Mkurugenzi Makete/Njombe kitanzini kwa kuwaibia wananchi wanyonge fedha zaidi ya tshs.Milioni 500

kilagalila

JF-Expert Member
Nov 8, 2018
320
154
Na.amiri kilagalila
mc.amiri/mr.mtaani

Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa Mkoani Njombe inawashikiria Watumishi wa Tano Wa Halimashauri ya Makete akiwemo Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bw Francis Namaumbo kwa Ubadhirifu mkubwa wa Fedha zaidi ya Milioni 500 Za Kitanzania.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Kamanda wa Takukuru Mkoani Njombe Chalse Nakembetwa amesema kuwa Upotevu wa Fedha hizo umetoka katika Makusanyo ya Mwezi July hadi Semptemba ambapo Makusanyo yake yalikuwa ni Zaidi ya Bilioni moja huku Taarifa zikionyesha kuwa zaidi ya Millioni 500 zimepotea na Wahusika wakishindwa kutoa Maelezo yakutosha baada ya Kuhojiwa na Taasisi hiyo.

Katika uchunguzi wake Takukuru imebaini wizi na ufisadi unaofanywa na baadhi ya watendaji wa halmashauri ya wilaya ya Makete jumla ya Tshs 569,537,02/(milioni mia tano sitini na tisa laki tano na thelathini na saba elfu na sabini na mbili) sawa na asilimia 46% zilizokusanywa kwa utaratibu wa POS kwa kipindi cha julai hadi septemba 2018 hazijulikani zilipo.

Makusanyo haya yalikuwa ni sehemu ya Tshs 1,245,632,633(bilioni moja milioni mia mbili arobaini na tano laki sita thelasini na mbili elfu na mia sita thelasini na tatu) yaliyokusanywa katika kipindi tajwa, alisema kamanda.

Aidha taarifa za kibenk na za kimfumo wa kompyuta zinaonyesha kuwa fedha zilizoingizwa benk katika kipindi hicho kina bakaa kubwa na hakuna maelezo yoyote kutoka kwa wahusika kuonyesha fedha hizi zilipelekwa na kwa madhumuni gani.

Kutokana na uchunguzi huo Takukuru mkoa wa Njombe inawashikiria baadhi viongozi na watendaji wa halmashauri ya wilaya ya Makete kwa ajili ya uchunguzi. Baadhi ya viongozi hao ni pamoja na.

1:bwana Francis Namaumbo
Mkurugenzi wa wilaya ya makete

2:bwana Edward Mdagachule
Mweka hazina wa wilaya ya Makete

3:bwana Edonia mahenge
Afisa biashara wilaya ya Makete

4:Goden Mbilinyi
Mtaalam wa Tehama Makete

5:Isaya madock
Mhasibu wa mapato Makete

Huku watuhumiwa wengine wakiendelea kutafutwa.

Katika hatua nyingine kamanda wa Takukuru mkoa wa Njombe Cherls Nakembetwa amesema kuwa watuhumiwa wote hapo juu wanashikiliwa kwa uchunguzi kwa makosa yafuatayo.

1.Matumizi ya nyaraka kumdanganya mwajiri K/F 22 cha PCCA/2007
2.Ubadhilifu na ufujaji K/F 28 cha PCCA/2007
3.Wizi chini ya kifungu cha 273 cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai (penal code)
4.Kujipatia manufaa K/F 23 cha PCCA/2007

Pamoja na makosa mengine yatakayobainishwa na uchunguzi.

Aidha takukuru kama chombo cha uchunguzi na mashtaka kinategemea kuchukua hatua kali kwa watakaobainika kuhujumu mapato ya serikali mara uchunguzi utakapokamilika ikiwa ni pamoja na kufungua kesi mahakamani.

MWISHO
IMG_20181114_162930.jpg
IMG_20181114_162941.jpg
IMG_20181114_162952.jpg
IMG_20181114_163001.jpg
IMG_20181114_163024.jpg
IMG_20181114_163034.jpg
IMG_20181114_163046.jpg
IMG_20181114_163200.jpg
 
Je nakimbetwa nyie takukuru mmemshughulikia na yeye kwani alikuwa na mgao mkubwa tangu tuhuma za tenda ya ushuru,fedha za miradi ya unicef,mishahar hewa ya wafu,wastafu,etc ya hosptali ya bulongwa,wizi wa ngombe uliofanywa na maafisa mali asili wa pori la mpanga kipengele,ajali hew ya gari la veta wakati wa unenzi wa chuo cha veta,etc
 
Ningependa kuona mwisho wa hizi tuhuma zisiishie kuchafuana!
MAKETE imekuwa shamba la bibi. Namaumbo uliniachisha kazi kwa uonevu uliotukuka. Leo kwako.malipo ni hapa hapa duniani mkuu.
mdagachule sijui Kama utachomoka mwakajana wakati wa Zara ya waziri mkuu ulisimamishwa then ukasafishwa. Leo tena!!baba! Jipange sawasawa.
Huyo Afisa biashara wilaya namjua alikuwa Mwalimu lupalilo sekondari, huko sijui kaingiaje!!!! Tangu awe hapo anapanua miradi usipime. Labda ningejua take home ya Afisa biashara wilaya. Nisingesema sana.!!!!
 
Je nakimbetwa nyie takukuru mmemshughulikia na yeye kwani alikuwa na mgao mkubwa tangu tuhuma za tenda ya ushuru,fedha za miradi ya unicef,mishahar hewa ya wafu,wastafu,etc ya hosptali ya bulongwa,wizi wa ngombe uliofanywa na maafisa mali asili wa pori la mpanga kipengele,ajali hew ya gari la veta wakati wa unenzi wa chuo cha veta,etc
Lazima ahusike mkuu. Ivi pale elimu pako salama?
 
MAKETE imekuwa shamba la bibi. Namaumbo uliniachisha kazi kwa uonevu uliotukuka. Leo kwako.malipo ni hapa hapa duniani mkuu.
mdagachule sijui Kama utachomoka mwakajana wakati wa Zara ya waziri mkuu ulisimamishwa then ukasafishwa. Leo tena!!baba! Jipange sawasawa.
Huyo Afisa biashara wilaya namjua alikuwa Mwalimu lupalilo sekondari, huko sijui kaingiaje!!!! Tangu awe hapo anapanua miradi usipime. Labda ningejua take home ya Afisa biashara wilaya. Nisingesema sana.!!!!

Uliachishwa kazi gani? Alikuachisha kazi kwa haki au uonevu?
 
Huko ndio nyumbani....hiyo wilaya wakati mwingine ni kama huwa inasahaulika tu na serikali.

Hongereni TAKUKURU maana huko wakati mwingine huwa wanaona wako nchi yao peke yao.
 
Ni hatua nzuri ya kuwafikisha Mahakamani ili haki itendeke na pia ni jitihada nzuri katika mapambano dhidi ya ufisadi ambao umetamalaki katika Ofisi za Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa mfano mmojawapo ni hii Halmashauri ya Makete.
 
MAKETE imekuwa shamba la bibi. Namaumbo uliniachisha kazi kwa uonevu uliotukuka. Leo kwako.malipo ni hapa hapa duniani mkuu.
mdagachule sijui Kama utachomoka mwakajana wakati wa Zara ya waziri mkuu ulisimamishwa then ukasafishwa. Leo tena!!baba! Jipange sawasawa.
Huyo Afisa biashara wilaya namjua alikuwa Mwalimu lupalilo sekondari, huko sijui kaingiaje!!!! Tangu awe hapo anapanua miradi usipime. Labda ningejua take home ya Afisa biashara wilaya. Nisingesema sana.!!!!
Nikifikiria umaskini wa ndugu zangu katika karafa ya Magoma wilaya Makete halafu wafanyakazi wanakomba fedha. Pambafu zao....
 
Nikifikiria umaskini wa ndugu zangu katika karafa ya Magoma wilaya Makete halafu wafanyakazi wanakomba fedha. Pambafu zao....
Hizi point of sales(pos) zitafunga watu ambao awazijui mpaka wachanganyikiwe unaweza kukusanya milioni kumi let say kwenye mnada ukienda kuchukua bill yako ili ulipe bill inasoma milioni nane labda na nusu,kidume unajiona umeibia serikali kumbe mtandao ulisumbua kwenye kupushi data nyingine zinabaki kwenye pos wewe hyo milioni na nusu unafuna mwezi unaofata unakuja kutoa bill unakuta kiasi ulichonacho ni kidogo ukiliganisha na bill yani imezidi kwa milioni na nusu nawewe pesa ushaitafuna aisee mbona utajibeba.
 
Ni hatua nzuri ya kuwafikisha Mahakamani ili haki itendeke na pia ni jitihada nzuri katika mapambano dhidi ya ufisadi ambao umetamalaki katika Ofisi za Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa mfano mmojawapo ni hii Halmashauri ya Makete.
Halimashauri zetu ni chaka mkuu,ningetamani siku moja tungeachana na mfumo wa halimashauri,madudu yamekuwa mengi mno..
 
Back
Top Bottom