Kuna demu mke wa rafiki yangu ameomba niongee na mume wake kwani hawana maelewano ndani ya nyumba. Kisa jamaa alisikia mke wake alikuwa anaandikiana sms za mapenzi na mtu mwingine na walishaenda gesti pamoja.Alivyomuuliza mkewe, mke anadai zile sms ni utani tu na kule gesti ni kweli waliingia lakini hawakufanya chochote kwani alimkatalia kufanya mapenzi. Jamaa hajasema msimamo wake lakini mke anaogopa maana hata mahusiano sio mazuri. Namshaurije mume mtu? Na atamuaminije huyo mke wake kama kweli hawakufanya chochote kule gesti?