mkuu Mshana jr hivi mwanga na mchawi wanaweza kukutana wote eneo la tukio kwa muda mmoja mf.mwanga kaja kwangu saa 8 usiku na muda huo huo aliofika akamkuta mchawi anafanya yake hapo huwa kinatokea nini.
Jana nilisoma huu Uzi usiku nikamuona mwanamke amenijia kwa nyuma miguuni anakuja fosi kwangu nikajitingisha mwili ili ajue Niko macho akarudi nyuma ,nikiacha ananifuata mwishi nikahisi nimenyanyuka na kumkea lakini sikumbuki nilaikuwa namwambia mini akapotea nikastuka.sijui ni ndoto au?
mshana jr, ukisha mfanyia hivyo siku ukitaka alone au tuseme Dawa yake ni nini? kuna swali LA Mdau mmoja ameuliza namna ya kukomesha Chuma ulete walitaka kunifilisi kabisa nikaleta mtu wa maombi...he kuna namna ya kumkomesha kama hii....
Mshanajr, nasikia wanauwezo Wa kujua alie mzuru sasa akinijua nimemfanyia hivyo si atanidhuru nami nitakuwa na kinga gani kwake?
Unajuaje kama huyu ndiye Hata uchote unyayo wake? Huu Uzi ni wa kichonganishi, ufutwe....
swali hili ndio muhimu lakini hataki ulijibu, uzi huu hauna maana kama hawezi kujibu hapa. Alipokanyaga mchawi unapaonaje?
swali hili ndio muhimu lakini hataki ulijibu, uzi huu hauna maana kama hawezi kujibu hapa. Alipokanyaga mchawi unapaonaje?
Post iko very clear sizungumzii mchawi nazungumzia wanga.... Always hawa watu kwakuwa mnakutana usiku kuna hisia fulani hukujia kuwa huyu ndiye kanijia usiku wa Jana.... Trust me hata ukimwangalia usoni utaona hana courage ya kukuangalia
Sasa kinachofuatia ni kuvizia hizo nyayo zake akiwa Peku.... Sio kazi rahisi kama kuagiza bia counter
Yeyote mwenye kadhia zitokanazo na hizi sayansi mazingara dawa yake ni Yesu tu huhitaji hata kidonge. Ni kazi ya dk sifuri hapo ndipo ninapomfuraiaga Yesu maana walimwengu wangetumeza tungali hai!!!Leo nafundisha live...!!! Kwa wale wasiopenda natanguliza kuomba radhi TUVUMILIANE kuna baadhi wanaohangaishwa yatawafaa
Wanga ni watu hovyo sana hukufanyia mambo ya kukuchosha mwili na vitu vya ajabu ajabu bila faida yoyote
Hivyo basi mtu wa kaliba naye hana budi kupata shida kidogo pale inapobidi
Tafuta ufanikiwe kupata mchanga wa nyayo zake akiwa peku,tafuta ndulele tatu jivu pilipili kichaa au ----- na kipande kidogo cha kaniki....changanya vyote ikibidi twanga ongeza na matone kadhaa ya damu yako kisha funga kaza sana kwenye kipande cha kaniki
1. Sigina na kisigino huku ukinuizia kama unataka miguu imuume
2. Choma na sindano ukitaka miguu ichome chome
3. Banika motoni ukitaka miguu yake iwake moto
4. Kaanga kwenye kikaango kikavu ukitaka miguu imuwashe
Fanya hivi kama unaamini hizi mambo na una roho mbaya ya visasi...kumbuka kuna hukumu siku ya kiama
Sihusiki na matokeo ya matendo yako
wewe jamaa mtata. uzi wako hauna uhalisia labda wanga wa ulaya au haya mambo umeyachukua kitabuni. Kumjua au kumuoa mwanga kunahitajika nguvu ya kishirikina na sio kirahisi hivyo unavyosema. Mi kwa umri wangu huu nakaribia miaka 50 sijawahi sikia mtu kumchota unyayo mwanga.