Mke wangu kabadilika kimuonekano

Mke wangu kabadilika kimuonekano

kitambiflat

Senior Member
Joined
Oct 16, 2015
Posts
163
Reaction score
228
Salaam wanajamvi,

Nimeishi kwenye ndoa miaka mitano sasa changamoto kubwa mke wangu amebadilika sana sio yule wa enzi zile.

Alikuwa mnene wastani, na kila kiungo cha mwili wake kilionekana kipo vizuri hapa namaanisha shape lakini sasa amepoteza muonekano wake amenenepa hovyo tumbo limekua kubwa kuliko makalio.

Kifupi amepoteza mvuto mbele ya macho yangu, nimejaribu kumsisitiza na kumueleza madhara ya unene amejitahidi lakini hapungui! Yaani shapeless sina hamu nae tena na ana mtoto wangu.

Wana JF nisaidieni kwa ushauri kijana mwenzenu.
 
Hii ni changamoto kwa wanawake wengi, haswa ukizingatia life style zetu.

Nenda nae taratibu, azingatie mazoezi na discipline katika ulaji.
It ll take time tho, kuwa mvumilivu.
 
Nahisi unawaza kuchepuka tuu hapo as a solution.

Anyway, unaweza kutumia participatory way , mazoez mnaenda nae, diet mnafanya nae.... Na kum soap soap Basi, mnunulie tupafyumu, na mafuta mazuri....


Pia jiandae kisaikolojia kukubaliana na mabadiliko, huenda zaman alikuwa msichana ila amekuwa mama now...
 
Si umemzalisha ulitegemea abaki vile vile apo utataka ushauri uambiwe mwache, uyo ni mkeo uliyefunga nae ndoa vumilia tu acha hzo tamaa
Kuzaa siyo hoja,usipotoshe umma please!!.......Mbona wanawake kibao kama vile akina Zamaradi,Zarie,Angelina jolie na wengine wamezaa watoto wengi tu ila wana shape kali???........Hoja hapa ni kula ovyo,uvivu wa kufanya mazoezi na kutokujipenda!
 
"Jogging"

Mvumilie mkeo kwenye raha na shida wala usimchoke. Ipo siku atakuelewa
 
Mbona rahisi tu; pale 6 kwa 6 mkiwa kwenye tendo mpe style ngumu kila siku.

Hayo ni mazoezi tosha kabisa
 
eti tumbo kumbwa kuliko makalio...

inauma sana mke wako ana kitambi alafu baba mwenye nyumba na kimbaombao
 
Suluhisho ni kumpa stress za kutosha,anza kurudi nyumbani saa sita usiku na ukifika home we chati jamii forums mpaka saa tisa usiku,kila mboga mgombeze ina chumvi nyingi,akiandaa breakfast mwambie unawahi kazini,zusha safari za kikazi kila wiki,then mkatalie katakata asiguse simu yako,baada ya miezi miwili njoo utupe mrejesho
 
Kuzaa siyo hoja,usipotoshe umma please!!.......Mbona wanawake kibao kama vile akina Zamaradi,Zarie,Angelina jolie na wengine wamezaa watoto wengi tu ila wana shape kali???........Hoja hapa ni kula ovyo,uvivu wa kufanya mazoezi na kutokujipenda!

hao ndiyo wanawake wengi mkuu? hao ni wachache mno ukilinganisha na ambao shep zimeharibika.

cha msingi ni kwamba shepu halisi ya mwanamke unaipata baada ya kuwa amezaa, ile tunayoiona wakati wa usichana wao na ambayo ndio inayotupelekea tuwaoe baada ya muda mfupi inabadilika pale tunapokuwa tumewazalisha.


Na ndiyo hapo tunapowachukia wake zetu na kuwachoka mapema wakati bado tuna safari ndefu ya kuendelea kuishi nao.

Kwa ambao hawajaoa bado ni bora ukaoa mwanamke skeleton kabisa kama na wewe ni miongoni mwa wanaopenda wanawake wembamba ili pale anapozaa afikie kiwango chako kwani ataongezeka tu.

na mleta mada mvumilie mkeo, mfanyishe diet na mazoezi ya kukata tumbo.
 
Aisee! Kuna binti mmoja nilimpenda sana. Yaani alikuwa mzuri ajabu. Mi nikaenda shule kuja kurudi baada ya miaka mitatu kumbe keshaolewa. Yaani niliumia mno.

Baada ya kupotezana naye mwaka huu May nikakutana naye Posta Mpya. Uwiii! Yaani Magreth wangu kanenepa sanamu la Michelin cha mtoto. Kumuuliza Magreth vipi anasema ana watoto wanne tayari na akalaumu uzazi na maisha ya deko (aliolewa kwa matajiri). Yaani hata chura kwishnei kabisa yaani nilisikitika sana.

Kwa kuwa huyo ni mkeo mnaweza kuanza kufanya mazoezi na kufanya diet pamoja lengo hasa likiwa ni kumsaidia yeye. Ila inabidi uwe careful usimuumize kisaikolojia.

By the way, amenenepaje yeye pekee wakati mnaishi wote na yeye ndiye mama wa nyumba? Na alipoanza kunenepa ulikuwa wapi kuingilia kati KINAMNA mapema?
 
Hiyo ndio shida ya kuoa mtu KISA SHAPE au SURA.
Sura inabadilika, hata isipobadilika macho yana tabia ya kuzoea kitu so with time utamzoea tu na kumuona wa kawaida.
Shape pia inabadilika....

Ila ukioa mwanamke mzuri wa mwenendo na tabia njema pamoja na roho na moyo mzuri.... That NEVER FADE
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom