Mkutano wa CHADEMA viwanja vya NMC Arusha

Mkutano wa CHADEMA viwanja vya NMC Arusha

Kuna mtu anaonekana kanyanya kadi ya ccm.
Wengi wanarudi kundini
 
Nasikiliza Arusha mambo hapa LIVE, kuna ngoma zinagongwa kinyama hapo NMC..

HIP HOP concious za ukweli!!

Lol!! Kama niko Arusha aisee!!

Mie nilikuwa nadhani kuna mkutano kuwaleza wananchi kuhusu hali ya uchumi wa Tanzania kumbe kuna Disco vumbi.
 
Kinachoendelea ni burudani za jukwaani tukiwasubiri viongozi wa kitaifa; kijana mmoja 'anachana verse' na 'songi' lake 'ujumbe wa sauti/voicemail' kuhusu ugumu wa maisha;
watu wameburudika kiasi cha kuomba arudie!

Sasa ng waheshimiwa madiwani wanawasalimu wananchi!
 
Muda wa madiwani kuwasalimia wananchi.
Anazungumza Chrispine Tarimo diwani wa Sekei

Anasema CDM waliahidi watakapoingia madarakani watabadilisha katiba.
Hatukupata rais tukapata wabunge, na sasa tunapata katiba.

Mazingira ya jiji ni machafu, bajeti imetengwa kwa ajili ya usafi wa jiji matokeo yake pesa zile zimetumika vibaya
 
saafi sana peoples power mkimaliza hapo shukeni kusini kusini kama songea peramiho mbinga nyasa namtumbo na tunduru
 
azimio la arusha lilianzia arusha azimio la cdm kuchukua nchi litaanzia arusha pipoz pawa
 
Madiwani wanakaribishwa kutoa salamu!!

Diwani kata ya Sekei Mh Chriss, anawashukuru kuja kuvua magamba!

Tumshukuru Dr. Slaa kwa kutimiza ahadi, kwani ilani ya CDM ilisema mchakato wa katiba utaandaliwa ndani ya siku mia!!

Kwa hiyo ni heko kwa wabunge wa CDM kusimamia hili mpaka sasa katiba inaanza kushughulikiwa!!

Suala la usafi, jiji la Arusha limepewa hati chafu tokana na uongozi mbaya uliopo wa Harimashauri!!

Kuamisha wamachinga ni lazima waandaliwe mahala pa kwenda ndio waondolewe katika maeneo waliopo sasa!!
 
Wale watu Milioni 1 tayari wameishachukwa kadi za Chadema? Tupeni Updates mliopo Arusha.
 
Baada ya mbunge kuondoka waliitisha kikao cha dharura madiwani wa CCM bila kuwashirikisha madiwani wa CDM na kuunda kamati inayosimamia mfuko wa jimbo unaotolewa na bunge!!

Sasa anafuata Mh. Sabina!! Viti maalumu!!

Tunasalimiana kwa waiper, kunja ngumi usiogope asikari, CCM wala Kikwete!!

Pipoooooooooz!!

Kikwete amechemsha na tutahakikisha tunapiga kelele mpaka kieleweke!
 
huyu mtangazaji amesema lazima hao wahuni walioanzisha mfuko wa mbunge bila kushirikisha madiwani wa chadema lazima wavue gamba kama Mawazo alivyovua gamba akavaa gwanda.

Huyu Mawazo ni nani?
 
Anazungumza Diwani Sabina Francis.
''wabunge wetu wamefanya kazi nzuri, lakini Kikwete amechemka.
 
Natamani sn kufika,ila nipo mbali.Ile sayansi ya kiafrika huwa inatumika usiku tu?maana nasikia huwa ni usafiri wa fasta kama air41 ngoja nimcheki mmagamba 1 aniekekeze fundi mkali,maana wenyewe wanawatumia sn.KUNA KIPINDI HATA IKULU ILIKUWA INA MTAALAM MAALUM WA AINA HII.

nimeipenda hii hapo mwisho.
 
Tunafahamu wenzetu wamfukuzwa na kulikuwa na ugomvi pata shika. Yule Meya anfanya mambo ya ajabu..

Wamesema wanaajiri vijana lakiniajira hizo zina nepotism kubwa tunafuatilia ni vijana gani halafu tutakuja kusema hapa!!

Mwaka jana ilikuwa bajeti Bil 48, ila kuna watu wana risiti feki nyingi na zinachukuliwa na viongozi wa halmashauri..

Ukilipa ada yoyote halmashauri ni lazima uangalie kama risiti ina muhuri wa halmashauri!!

Anayekusanya ushuru wa magari, analipisha watu mara nyingi kwa siku, huyu mtu hajapitishwa katika baraza na Meya ansema hafahamu!!
 
Diwani wa viti maalum Arusha Mjini anaeleza jinsi Halmashauri inavyopoteza mapato kwa kutengeneza vitabu 'feki' vya risiti; bajeti ya jiji imepanda toka bil 48 hadi bil 56 lakini vyanzo vipya vya mapato havionekani!
 
uwanja umejaa tope kutokana na mvua vinazoendelea kunyesha sehemu mbalimbali...
 
Ritz acha upumbavu bana. Aliyesema watu mil1 ni gamba mwenzako, sasa unajifanya haumjui. Tena nadhani yule jamaa anaweza kuwa wewe
Wale watu Milioni 1 tayari wameishachukwa kadi za Chadema? Tupeni Updates mliopo Arusha.
 
Back
Top Bottom