Mke wangu ananikera anataka attention yangu kila saa

Kazi za kufanya nizitoe wapi zaidi ya kupika na kupakua ana dip ila hataki kwaajiriwa anasema ameridhika kuka home
Uzi wako umenichekesha mwanzo mwisho, hebu kaa tuliza akili uzungumze na mkeo, kuna leo na kesho, ni vizuri akajishughulisha kidogo ili hata upande wako mambo yanapokua mabaya familia isiyumbe,akiwa ba kitu cha kumweka bize hata hizo simu za mara kwa mara hutazisikia.
 
Hivi na nyie wake zenu wanapenda attention kama huyu wa kwangu, ana nikera sanaa, sijui nifanye je nime dumu nae takribani miaka 11, huu ni wa 12 lakini bado iko vile vile nilidhani ataacha akikua ila duh iko vile vile, kwa siku anaweza akakupigia simu mara kumi usipo pokea ataendelea kubipu paka utakavo mpigia, na ukimpigia na kumuuliza kuna jimpya anasema hamna na kusalimia tu, weekend hamna ku concentrate au ku-compose ili upange mishe zako za j3.

Sio kwamba anapenda yale mambo mengine mnayo fikiria hayo anashibishwa kweli kweli ila bado anataka awe karibu nami kila moment, au kila wakati, kupumzika huwezi ikienda chumbani huyu hapo ukija sebuleni anakulalia arafu ni bonge ukimwambia unaniumiza anasema kumbe unipendi na wewe sio ramantic duh, akikutumia sms atatuma taarifa nusu paka umtumie sms zingine zaidi ya mbili kupata taarifa kamiri.......na kumuacha siwezi hiyo sio sabb ya kuacha mke wa watt wako, ila ni kero kweli kweli.
Mkuu kama hutajali niunganishie kwa watoto wake ili nioe nimeipenda hiyo mbengu
 
Umepata mke mwema sana. Piga magoti hapo ulipo na umshukuru Mungu. Ukisikia wenzio mambo wanayopambana nayo huko kwenye ndoa nadhani ungewaomba mods tu waufute uzi huu.

Kimsingi wanawake wote wanapenda attention sema tu wengi wamejikatia tamaa kwa sababu ya waume zao kutojali. Na wanawake wengi walio katika ndoa wanachapwa nje sana siyo kwa ajili ya pesa bali kwa kupewa attention tu, kusikilizwa, kujaliwa na kuheshimiwa.

Narudia tena: wewe umepata mke mwema na anayekujali na kukupenda. Mhakikishie tu kuwa unampenda sana na kwamba upo kwa ajili yake mpaka kifo. Vizawadi vidogo vidogo na ukipata mwanya huko kazini mpigie...hata kama ni kusema tu "Niko mkutanoni lakini nilitaka tu kukukumbusha kuwa nakupenda sana mke wangu" na kukata simu inatosha. Na siku hiyo kama una kahela mkononi mchukulie kakitafunwa kake akapendako...hata kama ni kipande cha nanasi au chips (ili azidi kuwa bonge zaidi ). Ndoa zinahitaji kazi na una bahati huyo wa kwako angalau unajua anachohitaji ili kuwa na furaha. Wengine (hasa vimbaumbau) ni minuno tu na ghubu kwa kwenda mbele hata tatizo hulijui.

Akiona kuwa unamjali sana; na akawa na uhakika kuwa penzi lako kwake halijapungua; na kwamba huna wengine huko nje hata ukimwambia kuwa waifu leo naomba privacy kidogo nifanye hiki...na kibusu kidogo ukampa au ukamparaza kikofi chokonozi cha takoni - atakuelewa tu...na ukipata mwanya na wakati sahihi unaweza kuongea naye tu kwa ustaarabu kuhusu nawe kuwa na privacy yako sometimes. Atakuelewa...labda awe na matatizo mengine ya kisaikolojia.

Take care of that marriage my man. That's your duty na ukishindwa mabaharia watakusaidia...na wanajua kutoa attention na ku-care hao usiombe....Usiwape hiyo nafasi maadam unajua weakness ya mkeo!
Wow
You are the best ná umesema kitu cha muhimu sanaaaa
 
Hivi na nyie wake zenu wanapenda attention kama huyu wa kwangu, ana nikera sanaa, sijui nifanye je nime dumu nae takribani miaka 11, huu ni wa 12 lakini bado iko vile vile nilidhani ataacha akikua ila duh iko vile vile, kwa siku anaweza akakupigia simu mara kumi usipo pokea ataendelea kubipu paka utakavo mpigia, na ukimpigia na kumuuliza kuna jimpya anasema hamna na kusalimia tu, weekend hamna ku concentrate au ku-compose ili upange mishe zako za j3.

Sio kwamba anapenda yale mambo mengine mnayo fikiria hayo anashibishwa kweli kweli ila bado anataka awe karibu nami kila moment, au kila wakati, kupumzika huwezi ikienda chumbani huyu hapo ukija sebuleni anakulalia arafu ni bonge ukimwambia unaniumiza anasema kumbe unipendi na wewe sio ramantic duh, akikutumia sms atatuma taarifa nusu paka umtumie sms zingine zaidi ya mbili kupata taarifa kamiri.......na kumuacha siwezi hiyo sio sabb ya kuacha mke wa watt wako, ila ni kero kweli kweli.
Umempata mke bora.Enjoy maisha Mkuu!😝😝😝😝😝😝
 
Ukikuta wewe ni introvert halafu uwe na mwanamke anataka attention yako kila saa utafikiri umembeba mgongoni unapata tabu sana.
Sasa introvert wenzenu huwa hamuwaoni? Humo ndani muwe kama mpo msibani.
 
Pole sana mkuu, kweli hii hua inakera sana, japo mimi sio ndoa ila ni mahusiano, mtoto wa kike alinipenda yani kila muda anataka time yangu, akimaliza kukupigia ataanza kuku chatisha, akimaliza hapo atakuja whatsapp hapa ndo usiombe akukute online,, ukimwambia sasa hivi nipo bize basi ananuna eti humpendi.

Unakuta kuna muda lazima u spend time alone, ndugu, marafiki n.k lakini yeye hajui hilo mfano nikiwa na wadau tuna watch ball unashangaa huyo kakutafuta ukimwambia naangalia mpira ananuna anakwambia kwa hiyo mimi na mpira nani wa muhimu?, ukimwambia nipo na jamaa zangu tuna discuss mambo yetu utasikia kwa hiyo mimi na hao jamaa zako nani wa muhimu.

May it's love but she complicate things.
 
Umepata mke mwema sana. Piga magoti hapo ulipo na umshukuru Mungu. Ukisikia wenzio mambo wanayopambana nayo huko kwenye ndoa nadhani ungewaomba mods tu waufute uzi huu.

Kimsingi wanawake wote wanapenda attention sema tu wengi wamejikatia tamaa kwa sababu ya waume zao
Niongezee nini kwa mfano,akishika maneno haya ataiona mbingu kupitia ndoa,"hakuna mwanamke asiyependa attention isipokuwa wengi wao washajikatia tamaa"emu screenshort huu ushauri alafu uwe unaupitia mara kwa mara na uufanyie kazi
 
Back
Top Bottom