Mkuu Zanta lile azimio moja kwa moja linamwingiza mkombozi pia kwasababu wamesema na Stanbic na benki nyingine zote zilizopokea pesa ya escrow. Kilichosababisha waseme hivyo ni kwasababu pesa zilipotoka BOT zote zilienda kwanza Stanbic halafu zikaanza kuenda kwenye mabenki mengine. Zile za rugemalila zikaenda mkombozi lakini kuna zingine zimepelekwa kwenye mabenki kama bank of India na nyinginezo ambazo taarifa zake zinatakiwa kutafutwa zaidi.
Mkuu kibona hapa nimekupata vilivyo sababu ya mkombozi kuachwa thanks
Zanta, na wewe unakubaliana na majibu ya Kibona!
Swali lako lililoeta mada lilikuwa safi. Benki zilizotajwa tangu mwanzo mwa mzozo ni mbili tu yaani Mkombozi na Stanbic. Tena ukumbuke kwamba Mkombozi imekuwa controversial sana kwa sababu ni ya Kanisa na pili ndiyo yenye list ya majina ya akina Tibaijuka, Kilaini, Nzigilwa na wengine.
Hivyo, kuhusuana na majina ya benki, Mkobozi ilijaa modomoni mwa watu kuliko hata Stanbic.
Sababu ya pili ingawa si ya muhimu sana ni kwamba Stanbic hata ingefanya uharamia zaidi ya huu, inajulikana ni benki ya kibiashara zaidi kwani uhuni wa benki za namna hii si kitu cha ajabu. Uajabu ni kuhusishwa kwa benki ya Kanisa, tena Kanisa Katoliki.
Hivyo, ubora wa swali lako ni kwamba kwa nini Mkombozi Bank iongoze kutajwa wakati wa tuhuma, halafu mwishoni isitajwe iishie kufumbiwa kwamba "
na benki zingine".
Neno "
na benki zingine" lingetumika baada ya kutaja zote mbiliMkombozi na Stanbic, maana hizi zimejadiliwa sana, tena Mkombozi ni zaidi, kuliko zingine zinazokuja kuibuka siku ya mwisho ya mjadala, tena siku ya hukumu.
Natumaini imeeleweka.