Brooklyn
JF-Expert Member
- Mar 17, 2009
- 1,459
- 284
Kwa masikitiko makubwa na kwa mara ya kwanza kwa zaidi ya miaka 16, watanzania wengi (hasa walalahoi) hawatopata nafasi ya kuangalia michuano ya fainali za Kombe la Dunia linalotarajiwa kuanza Ijumaa hii nchini Afrika Kusini.
Hii ni kutokana na uongozi wa TBC kuwatangazia watanzania kwamba TBC1, inayoonekana karibu nchi nzima kwa antena za kawaida itakuwa ikikatisha kurusha matangazo ya Kombe la Dunia ili kurusha matangazo ya moja kwa moja ya vikao vya Bunge linalotarajiwa kuanza siku chache zijazo mjini Dodoma.
Taarifa hiyo imezidi kueleza kwamba ni kwa wale tu watakaokuwa na ving'amuzi vya StarMedia vinavyouzwa katika mikoa mitatu tu yaani Dar, Dodoma na Mwanza ndio watabahatika kuangalia michuano hiyo kupitia channel mpya inayoanzishwa na TBC ya TBC2 itakayopatikana kupitia king'amuzi hicho tu.
Hili ni pigo kubwa kwa watanzania wengi ambao hawana uwezo wa kununua ving'amuzi hivyo vinavyouzwa kwa bei ya kati ya Tsh. 75,000 hadi Tsh. 90,000 na malipo ya kila mwezi ya Tsh. 9,000.
Ingawa uongozi wa TBC umepewa haki ya kurusha matangazo ya Kombe la Dunia bure na FIFA, swali je kwa nini wao wawauzie huduma hii watanzania ambavyo ni kinyume na matakwa ya FIFA inayowataka kurusha matangazo hayo free of charge????
Je kwa nini warushe matangazo ya mpira katika channel ambayo haina coverage kubwa nchini (TBC2) badala ya TBC1 yenye coverage kubwa?
Kwa nini waligombea kurusha matangazo ya Kombe la Dunia wakati walijua michuano hiyo ingeingiliana na vikao vya bunge? Si wangeacha michuano hiyo irushwe na ITV, Star TV au hata Channel 10?
Naamini huu unaweza ukawa ni mradi mwingine wa kifisadi unaotaka kuwalazimisha watanzania wanunua ving'amuzi vya StarMedia kwa nguvu!!
Binafsi naona ni bora TBC wangerusha michuano ya Kombe la Dunia kwenye TBC1 mechi zote bila kukatizwa katizwa na vikao vya Bunge, kwani vikao hivyo si vinaonyeshwa na STar TV.
Above all, binafsi naona vikao vya Bunge havina kitu kipya, ni bora watanzania tuangalie michuano ya Kombe la Dunia kuliko "kupoteza muda" kuangalia vikao vya Bunge.
Hapa ndipo naona yale malalamiko yanayotolewa na media zingine kwamba uongozi wa TBC unatumia vibaya kodi za wananchi na hivyo kuleta unfair competition kwa private media ni kweli kabisa.
Katika hili Tido Mhando umechemka BIG TIME!!
Hii ni kutokana na uongozi wa TBC kuwatangazia watanzania kwamba TBC1, inayoonekana karibu nchi nzima kwa antena za kawaida itakuwa ikikatisha kurusha matangazo ya Kombe la Dunia ili kurusha matangazo ya moja kwa moja ya vikao vya Bunge linalotarajiwa kuanza siku chache zijazo mjini Dodoma.
Taarifa hiyo imezidi kueleza kwamba ni kwa wale tu watakaokuwa na ving'amuzi vya StarMedia vinavyouzwa katika mikoa mitatu tu yaani Dar, Dodoma na Mwanza ndio watabahatika kuangalia michuano hiyo kupitia channel mpya inayoanzishwa na TBC ya TBC2 itakayopatikana kupitia king'amuzi hicho tu.
Hili ni pigo kubwa kwa watanzania wengi ambao hawana uwezo wa kununua ving'amuzi hivyo vinavyouzwa kwa bei ya kati ya Tsh. 75,000 hadi Tsh. 90,000 na malipo ya kila mwezi ya Tsh. 9,000.
Ingawa uongozi wa TBC umepewa haki ya kurusha matangazo ya Kombe la Dunia bure na FIFA, swali je kwa nini wao wawauzie huduma hii watanzania ambavyo ni kinyume na matakwa ya FIFA inayowataka kurusha matangazo hayo free of charge????
Je kwa nini warushe matangazo ya mpira katika channel ambayo haina coverage kubwa nchini (TBC2) badala ya TBC1 yenye coverage kubwa?
Kwa nini waligombea kurusha matangazo ya Kombe la Dunia wakati walijua michuano hiyo ingeingiliana na vikao vya bunge? Si wangeacha michuano hiyo irushwe na ITV, Star TV au hata Channel 10?
Naamini huu unaweza ukawa ni mradi mwingine wa kifisadi unaotaka kuwalazimisha watanzania wanunua ving'amuzi vya StarMedia kwa nguvu!!
Binafsi naona ni bora TBC wangerusha michuano ya Kombe la Dunia kwenye TBC1 mechi zote bila kukatizwa katizwa na vikao vya Bunge, kwani vikao hivyo si vinaonyeshwa na STar TV.
Above all, binafsi naona vikao vya Bunge havina kitu kipya, ni bora watanzania tuangalie michuano ya Kombe la Dunia kuliko "kupoteza muda" kuangalia vikao vya Bunge.
Hapa ndipo naona yale malalamiko yanayotolewa na media zingine kwamba uongozi wa TBC unatumia vibaya kodi za wananchi na hivyo kuleta unfair competition kwa private media ni kweli kabisa.
Katika hili Tido Mhando umechemka BIG TIME!!