Bashir Yakub
Member
- May 27, 2013
- 84
- 1,562
Na Bashir Yakub, WAKILI
Kanuni ya 135(11) ya Kanuni za Kudumu za Bunge za June 2020, inasema kuwa " Wenyeviti wa Kamati ya Hesabu za serikali(PAC), na Hesabu za Serikali za Mitaa(LAAC) wanatakiwa kutoka Kambi Rasmi ya Walio wachache Bungeni".
Kwanza kwa Kanuni hizi mpya hakuna kitu kinaitwa Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni, bali imebadilishwa na kuitwa Kambi rasmi ya walio wachache Bungeni.
Kanuni niliyotaja hapo juu inatafsiri kuwa hapawezi kuwa na kamati PAC na LAAC bila kambi rasmi ya walio wachache bungeni.
Na ili iwepo Kambi rasmi ya walio wachache bungeni ni lazima wabunge wa upinzani wafikie 12.5% ya wabunge wote kwa mujibu wa kanuni ya 21.
Mkwamo wa bunge la sasa ni kuwa wabunge wote wa upinzani hawafiki 12.5% ili waweze kuunda hiyo kambi rasmi.
Na kama hawawezi kuunda hiyo kambi maana yake kamati ya PAC na LAAC haziwezi kuwepo kwakuwa haziwezi kupata mwenyekiti aliyetakiwa atoke katika hiyo kambi.
Na bahati mbaya Kanuni hazisemi nini kifanyike iwapo Kambi rasmi haipo, au ikiwa upinzani haujafikia 12.5%.
Je inawezekana Bunge kuendeshwa bila Kamati muhimu na za lazima kama PAC ya hesabu za serikali na LAAC ya hesabu za serikali za mitaa?
Jibu ni hapana haiwezekani. Jambo moja kati ya matatu litatokea.
Moja, hiyo idadi ya 12.5% ilazimishwe ipatikane ili Kambi Rasmi ya Waliowachache Bungeni iwepo ili Wenyeviti wa PAC na LAAC wapatikane.
Mbili, itumike kanuni ya 174 ambayo inatoa uhuru kwa mbunge yeyote, waziri, au mwanasheria mkuu wa serikali kuleta Hoja ya kuomba Kanuni yoyote katika Kanuni za Kudumu KUTENGULIWA kwasababu na malengo maalum.
Maana yake mleta hoja ataomba Kanuni ya 135(11) inayolazimisha wenyeviti wa PAC na LAAC kutoka kambi rasmi ITENGULIWE, na baada ya hapo mwongozo mpya utatolewa.
Tatu, itumike Kanuni ya 2(2) inayomtaka Spika kutumia Sheria nyingine, Maamuzi ya mabunge yaliyopita, mila na desturi za mabunge, ikiwa kuna jambo au shughuli imejitokeza lakini haijaelezwa kwenye kanuni.
Nauona mkwamo huu ukimalizwa na moja kati ya haya matatu.
Wasalaam.
Kanuni ya 135(11) ya Kanuni za Kudumu za Bunge za June 2020, inasema kuwa " Wenyeviti wa Kamati ya Hesabu za serikali(PAC), na Hesabu za Serikali za Mitaa(LAAC) wanatakiwa kutoka Kambi Rasmi ya Walio wachache Bungeni".
Kwanza kwa Kanuni hizi mpya hakuna kitu kinaitwa Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni, bali imebadilishwa na kuitwa Kambi rasmi ya walio wachache Bungeni.
Kanuni niliyotaja hapo juu inatafsiri kuwa hapawezi kuwa na kamati PAC na LAAC bila kambi rasmi ya walio wachache bungeni.
Na ili iwepo Kambi rasmi ya walio wachache bungeni ni lazima wabunge wa upinzani wafikie 12.5% ya wabunge wote kwa mujibu wa kanuni ya 21.
Mkwamo wa bunge la sasa ni kuwa wabunge wote wa upinzani hawafiki 12.5% ili waweze kuunda hiyo kambi rasmi.
Na kama hawawezi kuunda hiyo kambi maana yake kamati ya PAC na LAAC haziwezi kuwepo kwakuwa haziwezi kupata mwenyekiti aliyetakiwa atoke katika hiyo kambi.
Na bahati mbaya Kanuni hazisemi nini kifanyike iwapo Kambi rasmi haipo, au ikiwa upinzani haujafikia 12.5%.
Je inawezekana Bunge kuendeshwa bila Kamati muhimu na za lazima kama PAC ya hesabu za serikali na LAAC ya hesabu za serikali za mitaa?
Jibu ni hapana haiwezekani. Jambo moja kati ya matatu litatokea.
Moja, hiyo idadi ya 12.5% ilazimishwe ipatikane ili Kambi Rasmi ya Waliowachache Bungeni iwepo ili Wenyeviti wa PAC na LAAC wapatikane.
Mbili, itumike kanuni ya 174 ambayo inatoa uhuru kwa mbunge yeyote, waziri, au mwanasheria mkuu wa serikali kuleta Hoja ya kuomba Kanuni yoyote katika Kanuni za Kudumu KUTENGULIWA kwasababu na malengo maalum.
Maana yake mleta hoja ataomba Kanuni ya 135(11) inayolazimisha wenyeviti wa PAC na LAAC kutoka kambi rasmi ITENGULIWE, na baada ya hapo mwongozo mpya utatolewa.
Tatu, itumike Kanuni ya 2(2) inayomtaka Spika kutumia Sheria nyingine, Maamuzi ya mabunge yaliyopita, mila na desturi za mabunge, ikiwa kuna jambo au shughuli imejitokeza lakini haijaelezwa kwenye kanuni.
Nauona mkwamo huu ukimalizwa na moja kati ya haya matatu.
Wasalaam.