Mke wangu hapendi ndugu zangu.

Mke wangu hapendi ndugu zangu.

Tarime one

JF-Expert Member
Joined
Nov 12, 2013
Posts
2,246
Reaction score
1,742
Jamani wana JF naomba ushauri wenu,niko ndani ya ndoa zaidi ya miaka kumi tuna watoto 3,kinachofanya niombe ushauri ni kwamba baada ya kufunga ndoa ndani ya mwaka 1 familia yangu ilianza kuwa na migogoro isiyoisha,tatizo mke wangu hapendi ndugu zangu hasa wazazi wangu,imefikia ndugu wa pande zote mbili wazazi wa mke na wazazi wangu hawasalimiani,kisa anadai mie nafanyiwa maamuzi na wazazi wangu,imefikia mahala sasa hataki kuwasalimia hata wazazi wangu,nifanyeje?
 
Jaman jaman!
Kile kipindi cha upenz na uchumba sio kipindi cha kutom.bana na kuhongana tu!
...
Ukilikoroga kule, lazima ulinywe huku!
Ona sasa kila ushauri haufai!
Pole!
 
Hapo pagumu, na umeshazaa nae dah!.. bhana mwambie ajifunze kuwapenda wazazi wako vyenginevyo...
 
....pole bro,,,, think ur kids......hapo hamna ndoa tena,,,,so miaka 9 migogoro na watoto mnazaa tuu...mkae chini mkubaliane namna bora ya kutunza watoto wenu,,, then think another happyness life,, tuliumbwa tuyafurahie maisha sio mateso....
 
Wazazi wako ni wazazi wako na hakuna wa kukutenga nao. Walikuelekeza jinsi ya kuishi hadi ukawa kijana morani na ukaja kuoa. Weka issue za familia yako mbali na issues za wazazi wako. Timiza wajibu wako nyumbani, na wajibu wako kwa wazazi.

Wa kulaumiwa ni wewe. Unashindwa jinsi ya kuwasiliana na wote. Hivi kuna siku ulishasema home 'jane yule receptionist, kaniambia friji za zec ndo nzuri kwa hiyo nitanunua' ? Kuwa muangalifu na taarifa unazopeleka kati yao. Namaanisha kuwa mwanaume. Jipange.
 
Huyo mkeo inaonesha unamuendekeza sanaaaa...we miaka tisa yote unapandwa kichwani tu!!!

Rudisha kwa wazazi wake huko wakamfunze namna ya kuheshimu mume na wazaa chema asilete umajinuni...
 
Lazima yalianzia mbali na wewe kiunganishi cha hizi pande mbili ulizembea sehemu!

Wewe na mkeo wote ni watoto kwa wazazi wako na wake,hebu jishusheni na mjifunze kunyenyekea hata kama hamuwategemei kwa chochote. Ongea na mkeo asahau yaliyopita,kawaombeni radhi wazazi maisha yaendelee kila mmoja akiwa kwake,mkikutana msalimiane ikipita 2weeks na zaidi watoto pigeni simu kuwajulia hali basi.

Usikubali kuwa katika nafasi ya kuchagua kati ya wazazi na mkeo na watoto maana kila kundi lina nafasi yake kwako na hakuna kundi rahisi wewe kulitelekeza hapo.

Mwambie mkeo Sikio Halizidi Kichwa!
 
Jamani wana JF naomba ushauri wenu,niko ndani ya ndoa zaidi ya miaka kumi tuna watoto 3,kinachofanya niombe ushauri ni kwamba baada ya kufunga ndoa ndani ya mwaka 1 familia yangu ilianza kuwa na migogoro isiyoisha,tatizo mke wangu hapendi ndugu zangu hasa wazazi wangu,imefikia ndugu wa pande zote mbili wazazi wa mke na wazazi wangu hawasalimiani,kisa anadai mie nafanyiwa maamuzi na wazazi wangu,imefikia mahala sasa hataki kuwasalimia hata wazazi wangu,nifanyeje?


Pamoja na hayo, Tatizo la Wanawake wengi, hususani africa, Wanataka wakiwa na mume basi asiwe na mahusiano tena na ndugu/Jamaa/Marafiki/

Lakini bila kujiuliza kuwa pia una ndugu, yeye atataka uwe wake tu, yaani hata usimsalimie mtu mwingine, Na hapo ndipo atapoanzisha vimbwanga, Hebu fikiria tu kidogo kama huyo mke wako hawapendi wazazi wako, Huoni pia wewe amekaa na wewe tu ili siku ziende.
"" ukipenda boga Upende na Ua Lake"""

Huyo mwanamke amekosa sifa ya kupenda boga pamoja na ua lake.

Kumbuka Udugu hauvunjiki milele lakini Ndoa huvunjika,;;
 
Ukioa lazima utimize majukumu kulingana na nafasi ya kila mtu mzazi wazazi wapate haki yao na mke nae apate haki yake kama mke na usiruhusu watu wengine waingilie ndoa yenu masuala yanayogusa ndoa yenu jitahidini muyamalize nyinyi mwenyewe na kama utahusisha mzazi akiegemea upande mmoja hapo tayari ni tatizo. Penda wazazi wako mkeo ajue wale wazazi wako unawathamini na yeye anapaswa kuwathamini pia penda mkeo familia yako ijue kuwa unampenda mke wako nao wanatakiwa kuheshimu ndoa yako basi kila kitu kitaenda sawa
 
Pole sana kaka, jarbu kumwelekeza taratbu atakuelewa 2! ila n tabia mbaya sana, au jarbu kuchunguza vzur kutakua na sababu inayomfanya mke wako kua ivo!
 
Cha kwanza Mzee, ukishaoa, Nenda mbali na wazazi wako. Hata maandiko yanasema Mtu mume atamuacha Babaye na Mamaye, nao wataambatana kuwa mwili mmoja. Kama Muumbaji anasema UTAWACHA WAZAZI WAKO, kwanini tunang'ang'ania kukaa nao TUKASHAOA??????? [Mwanzo 2 : 24 - Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.] (Si busara kuishi wewe, mkeo, ndugu, etc kwenye fensi moja) kama vivyo ndivyo mnavyoishi. Mkeo ni mwanadamu ana madhaifu yake, vivyo hivyo wazazi wako na ndugu zako nao ni wanadamu wana madhaifu yao. kwa hiyo hapo ni kuchunguza pande zote mbili.


Pili Jichunguze namna unavyomshirikisha mkeo kwenye maamuzi yako, Pia anagalia unavyowashirikisha wazazi kwenye maamuzi yako, isijekuwa unayopaswa kushauriwa na mkeo, unaenda kuwaomba ushauri wazee nakadhalika.

Tatu ongea na mkeo vizuri ili ujue shida ni nini hadi kufikia kuchukiana kiasi hiko, ukijua, fanyia kazi chanzo na sio matokeo unayoyaona.

Jamani wana JF naomba ushauri wenu,niko ndani ya ndoa zaidi ya miaka kumi tuna watoto 3,kinachofanya niombe ushauri ni kwamba baada ya kufunga ndoa ndani ya mwaka 1 familia yangu ilianza kuwa na migogoro isiyoisha,tatizo mke wangu hapendi ndugu zangu hasa wazazi wangu,imefikia ndugu wa pande zote mbili wazazi wa mke na wazazi wangu hawasalimiani,kisa anadai mie nafanyiwa maamuzi na wazazi wangu,imefikia mahala sasa hataki kuwasalimia hata wazazi wangu,nifanyeje?
 
Huwa napata shida sana kusikia mtu unakaa na mwanamke kwa miaka yote hiyo 10 na sasa ndio unakuja kuomba ushauri,hiyo miaka yote ulikuwa unaishije?Mara nyingi ushauri katika ndoa huwa mzuri kwa mtu anayekufahamu au anayewafahamu maana sisi wadau tutachukulia tatizo lako na kukushauri kwa namna ambayo tunaona inafaa huku kwako hali inakuwa tofauti.
Mshenga wako kaenda wapi?
 
umeshindwa kubalansisha kati ya mkeo na wazazi wako

Mke anapolalamika unafanyiwe maamuzi na wazazi wako ni kweli? Usikute wewe ndo aina ile ya wanaume ambao hata kununua kijiko mpaka ukaseme kwa wazazi wako???? Su ndugu zako watata?

Kaa na mkeo uzungumze

Halafu wazazi wanajiingizaje kwenye vita visivyowahusu???

Fix hilo tatizo

Nahisi kama kuna vita ya kugombra upendo kati ya wazazi wako na mkeo

Unless kama mkeo ana roho mbaya tu ya kuzaliwa mthibiti



 
Huyo mkeo inaonesha unamuendekeza sanaaaa...we miaka tisa yote unapandwa kichwani tu!!!

Rudisha kwa wazazi wake huko wakamfunze namna ya kuheshimu mume na wazaa chema asilete umajinuni...

isije ikawa yeye, mwanaume, ndiye anayetakiwa kurudishwa kwao akafunzwe jinsi ya kuishi na mke.. ni ngumu ku-judge kutokana na jinsi alivyoileta sory yenyewe, haijakamilika.
isije kuwa ni yule mwanaume anayemwambia mkewe "mama kasema tusinunue gari tununue shamba, mama kasema mtoto asiende shule hii aende ile, mama kasema bla bla bla...". atueleze vizuri
 
Jamani wana JF naomba ushauri wenu,niko ndani ya ndoa zaidi ya miaka kumi tuna watoto 3,kinachofanya niombe ushauri ni kwamba baada ya kufunga ndoa ndani ya mwaka 1 familia yangu ilianza kuwa na migogoro isiyoisha,tatizo mke wangu hapendi ndugu zangu hasa wazazi wangu,imefikia ndugu wa pande zote mbili wazazi wa mke na wazazi wangu hawasalimiani,kisa anadai mie nafanyiwa maamuzi na wazazi wangu,imefikia mahala sasa hataki kuwasalimia hata wazazi wangu,nifanyeje?
Piga chini yeye hajui wazazi wanapaswa kuheshimiwa bila kujali wanakukera au la!
Anafikiri sasa kwa kuwa na hao watoto 3 basi haiwezekani kumuacha mpe red card au jaribu basi hata yellow card kama hiyo red unaogopa!!!!!!!!!!!!
 
Dah! Ngumu hadi kushauri, Manake kama ni kidonda hili ni donda ndugu! ila bahati mbaya zaidi umejitakia mwnyw! Hapo lazima ufanye maamuzi sahihi la sivo, unakosa baraka za wazee wako na watoto wako hawakuelewa huko mbeleni!

Ngoja! Nikuambie hili kuna mzee kijijini alikuwa na wake wawili, kila siku ilikuwa ugomvi kati ya wake zake na watoto wake wakaanza kujenga uhasama, baada ya muda mrefu kupita akaamua leo iwe mwisho wa matatizo ya familia yake! akawaweka kikao wake zake akawaeleza waamue wamalize tofauti zao au la anawaacha wote! wanawake wakadhani mchezo baada ya masaa mawili kupita akawaapa talaka wake zake wote wawili!

kwa sheria ya dini yao wanatakiwa wakae kwa muda kabla ya kurudi kwao! basi baada ya talaka wale wanawake wakaanza kuongea vizuri kbs, na mwisho akawarejea wake zake na kwa sasa anaishi nao vizuri! imeshapita miaka zaidi ya 5-6 wanawake wanaelewana ingawa sio sana ila wanaishi kama familia moja!

So fanya uamuzi mgumu kumaliza tatizo hili otherwise, imekula kwako mazima.
 
Jamani wana JF naomba ushauri wenu,niko ndani ya ndoa zaidi ya miaka kumi tuna watoto 3,kinachofanya niombe ushauri ni kwamba baada ya kufunga ndoa ndani ya mwaka 1 familia yangu ilianza kuwa na migogoro isiyoisha,tatizo mke wangu hapendi ndugu zangu hasa wazazi wangu,imefikia ndugu wa pande zote mbili wazazi wa mke na wazazi wangu hawasalimiani,kisa anadai mie nafanyiwa maamuzi na wazazi wangu,imefikia mahala sasa hataki kuwasalimia hata wazazi wangu,nifanyeje?

Piga Windows Chini..
 
Jamani wana JF naomba ushauri wenu,niko ndani ya ndoa zaidi ya miaka kumi tuna watoto 3,kinachofanya niombe ushauri ni kwamba baada ya kufunga ndoa ndani ya mwaka 1 familia yangu ilianza kuwa na migogoro isiyoisha,tatizo mke wangu hapendi ndugu zangu hasa wazazi wangu,imefikia ndugu wa pande zote mbili wazazi wa mke na wazazi wangu hawasalimiani,kisa anadai mie nafanyiwa maamuzi na wazazi wangu,imefikia mahala sasa hataki kuwasalimia hata wazazi wangu,nifanyeje?

Mpe talaka

 
Back
Top Bottom