Duduwasha
JF-Expert Member
- Nov 3, 2010
- 5,703
- 3,653
Kuna Jamaa alienda Congo (Zaire) Katika Kutembezwa na Mwenyeji wake katika Jiji la Kinshansa wakakatiza katika mitaa karibu na soko kulikuwa na Njia ndogo na kwa mbele ya ile Njia kulikuwa na Mtu anaimba 27, 27, 27, 27, 27, 27, huku anazunguka Shimo lililokuwa mbele yake pia akilichungulia kwa ndani .. Jamaa akavutiwa Sana na ile hali ya Jamaa alivyokuwa akicheza huku analizunguka na kuchungulia lile Shimo, Mwenyeji wake akamuambia achana nae yule wakampuuza...
Baada ya mizunguko zaidi mjini pale wakawa wanarejea kwenye maskani yao walipofikia huku wakipita Njia ile ile karibu na Soko... jamaa alikuwa akimuwazia yule Mtu alivyokuwa akicheza kwani alivutiwa nae, ndipo walipofika maeneo ya karibu pale muimbaji alishabadili wimbo tena akiimba 28, 28, 28, 28 ,28 bila kuachia Pumzi, Jamaa akamsogelea Yule muimbaji achungulie ndani kuna nini Ghafla yule jamaa akaacha kuimba na akamsokomeza Mjamaa Ndani ya Shimo then akaanza kuimba tena 29, 29, 29, 29, 29, huku akilichungulia lile Shimo... Mwenyeji alibaki kaduwaa
Baada ya mizunguko zaidi mjini pale wakawa wanarejea kwenye maskani yao walipofikia huku wakipita Njia ile ile karibu na Soko... jamaa alikuwa akimuwazia yule Mtu alivyokuwa akicheza kwani alivutiwa nae, ndipo walipofika maeneo ya karibu pale muimbaji alishabadili wimbo tena akiimba 28, 28, 28, 28 ,28 bila kuachia Pumzi, Jamaa akamsogelea Yule muimbaji achungulie ndani kuna nini Ghafla yule jamaa akaacha kuimba na akamsokomeza Mjamaa Ndani ya Shimo then akaanza kuimba tena 29, 29, 29, 29, 29, huku akilichungulia lile Shimo... Mwenyeji alibaki kaduwaa