nez-o
Senior Member
- Apr 13, 2019
- 181
- 178
Wadau, leo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Masasi aliamua kumvua cheo Mwalimu Mkuu shule ya Msingi Chiwata tena mbele ya halaiki ya watu kisa kakosa hela ya kutoa harambee ya kuchangia maendeleo ya Kata.
Mkutano huo ulikuwa umeandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Ndanda, Cecil Mwambe. Mkurugenzi akaanza kulazimisha watendaji, Mratibu elimu Kata na walimu walioko kwenye mkutano watoe ahadi wanachangia kiasi gani.
Ilipofika zamu ya mwalimu huyo akadai hana hela, ndipo DED mbele ya watu akasema “nakushusha cheo”.
Wananchi wakashangilia “oyoooo”! Ila baada ya Mbunge kumuombea msamaha akamrudishia cheo chake!
Je, wadau huu si udhalilishaji? DED Masasi DC acha ukoloni na umwinyi!
Mkutano huo ulikuwa umeandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Ndanda, Cecil Mwambe. Mkurugenzi akaanza kulazimisha watendaji, Mratibu elimu Kata na walimu walioko kwenye mkutano watoe ahadi wanachangia kiasi gani.
Ilipofika zamu ya mwalimu huyo akadai hana hela, ndipo DED mbele ya watu akasema “nakushusha cheo”.
Wananchi wakashangilia “oyoooo”! Ila baada ya Mbunge kumuombea msamaha akamrudishia cheo chake!
Je, wadau huu si udhalilishaji? DED Masasi DC acha ukoloni na umwinyi!