Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,653
- 218,142
Wakuu asalaam aleykhum , baada ya salamu naingia moja kwa moja kwenye hoja , Mahakama imeifuta bodi feki iliyoundwa na Msaliti Lipumba , sasa yatokanayo na hili ni kwamba RITA walisajili bodi feki ya wadhamini , kwa makusudi au kwa maelekezo kutoka juu huku wakijua kwamba hawana kinga yoyote ile .
Imekuwa ni desturi sasa hukumu kama hizi zinapotoka huwa tunaishia hapa na kumwachia Mungu tu , bali kwa hili la RITA twende mbele kidogo ili liwe fundisho kwa wengine . Chama cha Cuf kiliionya mapema sana RITA kuachana na njama za kusajili bodi feki ya Lipumba , Maalim Seif aliita vyombo vya habari kumuonya mkurugenzi wa RITA kuachana na mpango huo ambao ulilenga kuvunja katiba ya nchi ( Jf inayo Taarifa hii bila shaka ) , lakini Mkurugenzi huyo aliendelea na mpango wake huo kwa maelekezo ya maharamia , sasa wakati wa yeye kuanza kulimia meno umefika rasmi , Hakuna cha mswalie mtume
Zipo tetesi kwamba Mkurugenzi aliyehusika anapanga kukimbia nchi baada ya kubaini kwamba hana kinga yoyote kutokana na uharamia alioutenda , sasa ni wakati wa wahusika kuhakikisha anadakwa mapema kabla hajatoroka.
Naomba kuwasilisha
Imekuwa ni desturi sasa hukumu kama hizi zinapotoka huwa tunaishia hapa na kumwachia Mungu tu , bali kwa hili la RITA twende mbele kidogo ili liwe fundisho kwa wengine . Chama cha Cuf kiliionya mapema sana RITA kuachana na njama za kusajili bodi feki ya Lipumba , Maalim Seif aliita vyombo vya habari kumuonya mkurugenzi wa RITA kuachana na mpango huo ambao ulilenga kuvunja katiba ya nchi ( Jf inayo Taarifa hii bila shaka ) , lakini Mkurugenzi huyo aliendelea na mpango wake huo kwa maelekezo ya maharamia , sasa wakati wa yeye kuanza kulimia meno umefika rasmi , Hakuna cha mswalie mtume
Zipo tetesi kwamba Mkurugenzi aliyehusika anapanga kukimbia nchi baada ya kubaini kwamba hana kinga yoyote kutokana na uharamia alioutenda , sasa ni wakati wa wahusika kuhakikisha anadakwa mapema kabla hajatoroka.
Naomba kuwasilisha