Waliomdhalilisha Tido Muhando na kumtoa TBC na kumbambikia kesi za jinai leo wanajitokeza bila aibu kumpongeza kwa mafanikio makubwa ya Azam

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
877
4,101
Tido mzee wa watu katika utumishi wake alijenga CV nzuri ndani na kimataifa. Walipoona anafanikiwa na anazidi kupata jina Duniani wakamwita na kumkabidhi TBC. Akaweka mikakati kiwe chombo cha umma kinachozingatia maadili. Akakataa miradi ya rushwa mara TBC ikaanza kupata watazamaji wakiwemo wa mpira. TBC ikaanza kuingia kwenye ushindani wa tenda za matangazo na ikawa na uwezo wakupewa tenda husika.

Baada tu yakuonekana kodi za wananchi zinatumika vizuri na matunda yanaonekana. Mawaziri na wanasiasa wengine wakaanza kumwonea wivu as if na wao wanaweza kufanya kama yeye. Wakamchongea kwa Magu kisha wakamtwisha makesi ya jinai. Wakamfukuza ukurugenzi huku wakitoka adharani nakumtusi kuwa ni fisadi na mwizi.

Vyombo vya habari vikahusika kumkaanga ikiwemo TBC aliyokuwa anaongoza. Wakamleta Ayubu nadhani mnaona tofauti ya TIDO na Ayubu. Kwamba tunamtaka Dr. na siyo mkurugenzi. TBC imepotea kwenye ramani , imebaki na nyimbo za asili na vipindi vya marudio. As long watumishi wanalipwa mishahara chakufia nini bora liende.

Wanaomfahamu TIDO na wacha Mungu wa kweli wakamchukua nakumkabidhi ofisi. Leo AZAM ni chombo kikubwa Afrika linapambana na DSTV kwenye baadhi ya maudhui. Mzee Bakharesa tofauti na pesa pia amepewa Moyo wakumtukuza Mungu kila anapopata nafasi. Kila jambo analofanya linafanikiwa kwa sababu anayo hofu Mungu ndani yake.

Hao wanasiasa walioshangilia kutumbuliwa kwa TIDO jana nimewaona wamejazana tena Azam wakimpongeza. Tofauti ya TIDO na wao ni kwamba wao wanaishi kwa dhuluma na Majungu na kuwaachisha wenzao kazi ila TIDO anaishi kwa taaluma na kipawa cha Mwenyenzi Mungu.

Tido siyo bosi basi amebeba vision na kila aliyepo chini yake atamshape aweze kuifikisha vision panapotakiwa. Natambua kazi hii anamkabidhi Salimu Kikeke ila bado viatu vitakuwa vikubwa sana.

Cha kujifunza: KUITWA WAZIRI AU KIONGOZI WA KISIASA HAINA MAANA WEWE UMEBEBA BARAKA ZA UNAOWAONGOZA. NI SUALA LA MUDA TU, ISHI VIZURI NA WATU, TAMBUA WENZAKO PIA WANAFAMILIA NA ELEWA NI PUMZI YA MUNGU NDIYO IMETUFANYA TUWE HAI. USIUMIZE WENZAKO ILI WEWE UNUFAIKE.
 
Tido aliondolewa kwasabb za kisiasa.

Kuna kipindi cha TV kilianzishwa cha "mchakato majimboni". Kabla ya kuanza kurushwa hewani, Tido alivishirikisha vyama vyote (kikiwemo ccm) na kusaini nao mikataba. Kisha akatafuta wadhamini kwa kutumia mikataba hiyo. Kipindi kilihusu wagombea ubunge ktk Jimbo husika kufanya mdahalo utakaorushwa na TBC mubashara.

Walianzia Jimbo la Ubungo ambapo mgombea ubunge wa ccm alikuwa Hawa Nhumbi na wa chadema alikuwa Mnyika, na WA vyama vingine siwakumbuki.

Hawa Nhumbi alitoa machozi mbele ya kamera kwa namna alivyobanwa na Mnyika.

Ccm kuona hivyo, walianza kupiga sim muda huo huo wa kipindi wakitaka kipindi hicho kufutwa. Tido akagoma. Ndipo wakamchakachua kwa kumpatia barua saa Saba usiku.

Tido ni mahiri sana lkn alitaka kufanya kazi na watu wasiopenda umahiri (ccm).
 
Tido aliondolewa kwasabb za kisiasa.

Kuna kipindi cha TV kilianzishwa cha "mchakato majimboni". Kabla ya kuanza kurushwa hewani, Tido alivishirikisha vyama vyote (kikiwemo ccm) na kisaini nao mikataba. Kisha akatafuta wadhamini kwa kutumia mikataba hiyo. Kipindi kilihusu wagombea ubunge ktk Jimbo husika kufanya mdahalo utakaorushwa na TBC mubashara.

Walianzia Jimbo la Ubungo ambapo mgombea ubunge wa ccm alikuwa Hawa Nhumbi na wa chadema alikuwa Mnyika, na WA vyama vingine siwakumbuki.

Hawa Nhumbi alitoa machozi mbele ya kamera kwa namna alivyobanwa na Mnyika.

Ccm kuona hivyo, walianza kupiga sim muda huo huo wa kipindi wakitaka kipindi hicho kufutwa. Tido akagoma. Ndipo wakamchakachua kwa kumpatia barua saa Saba usiku.

Tido ni mahiri sana lkn alitaka kufanya kazi na watu wasiopenda umahiri (ccm).
Angeipeleka TBC mbali sana
 
Tido aliondolewa kwasabb za kisiasa.

Kuna kipindi cha TV kilianzishwa cha "mchakato majimboni". Kabla ya kuanza kurushwa hewani, Tido alivishirikisha vyama vyote (kikiwemo ccm) na kusaini nao mikataba. Kisha akatafuta wadhamini kwa kutumia mikataba hiyo. Kipindi kilihusu wagombea ubunge ktk Jimbo husika kufanya mdahalo utakaorushwa na TBC mubashara.

Walianzia Jimbo la Ubungo ambapo mgombea ubunge wa ccm alikuwa Hawa Nhumbi na wa chadema alikuwa Mnyika, na WA vyama vingine siwakumbuki.

Hawa Nhumbi alitoa machozi mbele ya kamera kwa namna alivyobanwa na Mnyika.

Ccm kuona hivyo, walianza kupiga sim muda huo huo wa kipindi wakitaka kipindi hicho kufutwa. Tido akagoma. Ndipo wakamchakachua kwa kumpatia barua saa Saba usiku.

Tido ni mahiri sana lkn alitaka kufanya kazi na watu wasiopenda umahiri (ccm).
Tido ni Mahiri kutokana na uzoefu wake wa kuwahi kufanya kazi ktk Democratic World ambako kuna mfumo wa Uliberari. Isingewezekana hata kidogo umahiri huo aendelee kuwa nao huku Tz kutokana na Mfumo wa Utawala uliopo hapa wa Ujamaa/Ukomunisti ambapo wanasiasa watawala wanapenda kujikweza na kujifanya miungu-watu. Alifamya makosa kukubali Ofa ya kuja kufanyakazi ktk Serikali kama hii ya kwetu ambayo haitaki ukweli na uwazi kwenye mambo yake.
Lakini hii kesi yake ni funzo kwa watu wengine waliopo huko nje hususani ktk nchi zilizoendelea ambao Wana matarajio ya kuja kufanya kazi kwenye hizi Serikali zetu za ki-Afrika, wanapopewa ofa ya ajira wanatakiwa wajitafakari mara mbilimbili kabla ya kukubali au kuikataa ofa husika.
 
Tido mzee wa watu katika utumishi wake alijenga CV nzuri ndani na kimataifa. Walipoona anafanikiwa na anazidi kupata jina Duniani wakamwita na kumkabidhi TBC. Akaweka mikakati kiwe chombo cha umma kinachozingatia maadili. Akakataa miradi ya rushwa mara TBC ikaanza kupata watazamaji wakiwemo wa mpira. TBC ikaanza kuingia kwenye ushindani wa tenda za matangazo na ikawa na uwezo wakupewa tenda husika.

Baada tu yakuonekana kodi za wananchi zinatumika vizuri na matunda yanaonekana. Mawaziri na wanasiasa wengine wakaanza kumwonea wivu as if na wao wanaweza kufanya kama yeye. Wakamchongea kwa Magu kisha wakamtwisha makesi ya jinai. Wakamfukuza ukurugenzi huku wakitoka adharani nakumtusi kuwa ni fisadi na mwizi.

Vyombo vya habari vikahusika kumkaanga ikiwemo TBC aliyokuwa anaongoza. Wakamleta Ayubu nadhani mnaona tofauti ya TIDO na Ayubu. Kwamba tunamtaka Dr. na siyo mkurugenzi. TBC imepotea kwenye ramani , imebaki na nyimbo za asili na vipindi vya marudio. As long watumishi wanalipwa mishahara chakufia nini bora liende.

Wanaomfahamu TIDO na wacha Mungu wa kweli wakamchukua nakumkabidhi ofisi. Leo AZAM ni chombo kikubwa Afrika linapambana na DSTV kwenye baadhi ya maudhui. Mzee Bakharesa tofauti na pesa pia amepewa Moyo wakumtukuza Mungu kila anapopata nafasi. Kila jambo analofanya linafanikiwa kwa sababu anayo hofu Mungu ndani yake.

Hao wanasiasa walioshangilia kutumbuliwa kwa TIDO jana nimewaona wamejazana tena Azam wakimpongeza. Tofauti ya TIDO na wao ni kwamba wao wanaishi kwa dhuluma na Majungu na kuwaachisha wenzao kazi ila TIDO anaishi kwa taaluma na kipawa cha Mwenyenzi Mungu.

Tido siyo bosi basi amebeba vision na kila aliyepo chini yake atamshape aweze kuifikisha vision panapotakiwa. Natambua kazi hii anamkabidhi Salimu Kikeke ila bado viatu vitakuwa vikubwa sana.

Cha kujifunza: KUITWA WAZIRI AU KIONGOZI WA KISIASA HAINA MAANA WEWE UMEBEBA BARAKA ZA UNAOWAONGOZA. NI SUALA LA MUDA TU, ISHI VIZURI NA WATU, TAMBUA WENZAKO PIA WANAFAMILIA NA ELEWA NI PUMZI YA MUNGU NDIYO IMETUFANYA TUWE HAI. USIUMIZE WENZAKO ILI WEWE UNUFAIKE.
Inasikitisha sana nchi zetu hizi, watu wenye vipawa wanadhulumiwa na kusumbuliwa, huku mapoyoyo mengi yakitamalaki. Kisha maisha Yao hao wala hayamvutii mtu, wakishaondoka kwenye nafasi zao hata harufu Yao haibaki zaidi ya kuja kudhalilika mtaani.

Hongera sana Bro Tido, wewe ni media yenyewe. Umekwepa mishale mingi tangu Ujana wako. Mungu akumbuke sadaka zako, AMINI
 
Hii habari ya Tido inafanana na ya mwandishi mmoja aliyekuwa wa waziri mkuu Malecela....baadae akaja kuwa boss wa Tanzania magazeti
Sijui nini kilimpata bahati mbaya jina limenitoka...ila ni mpare.
 
Salim kikeke hawezi pewa UCEO wa kampuni kubwa kama Azam Media kirahisi hivyo, kuna kahemele mle ndani labda
Salim ni msomaji mzuri wa habari lkn sio mwanahabari mzuri. Mnakumbuka alivyo mu interview rais akiwa BBC.?
 
Tido aliondolewa TBC nadhani kabla mwendazake hajaonja matamu ya ikulu. Kaondolewa kipindi Makamba Ni karibu mkuu, kipindi Cha figisu, kipindi kilichomfanya Sita ashindwe kugombea usabuufa kisa sio mwanamke, kipindi MTU mwenye degree nne alipochungulia kaburi.
 
Tido aliondolewa kwasabb za kisiasa.

Kuna kipindi cha TV kilianzishwa cha "mchakato majimboni". Kabla ya kuanza kurushwa hewani, Tido alivishirikisha vyama vyote (kikiwemo ccm) na kusaini nao mikataba. Kisha akatafuta wadhamini kwa kutumia mikataba hiyo. Kipindi kilihusu wagombea ubunge ktk Jimbo husika kufanya mdahalo utakaorushwa na TBC mubashara.

Walianzia Jimbo la Ubungo ambapo mgombea ubunge wa ccm alikuwa Hawa Nhumbi na wa chadema alikuwa Mnyika, na WA vyama vingine siwakumbuki.

Hawa Nhumbi alitoa machozi mbele ya kamera kwa namna alivyobanwa na Mnyika.

Ccm kuona hivyo, walianza kupiga sim muda huo huo wa kipindi wakitaka kipindi hicho kufutwa. Tido akagoma. Ndipo wakamchakachua kwa kumpatia barua saa Saba usiku.

Tido ni mahiri sana lkn alitaka kufanya kazi na watu wasiopenda umahiri (ccm).
Katibu mkuu wa CCM alikuwa Makamba.
 
Back
Top Bottom