Mkenya aandika kitabu akikiponda "kikombe" cha babu wa Loliondo adai kiliua watu wengi badala ya kuwaponya

Watu walikuwa hawafi kabla ya kuja hicho kikombe?

Umeacha dawa hospitalini na kwenda kunywa mataputapu huko porini, ukifa utasema umerogwa au umejiua kwa upumbavu wako.
Na babu alishatoa tahadhari watu wasiache kunywa dawa za hospitali ,ila ndiyo hivyo waafrika tulivyo wapumbavu tukaenda kunywa dawa ya kisonono tukatupa dawa zakupunguza makali ya ukimwi
 
Hapo ndio utagundua Africa haikaliwi na watu bali aina fulani ya species yenye rangi nyeusi..

Yaani hili suala mpaka leo zaidi ya miaka mitano hakuna hata aliyefanya uchunguzi kupata ukweli wa hili na jamii kujifunza kitu??
 
Mkuu Yohana Mbatizaji, aka John the Baptist, asante for this, this is the bottom line, "Walioenda waliponywa kwa imani zao". Hata Bwana wetu Yesu Kristo, alipofanya miujiza ya uponyaji, aliwaambia walioponywa, "imani yako ndio imekuponya", wenye imani ya uponyaji, walipona, walipona, akiwemo fulani ambaye naomba nisimtaje, ili watu wasijiulize, "kumbe hata huyu alikuwa ni mgonjwa!". And I am very sorry, kwa wasio imani, walikufa.

Kinachoponya sio kikombe cha Babu, ni imani yako.
P

Paskali kikombe cha babu ilikuwa ni ushirikina 100%, na wote walioenda kupata ni washirikina. Hamna mtu mwenye imani ya kweli aliyeenda kwenye ule uhuni.
 
Mkenya huyo adai kikombe cha babu hakikuwa na uponyaji wowote kwani yeye hakupona na wengi alioenda nao kutokea Kenya walikufa baada ya kurejea nyumbani.
Akichoandika huyo mkenya kina ukweli mdogo angeandika wote walikufa angenikoma.Mwasapile ana akili nyingi mno na alilitolea ufafanuzi hilo.kuwa SI kila aendaye hospitali hata iwe na vifaa vya uhakika na madaktari bingwa wa uhakika hupona Kuna wengine hufa.Na akasema ndio maana kila hospitali kubwa duniani hata iwe ya rufaa Ina mortuary ili kuwakumbusha wagonjwa kila wanapoona Hilo Jengo la mortuary wakumbuke kuwa hiyo tiba waliyofuata kuna kufa au kupona.Aende akaandike kitabu kuhusu hospitali kubwa ya Kenya pale Nairobi Kama wote wanaooenda pale Kama huwa hawafi.Kwa mwasapile Kuna waliopona na Kuna walikufa.

Lakini huyu mwandishi asisahau pia kuandika jinsi uchumi wa kenya ulivyopaa kwa sababu ya Mzee mwasapile .Kenya airways ilimtumia Sana kujitangaza kuwa watu watembelee Kenya waone mbuga na tradional healer mwasapile! Ndege zikawa zinabeba maelfu toka nje wanatua Nairobi na makampuni ya usafiri na utalii Kenya yakawa yanabeba maelfu ya watu wa nje na Wakenya kuwapeleka kwa mwasapile na kupata mamilioni ya pesa.Kampuni za simu za kenya ziliingiza mabilioni kwa Wakenya waliokuwa wakitumia simu zao Wakiwa Tanzania kwa mwasapile nk
.Vituo vya mafuta Kenya vilifaidi kwa kujaza mafuta magari ya Wakenya waliokuwa wakienda Loliondo.Huyo mwandishi Kama kaandika only one side ya ubaya wa Mwasapile hicho kitabu Ni Cha kijinga na Cha hovyo hakistahili kusomwa na yeyote sababu hakina full story ambayo iko fair na balanced.
 
Paskali kikombe cha babu ilikuwa ni ushirikina 100%, na wote walioenda kupata ni washirikina. Hamna mtu mwenye imani ya kweli aliyeenda kwenye ule uhuni.
Tanzania Ina Uhuru na demokrasia kubwa mtu akiumwa Yuko huru kwenda hospitali au kwenda kunywa kikombe Cha kishirikina Cha babu.Wewe kinakuwasha Nini?
 
Tupo tunaopeta hadi Leo akiwemo mzalendo no.1
Nakubaliana na wewe mkuu make mzalendo no.1 nami namtilia mashaka kuhusu side effects.
Hivi mnajua hata dereva wa lori pia alikunywaga kikombe? Eeeh alikunywa ndio, unasema, kiongozi wa malaika? Eheh huyo huyo.Mbona yupo bado, tena nasikia alipona kabisa.
Magufuli si huyu hapa alipata kikombe cha babu wa Loliondo vile vile.
Sio kila aliyekwenda Semunge kupata kikombe cha Babu wa Loliondo alikuwa mgonjwa. Kuna baadhi ya Viongozi wetu walikwenda Semunge kupata kikombe cha Babu wa Loliondo kwa nia tuu ya kuonyesha solidarity lakini hawakuwa wagonjwa.

Viongozi wengine walifika Semunge sio ili kunywa Kikombe cha Babu wa Loliondo, bali walifika pale in line of duty, ili kumfacilitate mfano watu wa Tanesco waliompelekea umene wa faster, walikunywa kikombe, watu wa Tanroad waliompelekea barabara ya fasta, walikunywa kikombe akiwemo Mkuu wa Mabarabara wa enzi hizo, na watu wengine wote, waliofika Semunge kwa Babu wa Loliondo for logistical reasons, pia nao walikunywa kikombe kikombe cha Babu wa Loliondo bila kujalisha wanaumwa au la.

P
 
images.jpeg
 
Paskali kikombe cha babu ilikuwa ni ushirikina 100%, na wote walioenda kupata ni washirikina. Hamna mtu mwenye imani ya kweli aliyeenda kwenye ule uhuni.
No!, No!, No!, Mkuu Tindo, kikombe cha Babu wa Loliondo sio ushirikina, ni mitishamba au tiba asili, hadi Wazungu wanaitumia as alternative medicine, wenzetu Wachina wameiendeleza sana na kuisambaza dunia nzima as TCM (Traditional Chinese Medicine) and it real works.

Tofautisha tiba asili na ushirikina.
P
 
Jana nimeona hiyo makala citizen TV iliitwa ghost of loliondo wamehoji watu walioenda kwa babu na athari walizozipata, wengi wao wameshakufa leo j3 makala inaendelea kwa mwandishi kuhojiana na babu ambilikile mwaisapile, ni makala nzuri sana.
 
Mimi nilienda kwa Babu Loliondo. Bado ugonjwa uko pale pale. Nakubaliana na huyo jamaa wa Kenya.
 
Wengi hawakupona akiwemo huyo unayehofia kumtaja, kwani huoni vitendo vyake anamaamuzi ya kigonjwa kabisa.
Mkuu Yohana Mbatizaji, aka John the Baptist, asante for this, this is the bottom line, "Walioenda waliponywa kwa imani zao". Hata Bwana wetu Yesu Kristo, alipofanya miujiza ya uponyaji, aliwaambia walioponywa, "imani yako ndio imekuponya", wenye imani ya uponyaji, walipona, walipona, akiwemo fulani ambaye naomba nisimtaje, ili watu wasijiulize, "kumbe hata huyu alikuwa ni mgonjwa!". And I am very sorry, kwa wasio imani, walikufa.

Kinachoponya sio kikombe cha Babu, ni imani yako.
P
 
Mkuu Yohana Mbatizaji, aka John the Baptist, asante for this, this is the bottom line, "Walioenda waliponywa kwa imani zao". Hata Bwana wetu Yesu Kristo, alipofanya miujiza ya uponyaji, aliwaambia walioponywa, "imani yako ndio imekuponya", wenye imani ya uponyaji, walipona, walipona, akiwemo fulani ambaye naomba nisimtaje, ili watu wasijiulize, "kumbe hata huyu alikuwa ni mgonjwa!". And I am very sorry, kwa wasio imani, walikufa.

Kinachoponya sio kikombe cha Babu, ni imani yako.
P
Sasa Kama kinachoponya ni imani yako Kuna sababu gani ya kwenda kwa babu?
Ni kwa nini usikae tu nyumbani kwako ukanywa maji tu na kutumia imani yako ili upone?
 
Mimi nilienda kwa Babu Loliondo. Bado ugonjwa uko pale pale. Nakubaliana na huyo jamaa wa Kenya.
Wewe utakuwa na dhambi nyingi hospitali huponi kwa kikombe Cha babu huponi .Una dhambi nyingi Kama huyo mwandishi wa kitabu ambaye kashindikana hospitali zote Kenya na kashindikana kwa kikombe Cha babu.Wewe na mwandishi.muna dhambi nyingi za kutosha ndio maana Mungu haruhusu mponywe popote.
Mkamalizane na Mungu kwanza.Hakuna binadamu anawaweza kuwasaidia ninyi awe daktari bingwa au mwasapile.Mitatizo yenu na Mungu msimsukumizie Mzee mwasapile na kikombe chake.Malizaneni na Mungu kwanza
 
Hakuna cha kupeta hapa, ukishakunywa kile kikombe na kwa wengine akili zao haziwi sawa, siyo wote ni baadhi.

Wizara ya afya ilitakiwa ifanye utafiti kuhusu jambo hilo. (the body effect after using the medicine). Hadi leo kimya kabisa wakati baadhi ya watu wamedhurika hasa kiakili.

Kisheria alitakiwa Mchungaji akajibu mashitaka ya utapeli,--- hadi sasa kulingana na idadi ya vifo he seems not being apologetic. Sadly in the course he got lots of money.
Viongozi wanaona aibu kuliongelea kwa sababu na wao walishikwa akili wakawa ni miongoni mwa victims.
 
Huyo mkenya Hana akili, Ana uthibitisho gani waliokunywa wengi wamekufa. Kuna propaganda Za kijinga zinaenezwa
 
Back
Top Bottom