Soulmate mimi nitaungana na Babu Dark City, hayo makaratasi, hati, sijui mali ni sehemu au upande mwingine wa shilingi. Maamuzi yoyote ya kumchangua mwenzi wa maisha huambatana na vigezo 'vingine' ambavyo havihusiani na mapenzi ingawa vinacomplement kigezo cha mapenzi. So hata hayo makaratasi yanawezakuwa (au yasiwe) ni sehemu inayokamilisha u-mume au mke wangu.
Saaafi kabisa kajukuuu.....
Eti makaratasi? Yana tofauti gani nna vinyago vya kuchonga vya wale jamaa wa pale Mwenge??
Mie nilimwambia Bibi kwamba ndoa yetu ilifungwa (deep in our hearts) siku ile tulipokubaliana kwamba hatuna sababu ya kuendelea kutafuta wengine...kwamba tulishafika Kigoma mwisho wa reli....
Makaratasi hata hayana maana zaidi ya kukidhi matakwa ya kisheria na mambo mengine mengine madogo madogo...
Babu DC!!
wangu maana yule ninaemmiliki
Kihalali
Wangu aliyechukua nusu ya maisha yangu
Wangu maana ya mwili mmoja
Wangu kwa maana kiasili binadamu tunataka/penda kumiliki
Wangu maana nimeweka mipaka hapo kwamba ni territory yangu
Wangu maana mtu asinisogelee pande zangu
Wangu maana ndo alochukua moyo wangu
Wangu kwa maana ni sehemu yangu
Ya mwili wangu
Ya moyo wangu
Wangu kwa maana ya faraja yangu, furaha yangu, kicheko changu,
.......saaaaafi sana! Masuke....
Tafsiri yako nzuri sana, ila je?
Utakubaliana nami kwamba bila mapenzi na urafiki haki moja baada ya nyingine hukiukwa?!
....ukikubaliana nami, ina maana "UNAWAJIBIKA" pia kwake....
Hivi Babu Dark City..............hauna rafiki yako wa mwaka 47 kama wewe unimegee pande mjukuu wako? Najiona kama nimepitwa na wakati kwa Dot com sipo wala kwa sikinde...........naelea tu angani. Hebu ntafutie mzee nimlee ! (Soulmate hii post (haihusiani na thread - USISOME)
Yes.....kumbe kiswahili hukufeli eeh?
Btw, mzima?
haki zote? Ufafanuz plz.. Inamana kubakwa,kupigwa,kunyanyaswa pia ni haki ?jamii na sheria vinaruhuru kwa huyo mwanamke unayemmiliki?