Elections 2010 Mkutano Wa Hadhara Wa Wana-JF [Online]

Naunga mkono.

Agenda ya kwanza ninayopendekeza ni Jinsi ya Kupambana na ufisadi kwa lengo la kuwa na serkali adilifu yenye usimamizi thabiti na wenye tija.
 
Kwa kweli mwenyekiti... baada ya kufikiria zaidi naona kama itaundwa task force /kikosi-kazi basi kisitumie kodi za wananchi.Fedha zichangishwa kwa harambee, watu wajitolee. Pia siku hizi kuna teknolojia ya mawasiliano - itumike kupata taarifa.Mikutano ifanywe kupitia tele/video conference kupunguza gharama.Tafiti za kwenye internet zifanyike kukusanya data.

Pia wananchi wenye mapenzi mema walioko China na nchi za karibu wanaweza kupewa usihirikiano na ubalozi wetu na kwa pamoja wakakamilisha kile ambacho kingefanywa na Task force na kutuletea taarifa.Mwisho kabisa nadhani maofisa wetu wa ubalozi wanaweza kutufanyia kazi hiyo maana ndio wanatuwakilisha huko.

Nakubaliana na wewe WoS. Kwa mamlaka niliyopewa . . . Ooops! Niliyojipa, naomba nikuteue uwe mwenyekiti wa kamati teuli ya JF juu ya suala zima la hukumu ya kifo litakalokuwa na hadidu rejea zifuatazo:
  • Kuangalia ni makosa gani ya Kifisadi na kuhujumu uchumi ambayo yatastahili adhabu kali
  • Kujifunza kutoka kwa wenzetu Wachina ni nini hasa wanafanya na nini tunaweza kuiga katika kazingira yetu
  • Kupata maoni ya Watanzania juu ya ama kuwe na hukumu ya kifo ama la kwa watakao hujumu uchumi na kama la basi adhabu mbadala iwe ipi
  • Kuangalia uwezekano wa kuwa na mahakama maalumu itakayoyoshughulikia kesi za uhujumu uchumi na ufisadi kwa haraka badala ya ile ya kisutu ambayo miaka sasa kesi haziishi
  • Na mengineyo ambayo kamati itaona yanafaa
Unatakiwa uteue wanakamati 3 na uzingatie uwiano wa kijinsia na weledi. Report kamili iwe tayari siku ya Jumamosi kabla mkutano haujaisha.

Kuhusu masurufu na pesa ya safari, mnaruhusiwa kuendesha harambee na kuchangisha toka kwa wote wenye mapenzi mema.
 
Naunga mkono.

Agenda ya kwanza ninayopendekeza ni Jinsi ya Kupambana na ufisadi kwa lengo la kuwa na serkali adilifu yenye usimamizi thabiti na wenye tija.

Nimekusoma Mimi baba.

Hoja yako makini itazingatiwa katika majumuisho yaliyotolewa.

Je una kipaumbele chochote kingine katika sekta yoyote?
 
kipaumbele kiwekwe kwenye ELIMU BORA na sio BORA ELIMU, na tungeanzia kwa wawakilishi wetu(wabunge) walau wawe na Shahada ya kwanza, ili kuwawezesha kujadili miswada kwa kina kwa faida ya Taifa
 
Asante sana Kijana wetu Kiby,

Hakika unaonyesha una uchungu sana na Nchi hii ya Maziwa na Asali . . . .

Kwa hiyo unachosema ni kuwa "Kiongozi Wa Kuchaguliwa Atakayepatikana Anahujumu au Kuifisadisha Mali ya Taifa, Anyongwe Hadharani Mpaka Afe"?

Sasa hapa pana mgogoro kidogo? hatutakuwa tumevunja haki za binadamu? Wanaharakati mnasemaje kwa hili?

Kuna mfano wowote wa Nchi wanaofanya hivi?

.
Ee ipo nchi inafanya hivyo. China fisadi yeyote anaefisadi kwa kuhujumu uchumi anauawa hadhadhani mpaka kufa. Na mara nyingi huku kwetu utawasikia viongozi wakiyasifia maendelea ya haraka ya china bila kujua kwamba yanasababishwa na sheria kali zilizopelekea viongozi kuheshimu maadili ya uongozi. Kuhusu haki za binadamu ni kwamba sheria ya maumbile inaongozwa na kanuni ya uhai ambayo ni, ili kuwe na uhifadhi wa uhai ni lazima viumbe wengine wafe kwa ajili ya vingine. Sisi tunaishi kwa sababu wapo samaki, mbuzi, kuku, ngombe nk waliokufa. Na kama ukosefu wa maji, umeme, dawa, makazi bora nk vimesababisha walalahoi wengi kufa kisa ni mmoja au wachache wamefisadi pesa na miundombinu, kwa nini wasife ili kunusuru jamii ya walio wengi? NINACHOMAANISHA HAPA NI 'HAKUNA HAKI YA MTU MMOJA IKIWA HAKI HIYO INADHULUMU HAKI ZA WALIO WENGI. Mratibu mie bado nasisitiza tena nisiposikilizwa kakhyanani ntavuruga mkutano!!
 
Nakubaliana na wewe WoS. Kwa mamlaka niliyopewa . . . Ooops! Niliyojipa, naomba nikuteue uwe mwenyekiti wa kamati teuli ya JF juu ya suala zima la hukumu ya kifo litakalokuwa na hadidu rejea zifuatazo:

  • Kuangalia ni makosa gani ya Kifisadi na kuhujumu uchumi ambayo yatastahili adhabu kali
  • Kujifunza kutoka kwa wenzetu Wachina ni nini hasa wanafanya na nini tunaweza kuiga katika kazingira yetu
  • Kupata maoni ya Watanzania juu ya ama kuwe na hukumu ya kifo ama la kwa watakao hujumu uchumi na kama la basi adhabu mbadala iwe ipi
  • Kuangalia uwezekano wa kuwa na mahakama maalumu itakayoyoshughulikia kesi za uhujumu uchumi na ufisadi kwa haraka badala ya ile ya kisutu ambayo miaka sasa kesi haziishi
  • Na mengineyo ambayo kamati itaona yanafaa
Unatakiwa uteue wanakamati 3 na uzingatie uwiano wa kijinsia na weledi. Report kamili iwe tayari siku ya Jumamosi kabla mkutano haujaisha.

Kuhusu masurufu na pesa ya safari, mnaruhusiwa kuendesha harambee na kuchangisha toka kwa wote wenye mapenzi mema.


Mwenyekiti..uteuzi huu ni batili..huna mamlaka ya kujipa ujiko wa uenyekiti..kwa msingi huo huwezi kuniteua.Teuzi hizi nazo zinafanya kazi nzima iwe batili
 
Katika katiba mpya, swala la "balance and checks" liangaliwe kwa makini. Vyombo vya kusimamia maadili viwajibike kwa bunge na sio kiongozi wa Serikali mf. PCCB, Mawaziri wasiwe wabunge, wabunge wasiwe na majukumu ya executives...kama kuongoza bodi za mashirika
 
Mi naomba atakayechaguliwa kwanza atuambie hadhi ya Zanzibar ni nchi ama si nchi?:confused2::confused2:
 
Mi naomba atakayechaguliwa kwanza atuambie hadhi ya Zanzibar ni nchi ama si nchi?:confused2::confused2:
Jibu lilishatolewa....ina maana hadi sasa tulishapewa position ya serikali kuwa Zanzibar siyo nchi... ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano....( japo hata mimi bado nachanganyikiwa maana kama ni sehemu ya Muungano, na hapo hapo ina rais wake, bendera yake, Baraza lake la wawakilishi etc...inakuwaje, lakini coercive instruments of the State kama polisi, jeshi, etc hawana vya kwao)
 
Jibu lilishatolewa....ina maana hadi sasa tulishapewa position ya serikali kuwa Zanzibar siyo nchi... ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano....( japo hata mimi bado nachanganyikiwa maana kama ni sehemu ya Muungano, na hapo hapo ina rais wake, bendera yake, Baraza lake la wawakilishi etc...inakuwaje, lakini coercive instruments of the State kama polisi, jeshi, etc hawana vya kwao)

Sawa WoS,

Kilichonisukuma kusema ivo ni kwamba, majuzi hapa tumeona wamebadili katiba yao, kudefine eneo la Zanzibar na pia kumpokamadaraka Rais wa Jamhuri ya Muungano ya kugawa mikoa na kutea wakuu wao

hii inaashiria kuwa Zanzibar ni nchi ijapokuwa katiba inasema Tanzania inaumuisha eneo lote la znz na iliyokuwa Tanganyika....

Huenda pia tukahitaji kuchakachua concept ya taifa, nchi, na dola, lakini napatga mashaka kuwa aidha ZNZ wamechakachua mambo au siye katiba yetu ilichakachua mambo kinyume na artcles of the Union za 1964.

vyovyote tunahitaji mtu atayakeweza kutatua hili suala once and for all
 
Mimi nashauri ipatikane tume huru ya uchaguzi ambayo haitachaguliwa na rais wala kuwajibika chini ya utawala ulio madarakani.

Twahitaji tume itakayochaguliwa ithibitishwe na bunge na kuwajibika kwa bunge.
 
1) Hakuna kiongozi yoyote kutibiwa nje ya nchi kwa gharama za serikali-Itasadia kuboresha hospitali zetu.

2)Marufuku kwa serikali kununua vitu nje ya nchi ambavyo vinaweza kupatia hapa hapa nchi,mfano samani.

3)Mikataba na matumizi ya serikali iwe kwenye public domain, mfano safari za rais.
 
Hii JF ya wannandugu nini? maana Asubuhi hii nimetuma post yangu kuwa nimefungua tu naona meseji hii ikisema mkutano wana JF online sasa nikatuma meseji sawa mpka sasa nikifuatilia siiioni Je Mods ameifuta au nini.
 
Naomba majibu ndani ya masaa sita yajayo alaa Mods acha ubaguzi sisi tupo mstari wa Mbele kupinga Ufisadi kumbe wewe unausapot na kuuleta huku
:fencing:
 
Vipi kuhusu wanaotia na kutiwa mimba ,zaidi likihusishwa na madenti ,Ili suala watalitatua vipi kwani kusema kweli hali inatisha haina tofauti na ujambazi.

 
Last edited by a moderator:
M/kiti mkono wangu nimenyoosha mda mrefu bado naona siruhusiwi, basi napora mike kinguvu kwani haki haiombwi bali inachukuliwa.
Katika katiba mpya pia napendekeza iwe ma marufuku kama hivi:-
Ni marufuku mtu/taasisi/kampuni kutoa misaada kwa mtu mmoja mmoja, mfano kumpa kiroba cha unga, bati,sment, pocket money nk,labda iwe tu ni kwa dharura. Badala yake misaada itaelekezwa kwenye vikundi/taasisi ili kuwezesha miundombinu inayoweza kuharakisha maendeleo endelevu katika sector zote.
-Ni marufuku kwa kazi ya siasa kulipwa mshahara. Badala yake itakuwa ni kazi ya kujitolea na kitakachotolewa ni posho ya vikao tu. Mishahara minono na yenye kushawishi itaelekezwa kwenye ajira za kitaaluma ili kuepusha taaluma kukimbiwa na kusababisha taifa lisilozalisha ila kupiga domo mda mwingi.
-Ni marufuku watendaji wa serikali mfano wakuu wa mikoa/wilaya nk, kujihusisha na siasa. Kwa kuwezesha hili wasiteuliwe na rais badala yake wachaguliwe na wananchi na kuwajibika bungeni.
 
Leo ni siku ya pili yaa mkutano wetu hapa jangwani . . .

Mratibu wa Propaganda na Uenezi wa JF naona ndiyo anaingia hapa. Watu wameshaanza kumiminika . . .

Bila kupoteza muda naomba sasa niwakaribishe tena kuweza kutoa maoni yenu.
 
kipaumbele kiwekwe kwenye ELIMU BORA na sio BORA ELIMU, na tungeanzia kwa wawakilishi wetu(wabunge) walau wawe na Shahada ya kwanza, ili kuwawezesha kujadili miswada kwa kina kwa faida ya Taifa


Mujuni hoja yako ina mantiki na tunaiweka katika vipaumbele, kwamba Chama kitakachoingia madarakani kiweze "Kuleta na Kusimamia Elimu Bora" na si bora Elimu.

Vipi kuhusu hali ya maisha ya Watanzania?
 
Back
Top Bottom