..."'Mke Wangu'/'Mume Wangu!'"...Tafsiri!

..."'Mke Wangu'/'Mume Wangu!'"...Tafsiri!

.... Kongosho umeua ndege wawili kwa jiwe moja!
Umetafsiri kwa 'tafsiri' yako na umegusia suala muhimu kwamba "makaratasi" na viapo havitoshi kumfanya mtu ni mkeo/mumeo....

Ila, amini usiamini .... Wapo wengi tu ambao wameoana kwa ajili ya hiyo "hati" na viapo pia....and they claim every right watambulike kama Mke/Mume "halali" kukidhi matakwa yao fulani kwa muda fulani...
 
Last edited by a moderator:
....hivi, kwako wewe uliyeoa/ kuolewa, au kwako wewe uliyewahi kuoa/ kuolewa au hata wewe unayekaribia kuoa/kuolewa...

Nini tafsiri ya MKE WANGU/MUME WANGU?...fafanua plz 

View attachment 114653

Mke wangu ni first born baby girl,rafiki yangu,mwili mmoja,nyama katika nyama yangu na mfupa katika mfupa wangu,yeye ndiyo mimi na mimi ndiyo yeye, tafsiri yako Mbu ni ipi?
 
mpenzi wangu, mwenzi wangu, rafiki yangu, baba wa watoto wangu, mwandani wangu...

haha hahaaaa...
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Mke wangu ni first born baby girl,rafiki yangu,mwili mmoja,nyama katika nyama yangu na mfupa katika mfupa wangu,yeye ndiyo mimi na mimi ndiyo yeye, tafsiri yako Mbu ni ipi?

...,,,perfect!

Dalili zote za amani, upendo na masikilizano...
 
.....wowww!!! Soulmate, ur back halafu kimya kimya?!... Haya bana, karibu sana.

You are right kabisa, na kweli MwanajamiiOne, he hehehe.... Ngoja wenyewe wakuskie...

"Wangu" imegeuzwa maana au mie tu na weye soulmate ndio twajiuliza maana?!....

Mdahalo umefunguka upya kwa hilo neno, thanks Love 'wangu!'

Soulmate sijarejea nimekutumia salamu kwa Shemeji Mr Rocky kule uje unirescue maana............ mh. Ndio mie pia hii mume mke wangu yanichanganya maana hata mume wa mtu mwenye nyumba ndogo akienda kule aitwa mume wangu/ Mke wa mtu mwenye Serengeti boy naye aitwa mke wangu almuradi kizungumkuti. Ila kwa maana halisi au tuseme ile inayokubalika ni kuwa Mume wangu au Mke wangu huirepresent ile nafsi ya mwenzi wako ambaye amehalalishwa kiimani, kisheria na hata moyoni mwako umemkubali awe wako.
 
Last edited by a moderator:
Originally mume/mke ina maana yule ambaye umefunga nae ndoa bila kujalisha ni kitamaduni, kidini, kimila. Ila kunakuwepo formal ceremony ya kuwaunganisha kama mtu na mumewe. So kuna halali na haramu pia.

And legally..... Ukiweka ndani mtoto wa watu kwa miezi 6 tu tayari huyo ni mkeo Baba...!

Dah Mbu na maswali yako....! Ngoja tuendelee kupasua kichwa!
 
Last edited by a moderator:
.... Kongosho umeua ndege wawili kwa jiwe moja!
Umetafsiri kwa 'tafsiri' yako na umegusia suala muhimu kwamba "makaratasi" na viapo havitoshi kumfanya mtu ni mkeo/mumeo....

Ila, amini usiamini .... Wapo wengi tu ambao wameoana kwa ajili ya hiyo "hati" na viapo pia....and they claim every right watambulike kama Mke/Mume "halali" kukidhi matakwa yao fulani kwa muda fulani...
Soulmate mimi nitaungana na Babu Dark City, hayo makaratasi, hati, sijui mali ni sehemu au upande mwingine wa shilingi. Maamuzi yoyote ya kumchangua mwenzi wa maisha huambatana na vigezo 'vingine' ambavyo havihusiani na mapenzi ingawa vinacomplement kigezo cha mapenzi. So hata hayo makaratasi yanawezakuwa (au yasiwe) ni sehemu inayokamilisha u-mume au mke wangu.
 
Last edited by a moderator:
Soulmate mimi nitaungana na Babu Dark City, hayo makaratasi, hati, sijui mali ni sehemu au upande mwingine wa shilingi. Maamuzi yoyote ya kumchangua mwenzi wa maisha huambatana na vigezo 'vingine' ambavyo havihusiani na mapenzi ingawa vinacomplement kigezo cha mapenzi. So hata hayo makaratasi yanawezakuwa (au yasiwe) ni sehemu inayokamilisha u-mume au mke wangu.


Saaafi kabisa kajukuuu.....

Eti makaratasi? Yana tofauti gani nna vinyago vya kuchonga vya wale jamaa wa pale Mwenge??

Mie nilimwambia Bibi kwamba ndoa yetu ilifungwa (deep in our hearts) siku ile tulipokubaliana kwamba hatuna sababu ya kuendelea kutafuta wengine...kwamba tulishafika Kigoma mwisho wa reli....

Makaratasi hata hayana maana zaidi ya kukidhi matakwa ya kisheria na mambo mengine mengine madogo madogo...

Babu DC!!
 
Mzima swahiba Mbu??

Kwa wengine mke/mume wangu ni sawa na kibajaji au kikombe changu...just a property like anything else...lol!!

Nimekosea??

Babu DC!!
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: Mbu
Mke/Mume ni kiwakilishi
Wangu ni kivumishi cha kumiliki

Umiliki wa mke au mume huja baada ya tendo la uthibitisho ambalo huitwa ndoa.
Mke au mume huwa na mamlaka juu ya mwenzake kimwili.
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Saaafi kabisa kajukuuu.....

Eti makaratasi? Yana tofauti gani nna vinyago vya kuchonga vya wale jamaa wa pale Mwenge??

Mie nilimwambia Bibi kwamba ndoa yetu ilifungwa (deep in our hearts) siku ile tulipokubaliana kwamba hatuna sababu ya kuendelea kutafuta wengine...kwamba tulishafika Kigoma mwisho wa reli....

Makaratasi hata hayana maana zaidi ya kukidhi matakwa ya kisheria na mambo mengine mengine madogo madogo...

Babu DC!!

Hivi Babu Dark City..............hauna rafiki yako wa mwaka 47 kama wewe unimegee pande mjukuu wako? Najiona kama nimepitwa na wakati kwa Dot com sipo wala kwa sikinde...........naelea tu angani. Hebu ntafutie mzee nimlee ! (Soulmate hii post (haihusiani na thread - USISOME)
 
Last edited by a moderator:
Mke/Mume ni kiwakilishi
Wangu ni kivumishi cha kumiliki

Umiliki wa mke au mume huja baada ya tendo la uthibitisho ambalo huitwa ndoa.
Mke au mume huwa na mamlaka juu ya mwenzake kimwili.[/QUOTE watu8 Mke/Mume kiwakilishi nimeipenda na hapo uliposema umiliki wa mke/mume huja baada ya tendo hilo inawezekana kweli but sijaelewa unaposema tendo la ndoa unazungumzia lipi? Lile la kufunga ndoa au lile linguine lol? mana yote ni uthibitisho
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: Mbu
wangu maana yule ninaemmiliki

Kihalali

Wangu aliyechukua nusu ya maisha yangu

Wangu maana ya mwili mmoja

Wangu kwa maana kiasili binadamu tunataka/penda kumiliki

Wangu maana nimeweka mipaka hapo kwamba ni territory yangu

Wangu maana mtu asinisogelee pande zangu

Wangu maana ndo alochukua moyo wangu

Wangu kwa maana ni sehemu yangu

Ya mwili wangu

Ya moyo wangu

Wangu kwa maana ya faraja yangu, furaha yangu, kicheko changu,
 
watu8 Mke/Mume kiwakilishi nimeipenda na hapo uliposema umiliki wa mke/mume huja baada ya tendo hilo inawezekana kweli but sijaelewa unaposema tendo la ndoa unazungumzia lipi? Lile la kufunga ndoa au lile linguine lol? mana yote ni uthibitisho

Mmmh sijatumia moja kwa moja maneno 'tendo la ndoa' kuepusha mkanganyiko...

Uthibitisho niliolenga ni ule wa mtu mume kukabidhiwa mtu mke wakati wanapooana...and vice versa.

NB:
Ngono yoyote inayofanywa nje ya ndoa hiyo ngono huwezi itamka kama tendo la ndoa.
 
Last edited by a moderator:
Mzima swahiba Mbu??

Kwa wengine mke/mume wangu ni sawa na kibajaji au kikombe changu...just a property like anything else...lol!!

Nimekosea??

Babu DC!!

.....hahaha, swahiba Dark City wala hujakosea....ni mtazamo tu!
 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom