jamiif
JF-Expert Member
- Apr 30, 2012
- 2,413
- 990
mh, pole sana kaka kwa matatizo hayo. Mimi ninavyoona, inabidi kwanza uangalie upya namna unavyoiongoza na kucontrol nyumba yako wewe kama baba wa familia. Pili mi naona huyo dada atakuwa kapagawa na penzi la huko nje kiasi kwamba hata kama utaamua kumsamehe ukaendelea kuwa naye, hataacha tabia hiyo, na mbaya zaidi atazidi kukupa wakati mgumu pale anapokuwa anakununia kila wakati hadi uchikie nyumbayako. Sasa, nakushauri upeleke habari yote hii kwa wazazi wake na wazazi wako pia, au wale wazee wenu wa karibu ili wajue taarifa hii, ili wasije kukulaumu pale utakapoamua kuachana na huyo dada. Nasisitiza pia kuachana naye baada ya kutoa taarifa kwani atakuletea maradhi ukafa siku si zako bure...muhimu zaidi, wanajf tusimsahau huyu bwana katika dua zetu ili Mwenyezi Mungu amfanyie wepesi katika mtihani huu. Inshaallah Mungu atakuwa nawe!