Mkoa wa Arusha hali ni mbaya

Mkoa wa Arusha hali ni mbaya

Hoja unayo ila umeiwasilisha kikudakuda sana,kwani sisi wa Tunduru hatuhitaji barabara nzuri,mbona Iringa wanatulisha,acha kujifanya wathamani kuliko sisi.
Duuh Kama watu bado mna mawazo kama haya basi nchi inasafari ndefu Sana , mawndeleo yatakuja mpaka watu wa aina yako wapotee kabisa
 
Hyo barabara ipo kat kat ya mji?? maana barabara zote zilizo kati kati ya mji zinawekewa lami miji yote Tanzania.....nimeenda Tabora nimekuta lami za hatar zinawekwa.....sasa sijajua huko labda ni pembezon mwa mji
 
Tatizo uelewa wako Upo chini, ninacho maanisha hapo ukiitengeneza mkoa wa Arusha vizuri, watalii wataongezeka kwa kupata huduma nzuri, then pato la Taifa litaongezeka ndio na ww utaweza kutengeneza nchi kwa ajili yako.. Kwa kifupi katika nchi yeyote kuna mikoa imekaa kibiashara kitaifa.
Una hoja, lakini uwasilishaji wako una kasoro. Unaweza kuwa unaelekeza lawama kwa mtu asiehusika. Hizi barabara zina madaraja na kila daraja lina mamlaka inayoshughulikia. usipojua madaraja hayo utakuwa unaropoka badala ya kujenga hoja kwa wahusika sahihi.

Kuna barabara ziko chini ya Serikali za Mitaa, Halmashauri za wilaya, miji, manispaa, na majiji. Hizi wakuulizwa ni Madiwani na Wabunge wa eneo husika ndio wanaozitengea fedha katika bajeti zao kulingana kipaumbele cha eneo husika.

Serikali kuu inashughulika na barabara zilizoko chini ya Tanroad na Tarura.

Sasa tuambie barabara yako inaangukia kwa mamlaka gani tuwalaumu.
 
pamoja nina uraia wa 50% wa kaskazini lakini ukweli huko kidogo kulikuwa kuzuri kwa barabara kuliko mikoa mingine na si kweli kuwa Arusha serikali imekutelekeza ni swala la muda tu. yapo yaliyosogea pia
 
Binadam ni kiumbe wa ajabu sana.
Mimi binafsi nimekuwa nikipita arusha mara nyingi tu na kila nikipita ninakuta mabadiliko makubwa ya infrastructure. Arusha ya sasa ni tofauti kabisa na Arusha ya mwaka juzi. Natambua kwamba kuna matatizo mengi hasa kwenye vitongoji, lakini hayo yote hayawezi tatuliwa overnght.
Ila ni kweli asiee nilikuwa arusha jana tu, kuna mabadiliko makubwa sana ya kimiondombinu, zaidi sana si vyema kuona kidogo kilichosahaurika/kilichobaki na kusahau kikubwa kilichofanyika.
 
Daaah Brother hata wewe tena?
I thought I could see a comment like this from praise team and 7000/= aspirants.. but not from you. To me ua among the members who gives us thoughtful and constructive ideas.. but this one mmmmmmmmm
He is one of the praise team nowadays,no suprise!
 
Kwa kweli hii hali ni mbaya kweli!, ukiambiwa hapa kuna mbunge unaweza usiamini, its so sad and pathetic. Hivi mbunge wa hapa ni nani tena vile?. Fedha za mfuko wa jimbo anafanyia nini?, maana zinatosha hata kumwaga tuu kifusi. Wana Arusha mlifanya makosa sana, sasa msirudie makosa ili Arusha irudie ile hadhi yake.

P
Kumbe serikali inapokosa mapato kutokana na mbunge basi mbunge ndie anaekuwa amekomolewa, ! Sikufaham , anyway kwa hiyo Lema akiendelea kuwa mbunge hiyo barabara Serikali hawataitengeneza,? Awamu hii ina siasa za kipumbavvu kweli
 
Kwa kweli hii hali ni mbaya kweli!, ukiambiwa hapa kuna mbunge unaweza usiamini, its so sad and pathetic. Hivi mbunge wa hapa ni nani tena vile?. Fedha za mfuko wa jimbo anafanyia nini?, maana zinatosha hata kumwaga tuu kifusi. Wana Arusha mlifanya makosa sana, sasa msirudie makosa ili Arusha irudie ile hadhi yake.

P
fedha ya mfuko wa jimbo 200 million,walaumiwe TARURA mamlaka huru kabisa
ARUSHA CC mwenyekiti ni mkuu wa mkoa ,mbunge ni mjumbe tu
 
Mleta uzi umeleta uchochezi ambao hakuna tija nani asiye fahamu awamu ya tano ilivyo jenga barabara Arusha,achilia mbali barabara ya Arusha himo Nairobi taveta ambayo hivi sasa ni ya motorway yaani magari hayapishani.
Barabara za ndani katikati ya jiji kuunganisha kila mtaa.Serikali imejito na kujizaatiti japo kuwa Arusha kwa muda mrefu imekosa wabunge wa kusema shida za wananchi badala yake wa!ekuwa wakifanya vurugu tu bungeni.
Hiyo barabara uliyo ipost ya mianzini ukienda mbele imejengwa kwa kiwango cha lami hadi ilboru,kimebakia kipande kidogo sana cha kuunganisha kwenda hadi mataa mianzini.Hii yote ni juhudi ya serikali pasipo mbunge kuhusika kwani yeye yupo busy na kampuni yake ya utalii ili alipe madeni aliyokopa kwenye saccos yake ya ufipa.Kama mtakumbuka raisi alipita kwenye hiyo barabara akasimama maeneo ya haika kumuulizia mbunge hayupo kwenye ziara,mbumge kutafutwa kwenye simu anasema hana taarifa ya ziara na hayupo karibu.Ni wakati muafaka wa kumchagua mwakilishi mzuri anaye weza kusukuma gurudumu la maendeleo sawa na kazi jpm achaneni na hao wana sacoss ya ufipa.
 
Achana na mimi mpumbavu wew
Kwanza sikukujibu wew. Kwa hiyo Mbeya yenyewe haina umuhimu ktk nchi hii na inatoa mchele ilhali barabara zake si za kuridhisha. Mtwara je inayotoa korosho, na Geita inayotoa dhahabu. Mbona karibu nchi nzima kuna changamoto ya barabara. Eti maendeleo yanatolewa Arusha kupelelwa kwingine..mnaumwa nnyaa. Angesema Arusha kuna barabara mbovu na serikali ishughulikie hilo bila kuongea upimbi wa ukanda angepungukiwa nin we pongoo?
Kiwango chako cha argument, kinaashiria uelewa wako ni mdogo sana,mikoa yote ina umuhimu ila inatofautiana kwa umuhimu katika biashara, ndio maana dar, kuna flyover na sio mtwara
 
Hyo barabara ipo kat kat ya mji?? maana barabara zote zilizo kati kati ya mji zinawekewa lami miji yote Tanzania.....nimeenda Tabora nimekuta lami za hatar zinawekwa.....sasa sijajua huko labda ni pembezon mwa mji
Ndiyo umejibu hoja hapo.!!hongera.
 
Kwani hamfahamu kwamba kuna Political battle kati ya Utawala wa Jiwe na mikoa ya Kaskazini hasa Kilimanjaro na Arusha
 
Hapo vipi,

Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo chini, mkoa wa Arusha umeendea kusahaulika na kutelekwezwa, awamu hii japo ndio mkoa unaochangia mapato makubwa katika Nchi hii.

Miundo mbinu ndani ya mjini, imegeuka kama mito, chini ya uongozi wa Mrisho Gambo huu mkoa umekuwa na hali mbaya kimaendeleo.

Kuna hii barabara ya kutoka white rose na pale mianzini zimekuwa kama mito ndani ya mjini..

Cha kujiuliza mkoa nyeti Kama mkoa wa Arusha, yenye fursa za kitalii ,makao mkuu ya Afrika Mashariki.. Inatelekezwa hivi kisa hila za kisiasa ,inakuwa haina maana Kwa sababu hauwakomoi watu wa Arusha peke yao ila ni Taifa nzima, kwasababu watalii wanapenda mkoa wenye miundo mbinu nzuri.

Sasa Kama utamzungusha Mzungu kwenye mashimo namna hii, unategemea akirudi kwao atarudi tena au ataenda kumuhamasisha wezio waje watembelee mkoa wa Arusha.

Ni aibu kwa uongozi huu, Embu muache tabia za kimaskini, tufike mahali tuangalie maslahi mapana ya Taifa hili.

Mkoa wa Arusha unatakiwa utuzwe sio kwa maslahi ya watu Wa Arusha ila ni Kwa maslahi ya Taifa.

Leo kinachoendelea hapa Arusha ni siasa za kimaskini za kupokonya mkoa huu fursa na kupeleka mikoa mingine kwa hila.

Leo mikutano ya kimataifa ilifanyika hapa miaka mitano iliyopita , hata Bunge la East Africa sidhani kama bdo waendelea kufanyika hapa.

Juzi wanunuzi na wauza mawe wanaambiwa wasionekane tena mjini, eti waande Namanga, kufanyia biashara ni aibu.

Hivi mtu ametoka na Billioni zake Thailand, unamuambia aende Namanga akalale kwa guest kwa usalama upi.

Kinachoamua centre ya biashara sio maamuzi ya kisiasa ni miundo mbinu za kibiasha ni kimaanisha usalama wa wao na huduma muhimu kwao. Sasa Kama tunafikia pahala pa kuwaamurisha watu kama Ngo'mbe pasipo kukaa na wadau wenyewe ukapokea maoni yao,tafsiri yake hiyo mipango yenu ya kisiasa lazima itakwama au mtaharibu biashara ya madini moja kwa moja.
View attachment 1106188View attachment 1106191View attachment 1106199View attachment 1106202View attachment 1106205View attachment 1106205View attachment 1106188View attachment 1106202


Yule mbunge wao kiherehere yuko wapi?
 
Daaah Brother hata wewe tena?
I thought I could see a comment like this from praise team and 7000/= aspirants.. but not from you. To me ua among the members who gives us thoughtful and constructive ideas.. but this one mmmmmmmmm
Isikushangaze sana kwa kuwa huyo jamaa keshafika bei........
 
Hyo barabara ipo kat kat ya mji?? maana barabara zote zilizo kati kati ya mji zinawekewa lami miji yote Tanzania.....nimeenda Tabora nimekuta lami za hatar zinawekwa.....sasa sijajua huko labda ni pembezon mwa mji
Ni kati kati ya mjini Sana, imagine ni hatua kumi mpaka kwenye taa za kuongozea magari.
 
Hivi mbunge wa hapa ni nani tena vile?. Fedha za mfuko wa jimbo anafanyia nini?, maana zinatosha hata kumwaga tuu kifusi. Wana Arusha mlifanya makosa sana, sasa msirudie makosa ili Arusha irudie ile hadhi yake.

P
We Mzee umeandika nini hiki?
 
Mkuu paskali baraza la madiwani pamoja na mbunge wao wamefanya mapinduzi makubwa kwenye miundo mbinu,awamu zote za chama cha kijani wao ilikua kula pesa na ukabila.
Sasa hivi kuna barabara za mjini na kwenda tume ya atomic 27km zinawekewa lami.
Huku dar nyie pambaneni na dengua tu
Kwa kweli hii hali ni mbaya kweli!, ukiambiwa hapa kuna mbunge unaweza usiamini, its so sad and pathetic. Hivi mbunge wa hapa ni nani tena vile?. Fedha za mfuko wa jimbo anafanyia nini?, maana zinatosha hata kumwaga tuu kifusi. Wana Arusha mlifanya makosa sana, sasa msirudie makosa ili Arusha irudie ile hadhi yake.

P
 
Mleta uzi umeleta uchochezi ambao hakuna tija nani asiye fahamu awamu ya tano ilivyo jenga barabara Arusha,achilia mbali barabara ya Arusha himo Nairobi taveta ambayo hivi sasa ni ya motorway yaani mahari hayapishani.
Barabara za ndani katikati ya jiji kuunganisha kila mtaa.Serikali imejito na kujozatiti japo kuwa Arusha kwa muda mrefu imekosa wabunge wa kusema shida za wananchi badala yake wa!ekuwa wakifanya vurugu tu bungeni.
Hiyo barabara uliyo ipost ya mianzini ukienda mbele imejengwa kwa kiwango cha lami hadi ilboru,kimebakia kipande kidogo sana cha kuunganisha kwenda hadi mataa mianzini.Hii yote ni juhudi ya serikali pasipo mbunge kuhusika kwani yeye yupo busy na kampuni yake ya utalii ili alipe madeni aliyokopa kwenye saccos yake ya ufipa.Kama mtakumbuka raisi alipita kwenye hiyo barabara akasimama maeneo ya haika kumuulizia mbunge hayupo kwenye ziara,mbumge kutafutwa kwenye simu anasema hana taarifa ya ziara na hayupo karibu.Ni wakati muafaka wa kumchagua mwakilishi mzuri anaye weza kusukuma gurudumu la maendeleo sawa na kazi jpm achaneni na hao wana sacoss ya ufipa.
Hizo barabara unazotaja ni project iliyoanza kipindi cha Kikwete,na imejengwa na Nchi za East Africa na Sio fedha za serikali hii ya awamu ya tano.
 
Back
Top Bottom