo 92-94 timu yetu ya football ilikuwa inatisha. Tulikuwa tumejiwekea formula ya magoli i.e 5+n yaani timu pinzani ilikuwa ifungwe goli tano na kuendelea. Na siku moja nakumbuka kidogo watu wapoteze maisha kwa ugomvi baada ya kuwafunga Highland magoli kadhaa (nimesahau idadi yake).

Kwa wale waliosoma Chemistry watamkumbuka Mzungu mmoja Mr. Gorton mzee wa maelectron yanabadalishana (yaani yanabadilishana), mengine yanaanguka mbele mengine "nyama" (akimaanisha nyuma), basi akiingia darasani ilikuwa ni vicheko vitupu.

Bila kumsahau homeboy wangu Mwalimu Busanji mkali wa Mahesabu za Fizikia. Jamaa nondo zilikuwa zinapanda hasa, maana alikuwa anaweza kufundisha kwa masaa mawili akiandika notsi na kutoa mifano kutoka kichwani (i.e akiwa hana daftari wala kitabu chochote mkononi).

Pia nakumbuka watu walivyokuwa wanaenda na vindoo vidogo vya plastiki kuchota uji jikoni mida ya saa 10 alfajiri. That was Mkwawa complex real.
 
Back
Top Bottom