Mpita Njia
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 6,997
- 1,163
Asubuhi hii mjini Dodoma, Mkulo amekutana na waandishi wa habari na kutokana na yale aliyoyaeleza kuna uwezekano mdogo wa waliopanda Deci kulipwa fedha zai zote. Kwa mujibu wa maelezo ya Mkulo, hesabu zimekaa hivi:
Katika miezi mitatu ta mwisho kabla ya Deci kufungiwa, zaidi ya watu laki 3 walipanda zaidi ya Sh bilioni 39.
Sakasaka ya serikali iliambulia zaidi kidogo ya Sh bilioni 1 katika akaunti za Deci.
Sakasaka majumbani kwa viongozi ikaambulia Sh bilioni kama nane hizi zilizokuwa zimehifadhiwa majumbani (nyingibne kwenye maboksi).
Sakasaka kwenye akaunti za viongozi wa decci ikaambilia kiasi kingine na kufanya jumla ya fedha zalizshikiliwa na serikali kutoka DECI kuwa kama sh bilioni 14.
Hapo kuna pengo la zaidi ya Sh bilioni 25 iwapo itatakiwa kuwalipa wale waliopanda miezi mitatu ya mwisho ambao hawajavuna hata mara moja (kumbuka hapa hatujahusisha wapandaji wengine).
Katika miezi mitatu ta mwisho kabla ya Deci kufungiwa, zaidi ya watu laki 3 walipanda zaidi ya Sh bilioni 39.
Sakasaka ya serikali iliambulia zaidi kidogo ya Sh bilioni 1 katika akaunti za Deci.
Sakasaka majumbani kwa viongozi ikaambulia Sh bilioni kama nane hizi zilizokuwa zimehifadhiwa majumbani (nyingibne kwenye maboksi).
Sakasaka kwenye akaunti za viongozi wa decci ikaambilia kiasi kingine na kufanya jumla ya fedha zalizshikiliwa na serikali kutoka DECI kuwa kama sh bilioni 14.
Hapo kuna pengo la zaidi ya Sh bilioni 25 iwapo itatakiwa kuwalipa wale waliopanda miezi mitatu ya mwisho ambao hawajavuna hata mara moja (kumbuka hapa hatujahusisha wapandaji wengine).