Kweli kabisa moja ya mambo yanayoweza kusaidia kuokoa hiyo ndoa ni pamoja na mke kuwa karibu na mumewe na ikiwezekana aache kazi kabisa.Nakubaliana nawe ila inamlazimu shemeji yetu kuacha kazi huko,kwa sababu mbili kwanza kuwa karibu na mumewe ikiwezekana atafute kazi karibu ama mume amtafutie biashara yoyote afanye pili asiende kuonana na hao watu waliompelekea kusaliti ndoa yake
king'asti kama ulikuwa kichwani mwangu.Baba, pole na matatizo!
Nashindwa kuamini, ina maana huyo mchaga wa kimara baruti anaitumia na kuisasambua kiasi cha kuchoka ndani ya mwezi mmoja tu?! Ina maana wewe ulikuwaga unabofya tu?
Huo mtihani mkubwa ndugu
yangu. Hapo nakushauri umrudishe tu hapo Dar uishi naye akiendelea
kuishi peke yake huko Kibaha ataendelea kukusaliti.
Pole kwa yote yaliokukuta! ikiwa moyo wako URADHI kusamehe na KUSAHAU kuwa yaliopita sindwele, basi msamehe na usahau ingawa ni ngumu kwaninyi wanaume kusamehe, jenga familia yako kwa upendo ukiwa na mwenzi wako.
Dunia ya sasa imebadilika sana na haya mambo yapo sana kwenye ndoa nyingi, wapo wanaomba ushauri kwa kusema hadharani wapo wanaogumia moyoni kwa kuogopa kusemwa na mengine mengi.
Uamuzi mkubwa ni wako ila na kushauri umsamehe na wala usije fanya hasira ya kulipizia kwa wengine nje hapo utakuwa hujengi bali unabomoa, ni dhahiri mwanamke akikiri kosa na akiapa kutorudia huwa anamaanisha moyoni.