Mke wangu kaninasa kibao, nifanyeje?

kyanyangwe

JF-Expert Member
Oct 31, 2018
1,147
2,746
Habari za leo wananchi wenzangu wanyonge. Poleni na msiba wa kiongozi wetu sisi wanyonge.

Ndugu zangu, naombeni ushauri wenu wa mawazo.

Leo nilikuwa nimekaa na wife tunacheck tv, ikaingia message kwenye simu yangu, wife akaichukua haraka haraka na kuisoma. Nikashangaa ameniangalia usoni kisha akanilabua kibao kwenye shavu, akanirushia simu yangu kisha akaingia chumbani.

Mimi nikaisoma ile message ilikuwa imetoka kwa mdada mmoja tumezoeana kutaniana, yeye huwa anapenda kunitania kwa kuniita husband nami namuita wife, so nimeshangaa wife wangu hajaniuliza kitu badala yake kanipa kelebu.

Je, nifanyaje wakuu?

1619251300345.png

 
Back
Top Bottom