..."'Mke Wangu'/'Mume Wangu!'"...Tafsiri!

..."'Mke Wangu'/'Mume Wangu!'"...Tafsiri!

Mke/mume wangu huwa ina be applied kwa wale waliofunga ndoa na kuchagua ndoa ya mke /mume mmja tu ila kwa wale ndoa ya mme na wake wengi tunasema mume wetu kwa hiyo Mbu ongeza na mume wetu ili mada iende sawa sawia

.....ahhh, kumradhi Nivea, upo sawa kabisa. Enhee...
Hebu nawe toa mjumuisho wako,
#mumeo ana "maana" gani kwako?!
 
Last edited by a moderator:
Naona kama tunaelekea somewhere..
tukishasema huyu wa kwangu ndo na migogoro inaanza hapo
as if kwa kuwa ni wa kwako anakuwa 'anawajibika' kukupenda hata umuudhi vipi
au hata kama unam treat unfairly ?

.....umeona ee The Boss,....
We are getting there, ..."commitment" na compromises...

Mdahalo unaelekea kupata maana kamili.
 
Last edited by a moderator:
Mke wangu ni mwenza wangu na nimeweka nadhiri naye mbele ya usharika/public kwamba tutaishi pamoja kwa shida na raha mpaka kifo kitakapotutenganisha na tumekuwa mwili mmoja!! Ni nadhiri ngumu sana na inatakiwa iheshimiwe na wanandoa wote!!!
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Swali hili linajibiwa kwa kuzingatia utamaduni wa watu au imani za watu. Kikwetu ukisema mume wangu lazima awe amekamilisha taratibu zote kama mahari n.k. Kwa mume hali kadhalika. Waweza kuishi na mtu na mkabahatika kuzaa lakini bila kukamilisha taratibu SI MUMEO/MKEO. Katika madhehebu ya dini napo ni hivyo hivyo. Kwa mtu binafsi tafsiri yake ni mwandani, rafiki yako na zaidi ya yote faraja ya moyo.
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Ni swali gumu kwa kweli, kila mtu ana definition yake tofauti. Unaweza kuwa umeoana kihalali na mtu, tuseme Shabani, lakini 'mume wangu' akawa mwingine kabisa, tana anaitwa Emanuel.

Kuna saa unakuta kaoa mtu kihalali, ila akiwa kwa watu anasema 'ila huyu niliyenaye basi tu, mie mke wangu bana alikuwa fulani'.
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
simple sana hahahahahaaa...... mke wangu ni mke wa mume wangu, asante kwa kushiriki
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Mke ni nomino na wangu ni kivumishi kimilikishi, maana yake ni mwanamke unayemmiliki na una haki zote na wajibu naye, kijamii na kisheria pia.

haki zote? Ufafanuz plz.. Inamana kubakwa,kupigwa,kunyanyaswa pia ni haki ?jamii na sheria vinaruhuru kwa huyo mwanamke unayemmiliki?
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Soulmate Mbu, huu sasa uchokozi. Mie hata sielewi tena siku hizi........... mume wangu?? hata wapenzi tu wa kawaida huwaita wanaume wao mume wangu.
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: Mbu
mkuu Mbu mi nafikiri haya maneno yana maana hii:

kwanza tuone origin ya maneno haya "mme wangu" na "mke wangu" nionavyo mimi yametokana na jinsia zote mbili yaani mwana mke na mwana mme kwa hiyo linapokuja swala la mume wangu hii inamaanisha kuwa mwanamke amemchagua huyo mmoja wa jinsia ya kiume kuwa wake peke yake kati ya wengi walio wa kiume na hivyo kustahili kumuita "mme wangu",vivyo hivyo mke wangu inatokana na ukweli kuwa mwanaume anakuwa amemchagua mtu mmoja wa jinsia ya kike kuwa wake peke yake kati ya wengi wa jinsia hiyo na hivyo kumuita "mke wangu",lakini ikumbukwe hiyo ni mara baada ya kuthibitisha mbele ya mashahidi ambapo ndo kuna ndoa za kimila,kidini au kiserikali.

Hope nimeeleweka mkuu Mbu.
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: Mbu
.....wowww!!! Soulmate, ur back halafu kimya kimya?!... Haya bana, karibu sana.

You are right kabisa, na kweli MwanajamiiOne, he hehehe.... Ngoja wenyewe wakuskie...

"Wangu" imegeuzwa maana au mie tu na weye soulmate ndio twajiuliza maana?!....

Mdahalo umefunguka upya kwa hilo neno, thanks Love 'wangu!'
 
Last edited by a moderator:
Ni swali gumu kwa kweli, kila mtu ana definition yake tofauti. Unaweza kuwa umeoana kihalali na mtu, tuseme Shabani, lakini 'mume wangu' akawa mwingine kabisa, tana anaitwa Emanuel.

Kuna saa unakuta kaoa mtu kihalali, ila akiwa kwa watu anasema 'ila huyu niliyenaye basi tu, mie mke wangu bana alikuwa fulani'.

...... Kongosho umenielewa vizuri sana. Ndio maana nikaomba tafsiri ya kila mmoja wa wachangiaji juu ya hili...
 
Last edited by a moderator:
..... Nsuri, umejibu vyema ila hapo ulipoandika nadhiri ngumu...

Ugumu wake ni upi? Unamchukuliaje mke0 kwani!?
 
Last edited by a moderator:
'mme wangu/mke wangu' ni mtu ambaye nimewahi kuwa nae kwenye mahusiano, nikamkubali rohoni na mwilini, na atatimiza kwa kiwango ninachokikubali maana na matarajio ya mume/mke kwangu. Mtu wa aina hii ni rahisi kuwasialiana naye kimaneno na hata kihisia. Na ikitokea hata kuna ugomvi mkubwa kiasi gani, ni rahisi kusameheana sababu kuna kitu kimewaweka pamoja.

Nimewahi kuona mdada kaachwa na kijana akaenda kuoa mwanamke mwingine. Akalia weee, baada ya kama miaka kadhaa wakarudiana kwa siri na wakati yule dada ana mmewe. Kumuuliza tatizo nini, akajibu tu 'yule ndio alikuwa awe mme wangu, basi tu ndugu zake walimwolea kijijini kwao' How absurd!?!

Ndio maana kuna saa unakuta mke au mme ana shida, lakini anaenda kukisimulia kibuzi chake cha zamani. SI kwamba hawezi msimulia mmewe aliyenaye, labda kwa sababu kadhaa mme aliyenaye hawezi kuelewa au hawaoni jambo hilo katika mtazamo unaofanana, au unakuta yeye anakiona kibuzi cha zamani kilikuwa kiwe mmewe halali, basi tu alipokonywa na walimwengu.

Kwa hiyo, mie kuwa na vyeti na mtu kihalali mbele ya umati, haitoshi kuwa mme/mke wangu kiuhalisia. Ingekuwa hivyo usaliti katika ndoa ungekuwa mdogo sana, mioyo ya watu misitu.

It's complicated I guess.

...... Kongosho umenielewa vizuri sana. Ndio maana nikaomba tafsiri ya kila mmoja wa wachangiaji juu ya hili...
 
  • Thanks
Reactions: Mbu
Mie nikijaribu ku-redefine nitasema 'mke/mme wangu' ni mtu uliyeweka naye nadhiri moyoni mwako kuwa mwenza wa maisha yako. Si lazima kifo kiwatenganishe, walimwengu wanaweza kuwatenganisha tu. Ukabaki, ila fulani ndio alikuwa anatakiwa awe mke wangu.


Imagine umempenda binti, unamepeka posa, kwao hawakutaki,binti akaondolewa na kupelekwa mbali nawe. Maisha yakaenda na wewe ukaamua kuoa tu. Inategemea, kuna wengine wanaweza ku-cope na kuendelea na maisha mapya, wengine wanaoa huku mawazo yakiwa nyuma.


Public has nothing to do na ndoa, hata mkilishana yamini nyie wawili tu, inaweza kuja kuwa ndoa tamu sana kwenu.

Mke wangu ni mwenza wangu na nimeweka nadhiri naye mbele ya usharika/public kwamba tutaishi pamoja kwa shida na raha mpaka kifo kitakapotutenganisha na tumekuwa mwili mmoja!! Ni nadhiri ngumu sana na inatakiwa iheshimiwe na wanandoa wote!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom