Mke wangu hajui kusamehe hata ukiomba msamaha

Mke wangu hajui kusamehe hata ukiomba msamaha

and 998 others

JF-Expert Member
Joined
Jun 27, 2012
Posts
28,232
Reaction score
39,715
Mimi nimeoa yapata miaka 5 sasa na tumejaliwa watoto wa 3 katika ndoa yetu na mke wangu, sasa shida inakuja imetokea nimefanya kosa na kuomba msamaha kwa mke wangu, itachukua hata siku 4 au 5 "kusema nimekusamehe"

Hapo utadhani umesamehewa lakini siku imetokea ugomvi/kutokuelewana atakumbushia makosa yako yote toka enzi za uchumba na anakuambia hakusamehe kipindi kile.

Lakini yeye hata kama amekosea ukamuambia kistaarabu pale alipokosea hujihami kwa kupaza sauti kuwa amechoka na hii ndoa na kupiga makabati kisha hutoka chumbani na kubamiza mlango kwa nguvu.

Ushauri tafadhali
 
pole ndg. Joshua hizo ndio changamoto za ndoa, mimi nina mke mchaga (Mkibosho) siku mkikorofishana anabwabwaja ovyo mpaka unapata hasira ya kumtwanga ngumi maana hachagui maneno ya kuongea nilijaribu kumuonya naona akawa haelewi,

mara ya mwisho nikamuambia ukiendelea na hayo MAKELELE yako na KUTOKUSAMEHE ndo utakuwa mwisho wa mimi kuishi na wewe hapa home (nitaondoka nikapange chumba niishi huko) akajibu kwa dharau kuwa YUPO TAYARI TUACHANE,

Bro! mwezi uliofuata nilipanga chumba maeneo ya MIANZINI (Arusha) nikamuachia nyumba na gari. Na ninatuma pesa ya matumizi ya mtoto. Sasa nina amani hakuna wa kunipigia KELELE
 
Well said Boss. Huyo ambae hasamei atakuwa ama background yake ilikuwa mbaya toka utotni (alikuwa anadharauliwa tok utotoni) au WIVu wa kijinga tu. Kosa la miaka na miaka unakaa nalo la nini?
 
Insecurities, ukikosea kuwa fasta kusema samahani aikubali au hapana ni juu yake..
Asipotaka kukusikiliza kama kakosea... Mwandikie msg ndeeefuuu kwa simu ... Itakayomsuta moyoni... Of coz atasoma kama

kusikiliza hataki. Then kaa kimya endelea na shughuli zako. Itamla kichwani kwa nini hujibizani nae tena (km huwa unajibizana nae) taratibu. Taratibu utaona changes.

NB: uwe makini asikupande kichwani ndugu maana wanawake hatukawii tukiona mtu kaamua kuwa chini kueousha ugomvi, misimamo yako ibaki pale pale as a man.
 
Ndoa huja na gharama kadha wa kadhaa ikiwemo uvumilivu kwa mwenzake na kuombana msamaha ikiwa mwenzako hasamehi je yeye hakosei? ni jambo jema kuelekezana kwa upole hasa kwa wadada (Wanawake) maana wao ni viumbe dhaifu na wanahitaji kulelewa na kuelekezwa kwa upole ikiwa hataki kusamehe wakati wote basi ni bora ukampa muda zaidi wa kutafakari makosa yako kama hawezi pia, ni bira kuachana kuliko kuendelea kuumizana
 
pole ndg. Joshua hizo ndio changamoto za ndoa, mimi nina mke mchaga (Mkibosho) siku mkikorofishana anabwabwaja ovyo mpaka unapata hasira ya kumtwanga ngumi maana hachagui maneno ya kuongea nilijaribu kumuonya naona akawa haelewi, mara ya mwisho nikamuambia ukiendelea na hayo MAKELELE yako na KUTOKUSAMEHE ndo utakuwa mwisho wa mimi kuishi na wewe hapa home (nitaondoka nikapange chumba niishi huko) akajibu kwa dharau kuwa YUPO TAYARI TUACHANE, Bro! mwezi uliofuata nilipanga chumba maeneo ya MIANZINI (Arusha) nikamuachia nyumba na gari. Na ninatuma pesa ya matumizi ya mtoto. Sasa nina amani hakuna wa kunipigia KELELE
Very bad move ever. Kama umeoa kinanda ni siri yako ya ndani and nobody is perfect. Uvumilivu ni muhim sana.
 
wanandoa wanapaswa kumuweka Mungu mbele zaidi wanahitaji uvumilivu na Heshima baina yao. Magomvi yasiwe matangazo kila mtu anajua nyumbani (watoto, house girl, dereva, mlinzi n.k) Wa kufanikisha hili ni MKE (kuwa Shock Absorber) kutuliza hasira na kuja kuongelea baadae mkiwa katika hali tulivu
 
HUJIHAMI kwa kupaza sauti kuwa amechoka na hii ndoa na kupiga makabati kasha hutoka chumbani na kubamiza mlango kwa nguvu. Ushauri tafadhali

Kama ameanza hiyo tabia hivi karibuni inawezekana ana mchepuko unaomdanganya.

Hapo kwenye red...akirudia kusema hivyo...mwambie mlango uko wazi anaweza kutafuta sehemu nyingine kwa kupumzika. Jino kwa jino...ndoa ni ibada na si mateso.
 
Ukishajua madhaifu ya mwenzio tafuta namna ya kukabiliana nayo/ kuishi nayo huku mkiboredha ndoa yenu
 
wanawake tumekua na tabia fulani mbaya na chafu.kwasababu kunawatetea haki zetu basi tumemfanya mwanaume adui mkubwa.hivi kama mtu unampenda unampa tamu iyo jeuri unatoa wap?mbaya zaidi amekuzalisha haitoshi kukuthibitishia kua huyo ni mwanaume?pili na kubwa ukiona mtu anaguts zakujibu pumba na hayuko tayari kukusamehe anahitaji break time sivyo atafanya jambo ambalo hutaamini.

ushauri wangu aende nyumbani kwao apumzike kidogo kwa aibu ya kurudishwa nyumbani atajifunza.
hapo utajua kama anataka maisha na wewe au hataki.
ladies tuache ukorofi alafu tuna play victims sio sawa
 
pole ndg. Joshua hizo ndio changamoto za ndoa, mimi nina mke mchaga (Mkibosho) siku mkikorofishana anabwabwaja ovyo mpaka unapata hasira ya kumtwanga ngumi maana hachagui maneno ya kuongea nilijaribu kumuonya naona akawa haelewi, mara ya mwisho nikamuambia ukiendelea na hayo MAKELELE yako na KUTOKUSAMEHE ndo utakuwa mwisho wa mimi kuishi na wewe hapa home (nitaondoka nikapange chumba niishi huko) akajibu kwa dharau kuwa YUPO TAYARI TUACHANE, Bro! mwezi uliofuata nilipanga chumba maeneo ya MIANZINI (Arusha) nikamuachia nyumba na gari. Na ninatuma pesa ya matumizi ya mtoto. Sasa nina amani hakuna wa kunipigia KELELE

Mkuu...matatizo hayakimbiwi
 
pole ndg. Joshua hizo ndio changamoto za ndoa, mimi nina mke mchaga (Mkibosho) siku mkikorofishana anabwabwaja ovyo mpaka unapata hasira ya kumtwanga ngumi maana hachagui maneno ya kuongea nilijaribu kumuonya naona akawa haelewi, mara ya mwisho nikamuambia ukiendelea na hayo MAKELELE yako na KUTOKUSAMEHE ndo utakuwa mwisho wa mimi kuishi na wewe hapa home (nitaondoka nikapange chumba niishi huko) akajibu kwa dharau kuwa YUPO TAYARI TUACHANE, Bro! mwezi uliofuata nilipanga chumba maeneo ya MIANZINI (Arusha) nikamuachia nyumba na gari. Na ninatuma pesa ya matumizi ya mtoto. Sasa nina amani hakuna wa kunipigia KELELE
kaaah to bad.wanawake sie achen tu
 
kwa hili la blessings niwaelekeze dada zangu kuwa msitumie midomo yenu vibaya jamani. Mumeo/mpenzio kakuudhi maneno kibao na matusi juu kasha kupaza sauti kama Sheikh anapiga Adhana, HAIFAI hata kidogo basi hata kama una hasira jizuie kidogo basi usitamke hayo maneno mabaya. Ila tafuta wasaa mkiwa mmetulia umueleze kwa umakini. Wanawake wengi hudhan kupayuka na kujaza umati ni sifa
 
Kama ameanza hiyo tabia hivi karibuni inawezekana ana mchepuko unaomdanganya.

Hapo kwenye red...akirudia kusema hivyo...mwambie mlango uko wazi anaweza kutafuta sehemu nyingine kwa kupumzika. Jino kwa jino...ndoa ni ibada na si mateso.

Mwenzako ana watoto watatu, wakiachana watoto ndio watapata shida, ndo maana inakuwa ngumu kwake kufanya maamuzi magumu mpaka akaja kuomba ushauri hapa jukwaani. Mimi nahisi mkewe ana maswala yanayomkera rohoni ambayo amekosa pa kuyasemea au mumewe ameshindwa kumtatulia. Akae naye chini amuulize anataka nini pengine, au muda mwingine awe atampa muda wa Kutoka yeye na wanaye aende sehemu kwa mapumziko ya siku mbili au tatu. Pengine ni stress tu za kulea ukizingatia miaka mitano ya ndoa mna watoto watatu.
 
Mi tarehe 1 March mwaka huu alihisi namba fulan kuwa ni ya mchepuko (ila ni kwel) akaiandikia sms ya kimapenz, nao nchepuko wangu ukaingia kwenye taget, kumbe umetegwa. Baadae varangati likazuka hapa home, nikamsihi kwamba tutaongea usiku chumban kwetu.

Sasa imekuwa kero, mi nimemwomba msamaha lakini akisamehe kesho yake ngoma inarudi upya, baada ya kusamehe mara 4 na bado ananitukana tena hadharani mbele ya familia ndipo nikampapasa kidogo, huyo polisi nami nikamfuata hukuhuko polisi, akashitaki , polisi nikawaambia tatizo lake wakampuuza tena kwa kumtukana kwamba hatumii busara.

Kasema tunaachana kumbe ametafta madalali kuuza viwanja vyetu 4 hapa mwz, nikagundua nikamwambia viwanja vyote vimenunuliwa kwa jina langu,nikamwambia kama ndoa imekushinda basi itakushinda na bado nitakufunga kwa wizi. Tangua hapo amekuwa mpole, sasa nabadilisha style ya kuishi naye lengo tuendelee kuishi ppamoja, haina maana kuvunja ndoa,ni kuvumiliana humohumo tu jaman
 
Wanawake wengi (hasa WACHAGA) ni wazuri kung'ang'ania NDOA lakin ukishamuoa ni JEURI, KIBURI na DHARAU, wewe mwenyewe mwanaume utatafuta Mchepuko bila kuambiwa. Wanawake wa KICHAGA badilikeni

Hakuna kitu kizuri kama familia na jamii. Kuna mafundisho jamii wanayotoa bila maneno jinsi wake wanavyoishi na waume zao, jamii za kichaga nyingi hazifundishi mabinti zao kunyeyekea na kuishi na waume zao kwa heshima, kwanza hizo jamii zenyewe zimejaa mfumo wa haki sawa ingawa hausemwi yaani hakuna mwanamke kujishusha,

binti akikua katika mazingira hayo ni ngumu kubadilika. Ila sasa mjini kuna makitchen party labda yatasaidia. Na exposure zitasaidia. Ni ngumu sana kwa mchaga kwa mchaga kuachana ila wengi wanasurvive kwa mume kuamua kuwa juu na msimamo kuliko mke au mume kuamua kuwa mpole na kupotezea.
Ni mimi MCHAGA
 
Back
Top Bottom