rodrick alexander
JF-Expert Member
- Feb 12, 2012
- 17,300
- 24,207
Huyo mkeo kibokoHabari wanajamvi,
Katika hali isiyo ya kawaida nimegundua kuwa mke wangu wa ndoa ame-hack simu yangu na kuweza ku-access mawasiliano yangu yote hasa ya sms tokea mwezi wa 10 mwaka jana 2015 na kuzihifadhi kwenye simu yake.
Sina uhakika kama aliweza kupata mawasiliano mengine tofauti na sms.
Ninasema ku-hack kwa sababu tunaishi mikoa tofauti na hivyo hakuwa na namna yoyote ya ku-access simu yangu physically toka wakati huo, pia simu yangu ambayo ni smart phone ina security (password) in case angetumia mtu aliye karibu yangu.
Nimegundua hii hacking baada ya kuwa na hali ya kutoelewana kati yetu kwa muda sasa ambapo pamoja na mambo mengine niligundua kuna taarifa zangu za siri anazozifahamu ndipo nilipoanza uchunguzi na kugundua kuwa ana hizo sms.
Miongoni mwa sms anazoshikia bango ni zile zinazohusiana na miamala ya Mpesa ambapo nimewatumia pesa ndg, jamaa na marafiki ambao sikuona umuhimu wa kumtaaifu hivyo akazijengea hoja mbali mbali ikiwemo ya uhusiano wa kimapenzi wakati si kweli!
Nimejaribu kumbana aseme amewezaje ku-access "private communications" zangu ila amegoma kabisa kuweka wazi.
Cha kushangaza zaidi ni kuwa hana utaalam wowote wa masuala ya mawasiliano!
Kwa kuzingatia usumbufu uliojitokeza kwa kuingilia mawasiliano yangu ya siri hasa kupitia mis-perception ya taarifa alizokutana nazo, nimepata wazo la kumshtaki kwa mujibu wa ile SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAO, 2015 ila nikaona kabla sijafanya hivyo nililete suala hili hapa ili nipate michango yenu ya mawazo hasa juu ya nini cha kufanya.
Suala hili limenichanganya sana hasa ukizingatia kuwa tumekuwa kwenye ndoa takribani miaka 8 sasa na tuna watoto 2.
Naombeni michango yenu ya mawazo.
Ahsante!
Siri gani hizo ilhali mko kwenye ndoa?
Au mliwekeana makubaliano ya mipaka kwenye ndoa yenu kabla hamjaifunga?
Teh teh...amesahau kuwa mkishaoana mnakuwa mwili mmoja.Sehem za siri zenu mnaonyeshana hadi kuzaa watoto wawili, Ila sim inakufanya umshtaki!
Watu mnaingiaga kwenye ndoa huku mkiwa hata hamjielewi.
Inavyoonekana mnaingiaga tu ili kukidhi matakwa potofu ya jamii.
Sasa wewe unalalamika eti mkeo anazifahami taarifa zako za siri.
Siri gani hizo ilhali mko kwenye ndoa?
Au mliwekeana makubaliano ya mipaka kwenye ndoa yenu kabla hamjaifunga?
Hovyoooo!Shindwa na ulegee Nipo kwenye ndoa Mwaka wa7 huu. Case za sms na sim kwangu hazipo.
Wewe unadhani ikizama inakula kwangu au kwa huyo mwenzio?Yaan ana makosa anajijua halafu anataka msaada. Hizo siri; sir gan ambazo mkeo hatakiw kuzijua? Ngoja ndoa yake izamee
Filthy!Mbona hizo sms sio za siri, angalia sehemu zako za siri ndo utajua kuwa mawasiliano hayo sio ya siri
Hard truth but, we live in a time where couples are allowed to touch each other's private parts but forbidden their phones,...Filthy!
Mwili mmoja ni huko Ughaibuni sio Bongo! Hapa tu mnaonekana jinsi mitazamo yenu ilivyo selfish!Teh teh...amesahau kuwa mkishaoana mnakuwa mwili mmoja.
Hivi ndoa ikizama huwa inakulaga pande ipi vile? Ndio maana mnakuwa very defensive!Yaan ana makosa anajijua halafu anataka msaada. Hizo siri; sir gan ambazo mkeo hatakiw kuzijua? Ngoja ndoa yake izamee
Itakula kwako cz ni mkeo tayar labda useme humpend unamtafutia sababu ya kumuacha na watoto wako wapate shidaWewe unadhani ikizama inakula kwangu au kwa huyo mwenzio?
Mhalifu ataendeleaje kuwa mke wangu?Halafu ukishamshitaki ataendelea kua mke wako bado au?
Ninyi wote bado mnasumbuliwa na ubinafsi, imewapasa wana ndoa kuishi pamoja haya mambo ya wote mko Tanzania hii hii halafu mwingine yuko mkoa mwingine kwa makazi ya kudumu hua siyaelewi sana na nafikiri matatizo mengi huanzia hapo.
Hata kwako itakula tuu baba. Hiyo sheria ya mtandao weka kando kwanza bt huyo mmama anafight na haki yake ya kuwa mke kwako lazima ajue usalama wake. Siku hiz magonjwa meengiHivi ndoa ikizama huwa inakulaga pande ipi vile? Ndio maana mnakuwa very defensive!