stubborn wa Njombe
Member
- Dec 8, 2016
- 79
- 170
- Thread starter
- #81
Nimekuelewa mkuu. Ila huyu mama ni mzoefu hilo eneo na kuna vitu vingi sana nimegundua yeye anamuelekeza wife avifanye kwa Siri bila kunishirikisha.Mimi nikushauri tu; achana na huyu third party. Atapata sababu ya kusambaza mambo yako na mkeo eneo lote hilo, mkeo ataona biashara chungu. Anaweza kwenda hapo dukani akaanza kumbwatukia "kwahiyo umemwambia mumeo mimi ndo nakutaftia mabwana? Si ni umalaya wako" Tayari umefanya jambo dogo kuwa kubwa.
Zungumza na Mkeo kwa uwazi kabisa kuwa kuna vitu kama mume hutovumilia na vitapelekea kuvunja agano lenu. Kama huyo mama ndo kishawishi (i doubt this sana, nahisi huyu mama anatumika tu kama njia na mkeo) basi mwambie Mkeo akae naye mbali. Yeye atajua afanye nini. Hakuna mwenye jukumu la kulinda ndoa yenu zaidi ya nyie wawili.
All in all I pray mrudi katika hali ya awali.
Hivyo nahisi naye ni kirusi hatari sana Kwenye ndoa yangu.
Lakini nimeshamuweka sawa na nimeshavunja ukaribu kwa maana nimewaita yule mwanamke na mume wake na mke wangu pia nikaweka chini nikaomba kiustaarabu tu sitaki ukaribu au urafiki wao uendelee.
Hivyo bado ninachunguza lakini nasubiri kodi iishe nihamishe biashara pale.
Ahsante kwa ushauri mkuu.