Mke wangu amekutwa HIV+

Mke wangu amekutwa HIV+

Ndoa kama NDOA.

Mmmh ndoa NGUMU nyie.

Nikiwaambia msioe utasikia ""UNA MATATIZO YA SAIKOLOJIA""

Mmmh haya bana ENDELEENI TU KULA MIJEREDI.

MUNGU awaongoze...

#YNWA
 
Jamaaa inabidi amshauri mke wake arudi hosp

Yaan mpaka ngozi inaanza kua ya njano, kuna uwezekano INI lake limeanza pata shida.
Ndio inawezakana hata hiyo HIV positive hana kwa kielimu changu kidogo inaonesha Kama Mke wa jamaa ana hepatitis ndomana ya hiyo yelow ini limeanza kuleta shida
 
Cha kushangaza baada ya Kama miezi 6 msichana akaolewa na jamaa mwingine ,hiyo kidogo ilitushtua kwamba imekwaje gafla hivo ,inawezekana maruweruwe au daktari katoa vipimo feki
yeah, kuna uwezekano dokta alipangwa jamaa ateme mzigo.
 
Mimi siamini uwepo wa ukimwi kwasababu maeneo niliyopita na nikipima naambiwa sina naamini kabisa hili gonjwa ni kamchezo flani tu
Wanasema virusi vikikaa mwilini mwa mtu kwa muda mrefu chance ya kuambukiza inapungua tofauti na yule ambaye ndio kaupata. Kwa hiyo yawezekana hayo maeneo uliyopita hadi unashtuka ni kwa sababu tayari wamekaa navyo au tayari wanatumia dawa.

Mwalimu wangu aliyenifundisha semina kuhusu VVU alikuwa anasema yeye anajiamini akitembea na Malaya kuliko mtu wa kawaida. Huwa ananishangaza sana.
 
Ndio inawezakana hata hiyo HIV positive hana kwa kielimu changu kidogo inaonesha Kama Mke wa jamaa ana hepatitis ndomana ya hiyo yelow ini limeanza kuleta shida
Hepatitis vipimo vyake vinapatikana katika hospitali za zote? Kama za wilaya au rufaa au kuna hospital maalum?

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Wanasema virusi vikikaa mwilini mwa mtu kwa muda mrefu chance ya kuambukiza inapungua tofauti na yule ambaye ndio kaupata. Kwa hiyo yawezekana hayo maeneo uliyopita hadi unashtuka ni kwa sababu tayari wamekaa navyo au tayari wanatumia dawa.

Mwalimu wangu aliyenifundisha semina kuhusu VVU alikuwa anasema yeye anajiamini akitembea na Malaya kuliko mtu wa kawaida. Huwa ananishangaza sana.
Basi kama kweli ngwengwe ipo itabidi niokokee kwasababu kwa miaka 10 yangu toka 2008 mpaka 2018 haikua ya kawaida...sikuwahi kupoa kabisaaa na nimechomokaa si jambo dogo.
 
Basi kama kweli ngwengwe ipo itabidi niokokee kwasababu kwa miaka 10 yangu toka 2008 mpaka 2018 haikua ya kawaida...sikuwahi kupoa kabisaaa na nimechokaa si jambo dogo.
Okoka tu na utoe sadaka ya shukurani na uoe kabisa.
 
HIV na HB ni Co-infenction

Ndio maana mwenye HIV atapimwa HB..na mwenye HB atapimwa HIV.


Upimaji wa HIV sio km kupima Maralia, ndio maana kunafanyika upimaji wa vipimo viwili kwa pamoja au zaidi

Yaan chakwanza kinakua Sensitive sana kwenye kugundua...then chapili kinakua na specificity kubwa ya Kuthibitisha.


Kwahiyo huwa ningumu kupewa False Postive kama Jibu la mwisho.


Labda itokee uzembe wa watoa huduma kushindwa kutekeleza muongozo wa Upimaji.

Kwa mfano.....badala ya kupima na vipimo viwili...yeye akampima kwa kipimo chakwanza tu akahitimisha ....... Ndio hapo unampima mtu HIV, kumbe ana HB, kipimo kinareact , unaacha kwenda hatua ya pili. Weee unamuanzisha dawa .



Izo kesi zipo nyingi... Ndio maana HIV inathibitishwa kwa vipimo viwili mpaka vitatu.
Thanks mkuu hapa nimepata kitu hii ndo JF tunayoitaka
 
Habari za wakati huu JF?

Ndugu zangu Nina kisa cha kusikitisha ambacho ningependa kupata mawazo kutoka kwenu.

Nitajitahidi kuandika Kwa ufupi kadiri iwezekanavyo. Jitahidi tu usome upate cha kuniambia Yani.

Iko hivi, ninaishi na binti ambaye tumebahatika kupata mtoto mmoja wa mwaka na miezi miwili sasa.

Kisa chenyewe ni kwamba Tangu mwenzangu Huyu akiwa mjamzito wa miezi mitano (April/2020) sikuwahi kushiriki naye mapenzi hata romance yaani Hadi hivi leo mtoto ana mwaka mmoja na miezi miwili. Hii ilikuwa ni kumfanya apate nafasi ya kupumzika Hadi atakapojifungua, na hili tulikubaliana kabisa.

Sasa miezi kadhaa baada ya kujifungua bado akawa hataki hata nimguse yani. Alikuwa anasema ni Kwa sababu Hana hisia kabisa za mapenzi kutokana na kumbukumbu za maumivu wakati wa kujifungua. ( Ikumbukwe alijifungua kawaida kabisa uzao wake huu wa kwanza). Kutokana na Mimi kuwa mtu wa kusafiri huku na kule kutafuta riziki sikuwa na nafasi yakuweza kujua mienendo yake nikiwa mbali. (Yeye ni mwalimu wa primary school).

Hali imeendelea hivyo,, hataki kabisa hata nimguse. Ukimgusa tu ni ugomvi mkubwa. Sasa Kama mwezi mmoja umepita nilitoka kwenye mishe zangu huko kusini mwa nchi yetu,, nikiwa home jioni moja nikaona anameza dawa ambazo sikuwahi ziona kabla, nikashtuka kidogo maana alikuwa anameza Kwa kuibia hivi! Nikamuuliza vipi unaumwa? Akajibu ni kichwa ndo maana anameza paracetamol. Lakini ukweli hazikuwa paracetamol! Nikasubiri nilipopata nafasi kuziangalia zile dawa nikakuta ni " ISONIAZID" ambazo haraka niliingia mtandaoni nikagundua ni za Tuberculosis (TB).

Nilipomuuliza akasema walipita watu shuleni kwao ( yeye ni mwalimu) wanagawa eti wamepewa Kama prevention! Kama wanavyofanyaga Kwa dawa za minyoo n.k

Japo nilishashutuka,, nikaamua kukaa kimya kwanza ili nisivuruge uchunguzi wa kina. Sasa wiki iliyopita tukiwa tumelala usiku (taa zinawaka chumbani Kwa ajili ya mtoto), nilishtuka tu baada ya mtoto kuanza kulia bila Shaka ilikuwa ni njaa. Lakini mwenzangu hakushtuka labda kutokana na uchovu wa siku mzima. Hapo ndipo niliona ngozi za mapaja yake zikiwa na njano kabisa Kama ndizi mbivu!

Nikashtuka sana! Yeye aliposhtuka, baada ya muda kidogo Ile njano ikapotea akawa kawaida tu. Nikahisi labda ni Maruweruwe ya usingizi, hivyo sikumuuliza nikakausha.

Usiku uliofuata nikafanya sasa kuvizia nione Kama lilikuwa wenge au lah! Mambo yakawa vile vile! Nikasema ngoja nione tena na leo siku ya tatu,, Mambo yakawa vile vile rangi ya ngozi hasa huko mapajani ni njano kabisa na safari hii Hadi sehemu za mgongoni. Nikavunja ukimya, nikamuuliza lakini alinijibu Kwa kunibeza; "....eti haaa, mi najua umeniamsha kuna Jambo la maana kumbe ni...."

Hapo sasa akili ikanikaa nikajua rasmi anafahamu vema juu ya hilo. Asubuhi nikachelewa kutoka nyumbani lengo nifanye msako mkali labda kuna dawa Zaidi na labda anaumwa lakini anaficha..

Kwa bahati nzuri nikakutana na dawa kwenye mfuko wa kawaida tu ( zimeandikwa " LA 75". nika-googgle chap nikaambiwa ni Lamivudine! Aina mojawapo ya ARVs! Moyo ukapasuka! Nilitoka nikaenda kwanza kanisani akili itulie.

Jioni baada ya yeye kurudi nikamwita chumbani Kwa Sura ya kigaidi na mkanda mkononi,, (sikuwahi kamwe kumpiga) lakini ilibidi nivae Sura hiyo.. baada ya kumuuliza akawa mkali anabisha, nikafungua mkoba wenye hizo dawa nikamwonesha kisha nikashika vema mkanda mkononi. Kabla ya kuanza kichapo akaomba nisimpige atanieleza kila kitu. Basi Akafunguka..kwamba amegundua ameathirika huu ni mwezi wa sita sasa! Na alijua ni Mimi ndo nimemuambukiza ndiyo sababu ya kunichukia Kwa kipindi chote kile hata asitake nimguse!

Jioni hiyo hiyo nikaenda kupima,, Niko negative. Nikapita pharmacy moja hapa mjini pia nikanunua vile vipimo nikaja navyo nyumbani akanipima yeye mwenyewe maana ameshakuwa mtaalamu.. nikakuta negative pia.

Mengine yaliyoendelea siyo muhimu ,,lakini anasema hajawahi kuchepuka Kwa kipindi chote hicho. Sasa nikabaki na maswali inawezekana vipi mtu apimwe mara tatu wakati wa ujauzito awe negative, hajachepuka halafu miezi kadhaa baada ya kujifungu awe positive? Na Mimi mwenyewe sina maambukizi?!!

Hebu tieni neno wakuu. Nahisi kuvurugwa kabisa yaani. Kuhusu mtoto wanadai hawezi kupimwa Hadi afikishe miezi 18. Lakini Kwa mwonekani dogo yupo na afya njema.

Mnadhani possibility ya kuambukizwa ipo wapi Kama hakuchepuka?

Dah! Mungu nisaidie.
View attachment 1964380
Mkuu, check message box yako
 
Pole sana mkuu! Issue ya namna hiyo ilitokea hata kwa jamaa yetu wa hapa job.
Lakin yeye alioa tu mtu ambaye alimuamini kwa macho kulingana na mwonekano wa afya na umbile lake!
Kwa vile alikuwa pisi kali , chapchap jamaa akampiga mimba , wakati mtoto kazaliwa ndipo jamaa akagundua hilo siku mkewe alipotuma aletewe mikoba akiwa kwa mama mkwe ndipo katika kusearch jamaa akaziona hizo ARAV katika moja ya mabegi.
Ndo kwenda kumchukua wife, walipopima akakutwa ni HIV+ , lakini yeye jamaa hakuwa ameathirika!
Jamaa alipotafuta taarifa zaid akagundua kuwa bidada alishaanza kumeza hivo vidonge hata kabla hawajajuana, lakini ilikuwa siri yake!
Kilichofanyika walitengana lakini walikubaliana kuendelea kulea mtoto. Hadi sasa dogo ana miaka 4.
Kwa hiyo suala lako ni kama la huyo bwana. Hivyo chakufanya mchukuwe wife wako nendeni mkapate ushauri kutoka kwa Daktari, ili kama atashauri mtengane nae basi demu asione kama ni maamuzi yako binafsi bali ni kutekeleza ushauri wa kitaalam!
Mtoto kama Mungu kamjalia afya njema, anatakiwa anyonye ziwa la mama kwa kipindi cha miezi 6 tu, kisha mnamuachisha. Hicho ni kipindi ambacho maumbile ya mdomoni mwake huwa ni laini, yaani anakuwa hajaota meno!
Meno ya mtoto ndio husababisha vidonda kwenye nyonyo za matiti ya mama na hivyo kumuweka mtoto katika hatari ya kuambua ugonjwa!
 
Naomba kufahamu iyo yellowish inayotokea mapajan pindi anelala alaf akiamka inapotea, inakuwa ni nin wajuzi
 
Kwanza nikupe pole kwa maswaibu yaliyokukuta lakini pia nikupe big up kwa kuupata uhakika kuwa mwenza wako ni muathirika wa HIV na bado ukawa na ujasiri wa kuvumilia na kukabili changamoto kwanza kwa kwenda kanisani lakini pia kuja hapa JF kuomba ushauri hakika hiyo ndi sifa ya mwanaume KUKABILI CHANGAMOTO ZINAZOKUJA NA KUTOTETELEKA.Najua hivi sasa una mawazo mengi na ndio maana umekuja kupumua hapa JF na wengi wamekupa pole,kuuliza maswali kukushauri ama kwa uzoefu wao ama kitaalamu lakini wengine wamepondea au kukudharau kwa kadri ya kila mmoja alivyolipokea mimi upande wangu nataka nikushauri yafuatayo.

  • Maisha lazima yaendelee huwezi kuyabadilisha yaliyokwisha tokea songa mbele achana kabisa na kutaka kujua ukweli wa mwenza wako alipataje,na nani, lini ukiyajua yatakuumiza moyo na utakuwa mwanzo wa kupata stress ,mfadahaiko na magonjwa mbalimbali mfano shinikizo la moyo n,k.Wanawake ndivyo walivyo kukuambia ukweli ni 1 kwa kumi.
  • Wasiliana na wataalamu wa Hospitali kujua hali ya mtoto kama ameambukizwa au hapana kwa sababu nijuavyo mimi mama anapoanza clinic kipindi anapokwa mjamzito anapimwa afya na mojawapo ni kujua kama ana maambukizi basi wakati wa kujifungua kuna namna huyu mjamzito ataambiwa ili kumkinga mtoto asipate maambukizi kutoka kwa mama siku hizi kuna njia nyingi
  • Mnapofunga ndoa mlikula kiapo Kanisani kuwa mtakuwa pamoja katika shdia na raha,afya na ugonjwa ndiyo hapa sasa unatkaiwa kudhihilsha hicho kiapo.Tena Biblia inasema mke atamtii mume bali mume atampeda na kumlinda mke wake.Mshukuru Mungu umzima ni wakati wa ku kaa na mwenza kwa hekima na busara japoa haitakuwa rahisi atakuwa defensive ,mkali ili kuficha uongo wake ila muda ni mwalimu mzuri mtakuja pata suluhisho zuri baadaye hata miaka 2,3,5 ijayo
  • Utapata ushauri mbali mbali kutoka kwa ndugu, jamaa na marafiki na hapa JF ila sikiliza sauti yako ya ndani kutoka kwa Mungu sisi ni wasaauri tu lakini joto la jiwe anayelijua ni mjusi(wewe).
  • Wewe si kwanza kupata tatizo kama hili na sio wa mwisho ..wengi wanaugua na wamekubali hali hiyo maisha yanaendelea hivyo jpe moyo,,sasa ni wakati wa kupambana maradufu kutafuta maisha na wewe kujitunza.
 
Back
Top Bottom