Mkurugenzi wa Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere, kwanini usijiuzulu?

Mkuu ukifika International Airports eg. Schiphol hawanaga huo muda. Kama haupo utajipanga. Nilishawahi kuachwa na ndege huko Schiphol nikiwa na boarding pass tayari.
NB: ndege inabeba watu 400 wakatafute mzigo wako wakaushushe kisa umecheck-in?
Ama watakutafuta abiria upande ndege au watashusha mzigo wako. Kwa ajili ya usalama wa abiria, hawawezi kurusha ndege na mzigo wa abiria ambaye hayumo kwenye ndege husika!
 
Nasema hivi, Sijiuzulu Ng'o.

Hivi wewe katika vitengo vyote vya mamlaka za Serikali umeona hichi changu tu? Binti mbona una nongwa sana wewe?

Niambie ni mamlaka gani iliyoko chini ya Serikali hii ambayo wewe unaona kila kitu kiko perfect mpaka uje uiseme hii ya kwangu? Yaan ushaenda Bandari, TRA, TBS, Ewura, Latra, Sumatra, Tanesco, Dawasco au ATCL, Mifuko ya Jamii, etc ukaona utendaji wao mpaka uje useme eti nijiuzulu?

Na nikijiuzulu nikakosa mshahara nitakula Nini? Utanisaidia kulisha na kusomesha Watoto wangu? Nijiuzulu ili nikose posho na marupurupu ya vikao na Safari mbalimbali ambazo zingine najitungia mimi Mwenyewe?

We unavyoniambia nijiuzulu utanipa wewe VX ya kutembelea? Unaona wivu sana navyoweka kishoka nikiwa naendeshwa kurudisha au kuchukuliwa nyumbani ee? Au utanipa wewe Allowance ya Nyumba ingawa naishi kwangu?

Wewe nani umemuona wa Level ya Mkurugenzi amejiuzulu kwa tumakosa tudogo tudogo kama hutu mpaka uje uniambie Mimi pia nifanye hivyo? Na nikijiuzulu nani ataniita Boss? Au unadhani sipendi sifa za kuitwa Boss? Unadhan sipendi kunyenyekewa?

Unajua hata nimehangaika vipi kupata hichi cheo mpaka uje useme kirahisi tu kua eti nijiuzulu? Usitake nitoe siri zingine za ndani mpaka leo unaniona niko hapa, lakin nakuapia kwa sababu ulizozitoa mimi kujiuzulu hiyo sahau.

Mambo ya hizi taasisi zetu hayaendi kiholela kama unavyodhani. Lazima ufanyike upembuzi yakinifu, iitishwe tenda, apatikane mzabuni, afanyiwe vetting kupitia vikao mbalimbali ambavyo vitahitaji gharama mbalimbali kama vile posho ya kikao, refreshments, ukumbi, etc, ipatikane bajeti ya huo ukarabati n.k. Hivi vyote vinahitaji muda na fedha ili tufanye kwa umakini zaidi.

Sio unakurupuka tu eti nijiuzulu.
Fala kweli wewe🤣🤣🤣🤣
 
Lango la kuingia nchini linapokosa mtu makini lawama na kudumaa Kwa huduma lazima kuwepo; Kwa kipindi kifupi toka kuzinduliwa Kwa terminal 3 madhaifu yafuatayo yapo wazi na Kila msafiri makini anayaona.

1. TV zinazoonyesha ratiba ya safari terminal 2 zimeondolewa, hivyo hakuna sehemu unapata huduma yakutambua ndege Yako inaondoka saa ngapi au mpendwa wako anaingia saa ngapi.

2. Spika za matangazo hazifanyi kazi au matangazo ayatolewi Kwa mujibu wa sheria na taratibu kama viwanja vingi vya Kimataifa vinavyopaswa kufanya kazi.

3. Kukosekana Kwa matangazo na kuondolewa Kwa tv za matangazo kumepelekea wasafiri wengi kukataliwa kusafiri Kwa kuambiwa geti zimefungwa na wanapolalamika mbona walikuwa uwanjani awapewi msaada.

4. Hakuna mtu anayesimamia huduma za precision na air Tanzania, watoa huduma wapo too slow lakini pia wanarundikana kaunta wakipiga stori huku wateja wapo Kwenye foleni.

5. Nimesafiri mara kadhaa mwaka huu kila ukiingia uwanjani usipokutana na abiria wanalalamikia huduma za air Tanzania utakutana na lawama kwenye ndege. Inaonekana wapo baadhi ya wafanyakazi wa air Tanzania wanatoza wasafiri fedha kinyume na tiketi zao,au wapo wahudumu wanakataa kuwahudumia wateja Ili wawalipishe tiketi upya na wapewe commission na shirika au wapo watu wanaoshindwa kuwajibika kutoa taarifa SAHIHI Kwa wateja nk naamini Kuna uzembe

6. Hakuna siku nimewahi kusafiri na air Tanzania nikaona wahudumu wao wakitafuta wateja ambao walifanya booking wakalipia lakini awajacheck in; ukienda viwanja vyote vikubwa lazima uone wahudumu wa mashirika ya ndege wakitembea Hadi nje ya uwanja kutafuta abiria ambao awajacheck in . Hapa Kwetu utadhani tuna laana; muhudumu kuangalia system na kutoka kutafuta abiria kabla yakufunga kaunta hakuna na hapa Nadhani ndipo Dili linapofanyika. It's like wapo tayari ndege iende na watu wawili lakini waache abiria au wawakatishe tickets twice.

Haya na mengine mengi yanakufanya ujiulize msimamizi wa Uwanja huu yupo serious? Anafanya ukaguzi-? Wageni kutoka nje hasa wanaokwenda kwenye utalii kaskazini wanalalamikia hizi huduma zetu sijui anasikia? Spika inacost shilingi ngapi? Mtoa matangazo Kwanini asiwajibishwe? Huyo aliyetoa screen anasubiri Nini ofisini? Air Tanzania Kwanini wahujumu shirika Kwa huduma mbovu wasiwajibishwe? Don't you have standards? Wageni wanaposikia makelele uwanjani mnajisikiaje? It's shame mjue? But why everyday mnarudia same mistakes? Je, hakuna CCTV camera zakuonyesha ubovu wa watoa huduma?

Naamini terminal 3 Haina Muda nayo itakufa Kwa sababu mentality ni zile zile; mkurugenzi Toka ofisini angalia miundombinu ya uwanja inavyohudumiwa lakini pia angalia watoa huduma sidhani kama wanakutakia mema.

Contrary basi tutaanza kuamini mnamhujumu mama Kwa Sasa yule Mzee amkumfanyia haya; mnataka air Tanzania ipewe jina baya ikose abiria Jambo ambalo Lina tija Kwenu ila halina tija Kwa Taifa.

Roho wa Mungu akuongoze uwekeze Kwa watoa taarifa wanaokuambia nini kinafanyika hapo uwanjani kwako; Hali si shwari.
Ona baadhi ya Watanzania wasivyo makini! Mwanzisha uzi huu anazungumzia suala la maana wao wanaleta maneno ya upuuzi. Tukiita Uswahili wanasema tunatukana! Kwa hakika huduma kwenye ofisi nyingi za Umma si jambo la kujivunia. Ukiona Rais anajihusisha na kutangaza watalii waje Tanzania wakati Watanzania hatujafikia viwango vya kimataifa vya huduma ndipo unapomwonea huruma Rais wetu maana anafanya kazi bure. Watalii wanakuja Tanzania sababu ya wanyama na nchi yetu ilivyoumbwa na si kwa sababu ya huduma nzuri. Wengi wa hao watalii wakija Bongo mara moja hawaji tena na pia wanawaambia wenzao wasije kwa sababu ya maudhi ya huduma. Hapo hujazungumzia taxi services na taarifa zao za kumsaidia mtalii/mgeni hapa kwetu! Tukielewana hapo ndipo tutaanza na nini tuanze nacho ili tuweze kuwa na biashara yenye faida na ya kudumu.
 
Ni lini malalamiko Tanzania yameisha....??

Wakitekeleza yote, ikifika uchaguzi wataombea kura kitu gani.....

Serikali kazi yake ni kutengeneza matatizo na kuyatatua ili iendelee kubaki madarakani... Hzo TV walizotoa wakizirudisha utakuja kuona wana Lumumba wanakuja kusifia humu

Hovyo sana...
 
Nenda uone uchafu uliopo kwenye vyoo vya nje vya terminal two. Pale ndo lango la nchi. Kwa mtu aliyeweza kuingia vyoo vya Schippol Airport ya Uholanzi kwa ajili ya kujihifadhi utasikitika sana ukilinganisha na vyo vya JNNIA. Hii ni aibu kwa nchi.
 
Consistency kwa mwafrika ni msamiati mgeni sana, hushangai mwendokasi tu mpk leo tiketi zinachanwa badala ya scanners kukagua.

Mfano rahisi; kama ulikulia pahala choo ni kwenda vichakani, mara nyingi yale maisha utajikuta unaendelea nayo hata kama si 100%
Uko sahihi kabisa mkuu kwa huo mfano wa mwendokasi. Sasa hivi hata kuandika kuwa bus linakwenda wapi wameshindwa. Gari ikifika kituoni abiria wliopo wanaanza kukuliza abiria walioko ndani kuwa bus hili linakwenda wapi, au dereva anatoa kichwa nje na kuanza kuwaambia abiria walioko kituoni kuwa bus linaenda kivukoni au Gerezani. Kwenye vituo vingine wameandika sehemu za kusubiria bus za Muhimbili, Morocco na Kimara, ila vituo vingine hakuna bango lolote. Kimara terminal mabango hayaakisi ukweli.
 
Hii NCHI ndio maana yule MZEE alikuwa anatupeleka mchakamchaka, alijua wazi kuna SHIDA kubwa somewhere.

Leo kila kitu kimesimama kila sehemu shida watu wapo busy kutafuta MABAYA ya mzee MAZURI hayazungumzwi.
Ni kwa sababu mabaya yake ni mengi kuliko mazuri. Jiwe alikuwa muuaji.
 
Mkuu umeongea kwa uchungu sana, huu sasa ndiyo uzalendo.

Mamlaka husika kama mmepitia uzi huu chukueni hatua.

Ilifikia mahali eti mpaka vyeti vya Covid-19 navyo ni dili pale uwanjani.
Kuna siku mwaka jana mwishoni jamaa yangu kabisa anafanya hapo terminal 2 nilimwomba msaada wa kupata cheti cha yellow fever bila kudungwa sindano akataka nimpe 70,000/=,kwenda ofisini terminal 3 nikakipata kwa 30,000/= pia bila kudungwa sindano.
 
Tuhuma nyingi ulizozitoa sio za kweli,inawezekana huna taarifa sahihi ,biashara ya aviation ina standard zake sisi wabongo bado tumelala ndio maana ni nadra kuona mzungu ameachwa na ndege.
Kwa hiyo TV na Speaker za matangazo zinafanya kazi?
 
Kuna siku mwaka jana mwishoni jamaa yangu kabisa anafanya hapo terminal 2 nilimwomba msaada wa kupata cheti cha yellow fever bila kudungwa sindano akataka nimpe 70,000/=,kwenda ofisini terminal 3 nikakipata kwa 30,000/= pia bila kudungwa sindano.
Huna tofauti na hao wala rushwa unatakiwa kuwa jela wewe
 
Yule manager alikuwa rafiki wa jiwe ndie aliyempa nafasi nae akampa jiwe hela za kampeni so hakuna wa kumng'oa akitembelea mindset za jiwe.
 
Yaani haitakiwi hata nukta ubao wa matangazo ya ndege uzime au uondolewe, ubao ndio dira ya abiria kujua time.
 
Nasema hivi, Sijiuzulu Ng'o.

Hivi wewe katika vitengo vyote vya mamlaka za Serikali umeona hichi changu tu? Binti mbona una nongwa sana wewe?

Niambie ni mamlaka gani iliyoko chini ya Serikali hii ambayo wewe unaona kila kitu kiko perfect mpaka uje uiseme hii ya kwangu? Yaan ushaenda Bandari, TRA, TBS, Ewura, Latra, Sumatra, Tanesco, Dawasco au ATCL, Mifuko ya Jamii, etc ukaona utendaji wao mpaka uje useme eti nijiuzulu?

Na nikijiuzulu nikakosa mshahara nitakula Nini? Utanisaidia kulisha na kusomesha Watoto wangu? Nijiuzulu ili nikose posho na marupurupu ya vikao na Safari mbalimbali ambazo zingine najitungia mimi Mwenyewe?

We unavyoniambia nijiuzulu utanipa wewe VX ya kutembelea? Unaona wivu sana navyoweka kishoka nikiwa naendeshwa kurudisha au kuchukuliwa nyumbani ee? Au utanipa wewe Allowance ya Nyumba ingawa naishi kwangu?

Wewe nani umemuona wa Level ya Mkurugenzi amejiuzulu kwa tumakosa tudogo tudogo kama hutu mpaka uje uniambie Mimi pia nifanye hivyo? Na nikijiuzulu nani ataniita Boss? Au unadhani sipendi sifa za kuitwa Boss? Unadhan sipendi kunyenyekewa?

Unajua hata nimehangaika vipi kupata hichi cheo mpaka uje useme kirahisi tu kua eti nijiuzulu? Usitake nitoe siri zingine za ndani mpaka leo unaniona niko hapa, lakin nakuapia kwa sababu ulizozitoa mimi kujiuzulu hiyo sahau.

Mambo ya hizi taasisi zetu hayaendi kiholela kama unavyodhani. Lazima ufanyike upembuzi yakinifu, iitishwe tenda, apatikane mzabuni, afanyiwe vetting kupitia vikao mbalimbali ambavyo vitahitaji gharama mbalimbali kama vile posho ya kikao, refreshments, ukumbi, etc, ipatikane bajeti ya huo ukarabati n.k. Hivi vyote vinahitaji muda na fedha ili tufanye kwa umakini zaidi.

Sio unakurupuka tu eti nijiuzulu.
Aaah mkurugenzi umeua,palilia basi kibarua hata tv tu za matangazo unang'oa kwani mafungu hayaji.Mbona una vitega uchumi vingi tu parking,mabango ya matangazo,kodi za frem za maduka,nk.
Pili huduma zote zile pale kuanzia choo,wifi, haki ya matangazo,nk si abiria analipa kupitia makato ya nauli yake,so uoni huo ni wizi.
Au tegemeo lako ni yule karumanzila. Timiza wajibu wako ukuwekwa hapo kuuza sura.
 
Back
Top Bottom