GE2025 Mkoa wa Dar es Salaam: Matukio na Matokeo ya Uchaguzi Mkuu 2025 kama yanavyotujia

GE2025 Mkoa wa Dar es Salaam: Matukio na Matokeo ya Uchaguzi Mkuu 2025 kama yanavyotujia

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
4,783
Reaction score
14,975
Wakuu,

Mada hii itakuwa na 'Updates' za Uchaguzi Mkuu 2025 kama yanavyotujia kutoka kwenu kutoka mkoa wa Dar es Salaam. Ukiwa na taarifa yoyote ambayo ni ya eneo hili tafadhali usisite kuweka.

Mkoa wa Dar es Salaam una jumla ya majimbo ya uchaguzi (12) ambayo ni
  1. Jimbo la Kinondoni
  2. Jimbo la Kawe

  3. Jimbo la Ilala

  4. Jimbo la Segerea

  5. Jimbo la Ukonga

  6. Jimbo la Temeke

  7. Jimbo la Mbagala

  8. Jimbo la Kigamboni

  9. Jimbo la Ubungo

  10. Jimbo la Kibamba

  11. Kivule

  12. Chamazi

Updates (Walioshinda Ubunge Mkoa wa Dar Es Salaam)

CCM imeshinda majimbo 10 ya uchaguzi kati ya majimbo 12 yaliyopo isipokuwa jimbo la Ukonga ambalo ACT-Wazalendo wameshinda na Jimbo la Segerea ambalo CHAUMMA wameshindi kiti hicho.

Majimbo yote ni kama Ifuatavyo;

  • Abbas Gulam Tarimba (Jimbo la Kinondoni)-CCM
  • Geofrey Anyosisye (Jimbo la Kawe)-CCM
  • Mussa Azzan Zungu (Jimbo la Ilala)-CCM
  • Agnesta Kaiza (Jimbo la Segerea)-CHAUMMA
  • Bakari Shingo (Jimbo la Ukonga)- ACT-WAZALENDO
  • Mariam Kisangi (Jimbo la Temeke)-CCM
  • Kakulu Buchard Kakulu ( Jimbo la Mbagala)-CCM
  • Haran Nyakisa Sanga ( Jimbo la Kigamboni)-CCM
  • Prof. Alexander Kitila Mkumbo (Jimbo la Ubungo)-CCM
  • Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki (Jimbo la Kibamba)-CCM
  • Dougras Didas Masaburi ( Jimbo la Kivule)-CCM
  • Abdallah Jafari Chaurembo ( Jimbo la Chamazi)-CCM

Kupata matukio ya nyuma kabla ya siku ya Uchaguzi soma > PreGE2025 - Dar es Salaam: Matukio Yanayojiri Kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
 
Kijazi hapa jamaa wametega.

Kijazi.png
 
Mi ninacho ona huku mtaani kwetu hajatoka mtu hata mmoja kwenda kupiga kura, kituo cha kupigia kura jirani hapa kilicho shule ya msingi ni peupe sana kama hamna chochote .
 
Hali katika vituo mbalimbali vya kupigia kura ni tulivu huku watoa huduma katika vituo hivyo wakitoa maelekezo na kufuata procedures zote.

Watu wanaendelea kujitokeza
 
Hakuna watu bwana acheni uongo,mm nipo hapa nasimamia kituo hakuna watu tupo tu tunakula upepo
 
Vijana wa Wilaya ya Temeke wameendelea kujitokeza kwa wingi kutimiza haki yao ya kupiga kura na kuchagua viongozi wanaowataka Madiwani, Wabunge na Rais.

 
Habari picha inaonesha watanzania wakiendelea na zoezi la upigaji kura
thumb1.jpg
thumb.jpg
thumb2.jpg
 
Mi msimamizi nipo Mwanza hapa kituo chetu hadi sasa tangu tumefungua saa 1 asubuhi waliokuja kupiga kura hata 10 hawafiki nipo tu napunga upepo
 
Nyumbu wote wamekuwa wasimamizi wa vituo vya kupigia kura.Uchaguzi waliosema haupo.Nyumbu wamekuwa vigeugeu sana
 
Nimepata bahati ya kutembekea vituo vyote vya kupigia kura vilivyoko kwenye kata yangu nimejionea kwa macho yangu uchache wa watu wanaojitokeza kupiga kura
 
Back
Top Bottom