Mkuu wa wilaya Singida aapa kupambana na Tundu Lissu, CHADEMA!

tehe tehe huyo mkuu wa wilaya naona anawazimu anacheza na peoples power eeenh! soon atahamishwa huyo
 
Tunakoelekea ni kubaya zaidi, huwezi himiza watu wachangie michango mbalimbali wakati hali zao zinakuambia nooooooooooooo.
nahisi kama unakuwa unawakejeli vileeeeeeeeee
 
Anafundisha watoto au anahutubia ? hana ubavu wa kushindana na Shujaa Tundu Lisu
 
1.DC-Pachal-Mabiti-2.jpg


Kwanini wanafungua kata shuleni? au wakaazi wa hiyo kata ni wanafunzi na waalimu wao tu!

engmtolera,kweli amevutiwa na habari hii mpaka akafungua jf au ni ushabiki tu! Maana hata upumbavu huu hata serikali yenyewe haijaagiza. Kwanza ela ya mlinzi yupi?polisi au mgambo?au polisi jamii? Ni mbumbumbu pekee asiyependa kumuelewa Tundu Lissu,uyu mbunge alisema hawawezi kuchangia wakati ela inarudishwa hazina kila mwaka. Na ili mbunge alitoa takwimu! Pia mbunge si comedian kusema atakayechangia atashtakiwa!hapana,ila asiyenacho asilazimishwe! Najua uyu dc babu atalaani maana chanzo cha ufisadi kinakatwa mzizi,acha hao matajiri walio pichani ndo wachangie ili ela inayorudi hazina iwe nyingi. Ivi iyo picha babu kapiga amemwangalia mpiga picha alaf wakereketwa wako nyuma yake ina maana babu alikuwa anamhutubia cameraman au ndo kujipanga kupiga picha? Mababu kama hawa nadhan wakatazwe kuiongoza jamii!
 
jm kikweto aliwaambia wauze usara kwenye vyombo vya habar ndo wameanza hivyo,tatizo kaz za kishoga za kuteuliwa hata kama huna uwezo.katiba mpya futa wakuu mkoa,wilaya,manaibu wazir etc ambalo n mizigo kwa taifa na ipunguze madaraka ya rais bila hivyo matatizo kila kona tz.hawana adabu kaz kuiba kura tu hao vimeo
 
Lini anaanza mapambano, na anategemea lini kumaliza hayo mapambano! Tz yangu naililia, kama viongozi wenyewe ndo kabila hii! Tunahitaji kutolala, tuwaong'oe ikibidi hata kwa nguvu.
Mtu ana njaa, hawezi kulitosheleza tumbo lake mwenyewe, unakwenda kumuomba achangiye nini? Nenda ukamwambiye mwajiri wako ashughulike na majambazi ya rasilimali za taifa, fedha za hilo bwawa na hiyo shule utapata in a second.
 
kwanza naishanga sana serikali hii hv unajua huyu mzee ameanza kuwa mkuu wa wilaya muda mrefu sana mimi niko shule ya msingi pale tarime mke wake alikuwa mwalimu amenifundisha darasa la tano kitu kama hicho miaka ya 93 au 94 mpk leo ni mkuu wa wilaya jamani kwani akuna watu wenye haki ya kuwa wakuu wa wilaya kama yeye mpaka leo yeye ni mkuu wa wilaya na kutoa matamko yake ya ajabu hapa ashindwe na alegee fisadi mkubwa huyo kila mahali anapofanya kazi anajenga majumba hana lolote aende zake wananchi wa singida wanamaisha magumu sana alafu anawambia wachange pesa wakati kodi zao ndizo wanazo zitumia kwenye starehe zao.
 
Sasa kama wananchi hao wanakabiliwa na balaa la njaa watachanga nini? siwatumie pesa kidogo walizonazo kujinunulia chakula. Tundu Lisu analaumiwa kwa lipi hapo? Na Mabiti atapambana na Lisu kwa lipi? mbona anachekesha!

hahaah Unaakili sana !"Sasa kama wananchi hao wanakabiliwa na balaa la njaa watachanga nini? " Kama wananjaa , na wanapesa za kuchangia , si wakanunue mahindi ? Jamani Tambwe kaambukiza upupu mpaka wakuu wa wilaya, damn. . ! The gambaz .
 
Hiyo hotuba ni ya wananchi au viongozi wa kata?? Maana wanachokilalamikia na anachowashauri lissu ni kitu kilekile!
 
Hiyo hotuba ni ya wananchi au viongozi wa kata?? Maana wanachokilalamikia na anachowashauri lissu ni kitu kilekile!

nasikia hata darasa la saba waligoma kwenda kumsikiliza, hao ni darasa la kwanza hadi la sita.
 
Huyu Mabiti ndo alikuwa musoma akawapiga waandishi wa habari wakati wanafuatilia mgogoro wa koo,huyu naye ni mtu hatari ni kada wa Magamba mkubwa sana.
 
Kama mnakumbukumbu nzuri huyu Mabiti (Hyenasau mafisi) ni mshatakiwa wa kesi fulani za haki za binadamu huko Serengeti alitakiwa na tume ya haki za binadamu ashughulikiwe kwa kukiuka haki za msingi za raia. Sasa leo anasema awachangishe watu wenye njaa wachange nini. Huyu anatakiwa apelekwe kwa OCAMPO
 
Wanajf huyo mkuu wa wilaya akapimwe akili hawezi kusimama na kuongea upupu mbele ya watoto wale.
kweli serikali ya magamba imefikia ukingoni kung'oka sasa viongozi wanatapatapa tu
 
Pascal mabiti kumbuka huyo Lissu ndiye aliyekuondoa kutoka Tarime wakati ulikuwa ukijifanya nunda kupambana na wangwe sasa sijui umesahau kuwa huyu ni mwingine baada ya kufika huko singida ambako hata yy anatokea kama wewe mwenyewe
Umesahau wakati gari lako limeondoshwa kutoka mahakamani baada ya muda wa kazi kuisha na bado ukiwa mahakamani na gari likiwa linakusubiri nini hasa unachokumbuka labda nikukumbushe tu ulitembea kwa mguu kutoka mahakamani [w]hadi kwako huku kijasho kikikutoka hadi makalioni, ama kweli wewe ni Ngire huwa unatabia za kusahau mapema sasa endelea kukata mti wakati umeukalia
 
Mkuu wa Wilaya ya Singida Pascal Mabiti akizungumza na wananchi wa Kata Mpya ya Lighwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Singida.
Mkuu wa Wilaya ya Singida Paschal Kulwa Mabiti ameahidi kupambana na Mbunge wa jimbo la Singida Mashariki Mhe. Tundu Lissu, kutokana na kile alichodai kuwa Mbunge huyo amewadanganya wananchi wasichangie fedha kwa ajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo katika jimbo lake.

Katika risala hiyo, wananchi pia wameiomba serikali kuwapatia msaada wa chakula ili kukabiliana na tishio la njaa, wajengewe ofisi ya kata, huduma ya maji safi kwa kuchimbiwa visima virefu na kukarabati bwawa kwa ajili ya matumizi ya mifugo yao.
.

Hapo penye red ndio alipotakiwa kutilia mkazo uko kwingine ni "politiki zisizo na maana". Kwanini asi-ape nasio kuapa tu alimalize kabisa tatizo la njaa, that itself would have been enough to prove Lisu wrong. Otherwise hayo mengine hayamsaidii mwananchi wakawaida. Karne hii bado viongozi hawana soln za matatizo ni ubabe tu.
 
huyo mkuu sio kama hajui afanyacho ila anafanya hivyo ili mkuu wake wa kazi amusikie tu. ebu angalia watu anao waeleza mambo hayo wana umri gani na yeye! kama ni kiongoz mwenye busara angeliamuru wanafunzi waende wakasome au waende nyumban lakin yeye kaona wanafaaa kusikiliza hutoba yake. SIJUI TUNAKWENDA WAP WATZ? INASISHIKITSHA!!!!!!!!!!!
 
Nimpe kaushauri kadogo ka akili ya kuvukia road,huyo mteule wa prezidaa,kabla ya kupambana Na Mpiganaji Lissu,apambane na matatizo yanayowakabili wananchi wa eneo hilo atamshinda Mh.Lissu kiulani mpaka bosi wake mtamwamishia wilaya ya Ilala awe anakula nae good time,la sivyo anatimiza wajibu wa desturi yao ya kutoa matamko lakn si utatuzi wa matatizo ya nchi yetu.Ni hayo tu Kulwa na wenzako wenye tabia hiyo.Msipambane na watu pambaneni na matatizo yetu.
 
Hao madenti hawajanywa chai unafikiri wanaelewa kitu hapo?hiki chama changu ntakihama...
 
Kama mnakumbukumbu nzuri huyu Mabiti (Hyenasau mafisi) ni mshatakiwa wa kesi fulani za haki za binadamu huko Serengeti alitakiwa na tume ya haki za binadamu ashughulikiwe kwa kukiuka haki za msingi za raia. Sasa leo anasema awachangishe watu wenye njaa wachange nini. Huyu anatakiwa apelekwe kwa OCAMPO

Huyu ndugu yake Nyani Ngabu hana kabisa kitu naitwa "Community approach",.... nimekuwa nikisikiliza viongozi wengi wa serikali ya Magamba wakiongea na wanainchi wakiwa wanajaribu kushawishi jamii kwa vitisho huku wakionyesha kuwa wao ndio alfu lela ulela, Wasomi na mabosi wa jamii etc bila kufikiria kuwa jamii wanazozungumza nazo zina taratibu za kienyeji kufikia muafaka katika jambo lolote, Hivi na hizo semina elekezi huwa hazitoi elimu hata ya communication skills kwa hawa viongozi?
 
Back
Top Bottom