Mkutano soko kuu Mtwara- muendelezo wa gesi.

Mkutano soko kuu Mtwara- muendelezo wa gesi.

Lkini,kwa mujibu wa VUTA-NKUVUTE aka Mzee Tupatupa,hao watu wanaandaliwa adhabu na CCM...nchi hii sasa imekuwa Comedy tupu
 
Last edited by a moderator:
Hoja yao ni gesi ianzie kutumika Mtwara kwanza kabla ya kupelekwa popote ndani au nje ya nchi.

Wanauliza kwanini ichimbwe Mtwara halafu ipelekwe Dar/Bagamoyo kwanza na sio kubaki Mtwara kwanza?

Kwa hiyo wao wanachotaka wawe wa kwanza kuituia? Hoja ya ajabu hii..Kwani ikiletwa Dsm wao wameambiwa hawatapata gesi?wameambiwa watakua wa mwsho kutumia?..sasa wanasema gesi ibaki mtwara sasa maana ya hiyo nishati kupatikana ni nini kama haitasambazwa kwa watanzania..
 
Hapa kuna hamasa kubwa sana, wanasema km nchi ni ya kilimo na serikali inasema dsm inatoa mapato asilimia 80 je dsm kuna kilimo gani?

Kuna mbunge mmoja aliwahi kuropoka hivyo hivyo, eti DSM ndo inaingiza pato kubwa nchini! Wanuza maji ya chumvi?

Rais naye anaonekana hajuo afanyalo. DSM inaweza kuwa ndo inalipa kodi kubwa nchini lakini nchi hii haiendelei kwa sababu ya kodi. Forex zinazoingia nchi hii zinatokana na utalii na madini. DSM hakuna madini, yako kanda ya ziwa. Utalii uko kanda ya North, Arusha & Moshi. Kilimo cha biashara hakiko DSM, ni mikoani, Shinyanga, Rukwa, Iringa, Arusha, etc.

Sasa hiyo DSM inaleta kitu gani? DSM ina wafanyabiashara wanaosubiri bidhaa toka miokoni, basi!

Hebu tusiwe nchi ya wajinga. Wasiojua hata umuhimu wa kila sehemu ya nchi.
 
Serekali yetu ifanyejuhudi za makusudi kusikiliza kilio cha wananchi wa mikoa ya kusini, historia inatuambia kwamba eneo hili wamekua nyuma kimaendeleo kwa kipindi kirefu sasa walitegemea GESI ingekuwa kigezo cha kufungua mipango mingi ya maendeleo,sipendezwi na majibu mepesi yatolewayo na viongozi wetu kutokana na maswali magumu wanayo uliza wananchi..
 
nimeanza mchakato na upenguzi yakinifu wa kubadili uraia wangu kutoka mwanaMara kuwa Mtwaran, Mjerumani alifanya makosa kuingia Mtwara, JK anarudia makosa yale yale!!!
 
Nahisi harufu ya damu inanukia Mtwara! Siku si nyingi.
 
nimeanza mchakato na upenguzi yakinifu wa kubadili uraia wangu kutoka mwanaMara kuwa Mtwaran, Mjerumani alifanya makosa kuingia Mtwara, JK anarudia makosa yale yale!!!

Hapana mkuu usitukimbie wana Mara bali tukawaelimishe wana Mara wenzetu nasi tusiwe nyuma kwenye maswala ya maendeleo ya Musoma na Mara nzima...haiwezekani wazungu wanafaidika tu sie tunauliwa....
 
wale wanaodhani hii kitu ni masihara
time will tell them,
hii gesi italeta maafa nawaambia
 
Kweli nimeamini usimwamshe alie lala. Kusini wameanza kuamka baada ya ccm kula kwa ulafi na bila kunawa.UOTE=suleym;5386187]Hapa kuna mkutano agenda kuu ni kuhus kusafirisha gesi kwenda dar es salaam hapa wanasema kikwete amechokoza moto hawata rudi nyuma. wanasema gesi haitoki liwalo na liwe. nawasilisha. na zaidi wanamlaani hawa ghasia wanamwita msaliti.


View attachment 78366View attachment 78369View attachment 78375View attachment 78378View attachment 78379View attachment 78380View attachment 78381[/QUOTE]
 
salam zimfikie
jeikei
muhongo
membe
ghasia
mkuchika na chikawe
ukombozi tutauleta sisi wenywe
 
Uraia wa wananchi wa mtwara unatia shaka, sauti yao na maoni yao ni haki yao na ni muhimu ila sura ya madai yao yanazidi kuacha maswali yenye majibu wasiyoyataka kuyasikiliza..nasikia huko Mara nao wanaandamana kutaka madini yao ya nyamongo waachiwe...hakuna hoja gas iletwe Dsm.

u must be so so dull and dumb
 
Wanaoratibu mikutano hii wawe wazi kwa Wananchi,haiwezeakani gas isiende Dar ila la kupigania hapa ni kuwa kabla haijaenda angalau serikali ihamasishe wawekezaji walete viwanda Mtwara,Lindi.
Angalia Kilwa,gas imekwenda Dar lakini la maana walilopata ni kuwekewa umeme toka kituo kidogo cha Somanga.
Kwanini pasingejengwa hata kiwanda kidogo cha cement na kuboresha bandari.
Serikali itoe vivutio kwa wawekezaji ili kusini pawe na maendeleo.

We mwenyewe u-shuhuda wa yaliyo wakumba watu wa KILWA(Mh MIGNON -acha kushabikia jani lenye sumu),Sheli-kali imekataa umeme kufuliwa MTWARA ipeleke VIWANDA VINGINE yakuingia akilini?,Usha ambiwa viwanda ni BAGAMOYO,na HATAna mpango ni gesi baadae itapelekwa viwandani BAGAMOYO na sio viwanda vije MTWARA.
USHAURI:
- - - - - - -MTWARA -komaeni tena fanyeni mikutano mara kwa mara,BEN aliwatosa,GASIA nae kawatosa,yaonesha JANI LA TUMBAKU si wenzenu hata kidogo wao wako zaidi ki-10%.tupo nyuma yenu full sapoti,umeme ufuliwe MTWARA kisha usambazwe nchi nzima.KWA nini sifa hii ihamie DAR?,ufisadi DAR,bara bara DAR,Bandari DAR, na GESI pia ije DAR...?haiwezekani hii ni ya CHINGA MEN...
 
Lkini,kwa mujibu wa VUTA-NKUVUTE aka Mzee Tupatupa,hao watu wanaandaliwa adhabu na CCM...nchi hii sasa imekuwa Comedy tupu

Ukimwazibu leo nae atakuvizia aku adhibu na hapo ndo itajitokeza definition ya terrorist yaani vita/mashambulizi ya kuvizia,ACHENI MTWARA iwe GAS-CITY tamaa za BAGAMOYO za nini kama CHINGA Kashtuka kubalini yaishe.
 
Wanaoratibu mikutano hii wawe wazi kwa Wananchi,haiwezeakani gas isiende Dar ila la kupigania hapa ni kuwa kabla haijaenda angalau serikali ihamasishe wawekezaji walete viwanda Mtwara,Lindi.
Angalia Kilwa,gas imekwenda Dar lakini la maana walilopata ni kuwekewa umeme toka kituo kidogo cha Somanga.
Kwanini pasingejengwa hata kiwanda kidogo cha cement na kuboresha bandari.
Serikali itoe vivutio kwa wawekezaji ili kusini pawe na maendeleo.

KILWA UKIACHA UMEME KUTUMIKA MANYUMBANI,PIA KUNA VIWANDA VIDOGO2, PIA KUNA KIWANDA CHA SARUJI KINATOA SARUIJI INAITWA KILWA CEMENT AMBAYO INATUMIKA KUSINI KUTOKE,HALAMASHAURI INAPATA KARIBU MIL 100 KILA MWEZI KUTOKANA Na gas..... UKIANGALIA KIUCHUMIA KWA KILWA GAS IMEWANUFAISHA WANANCHI HUSASANI KWA BIASHARA ZINAZOTUMIA NISHATI YA GAS.......
 
Wananchi wa kanda ya Ziwa 2010, wao walifanya kweli kupitia sanduku la kura... so Mtwara na Lindi fanyeni kweli 2015
 
KILWA UKIACHA UMEME KUTUMIKA MANYUMBANI,PIA KUNA VIWANDA VIDOGO2, PIA KUNA KIWANDA CHA SARUJI KINATOA SARUIJI INAITWA KILWA CEMENT AMBAYO INATUMIKA KUSINI KUTOKE,HALAMASHAURI INAPATA KARIBU MIL 100 KILA MWEZI KUTOKANA Na gas..... UKIANGALIA KIUCHUMIA KWA KILWA GAS IMEWANUFAISHA WANANCHI HUSASANI KWA BIASHARA ZINAZOTUMIA NISHATI YA GAS.......

Yani Mil 100 wenyewe mmeona mnapata? Kweli mjinga mjinga tu!
Badala ya kukoma wajenge mashule , mahospitali na miradi mingine yenye faida nyie mnashangilia 100 Mil. Hii mbona ni ushuru wa wiki tu Pale Ubungo Terminal?
 
Back
Top Bottom