Nimesoma na ninaelewa vizuri, sio nijifunze kusoma na kuelewa. Unaposema kuwa kawaamsha wasukuma wenzake unajidanganya coz hata mkutano wake mmoja alioufanya Didia na Mbugani nilikuwepo na anachoweza jukwaani sio kunadi sera zake bali kuendeleza malumbano mara ya ZZK na CC, mara CCM imefanya vile badala ya kutushawishi atafanya nini yeye kama yeye. Kura za kupigiana kisa ukabila na uchama zishapitwa na wakati na hakuna mtu anaemuita aende kugombea kwenye hayo majimbo 9 unayosema labda ni wapiga debe wake ndo wanamlaghai ajaribu kugombea.
Tusijaribu kupigia kura mtu kwa kuangalia chama, kumbuka hata huyu Mawazo mwanzo alikuwa CCM na watu walimwamini wakamchagua sio kwa vile ni mgombea wa CCM bali kwa vile aliweza kuwashawishi kwa sera zake. Unaposema kwamba hakuna mwanasiasa yeyote wa CCM anayeweza pambana naye unakosea coz watu wanachoangalia ni uwezo wa mtu.
n way tuachane na hayo man chester amefungwa ngapi?
ulikuwepo mbugani ipi? mawazo anakubalika toka Nyang'wale,Buchosa,Sengerema,Misungwi,Magu,Busega,Bunda,Maswa nk.Nakumbuka tulipiga naye kazi katika uchaguzi mdogo Magu tukachukua vitongoji,mitaa na vijiji kibao ukuwemo mtaa wa Bank-Magu yalipo makao makuu ya ccm wilaya!