Mke anataka waachane, mume hataki bado anampenda

Marco Polo

JF-Expert Member
Jan 16, 2014
8,988
12,442
Kuna jamaa tunafanya nae kazi nje ya mkoa wa Dar ameoa (ndoa ya kikristo) na ana watoto wa 3 mke ni mfanyakazi katika taasisi moja ya kibenki. Huyu mke jamaa ndio kamsomesha kuanzia degree mpaka post graduate.

Wamekuwa na ugomvi na mke wake siku nyingi tu ila kama miezi 5 iliyopita ugomvi wao umepitiliza, mke akawa anahitaji talaka na jamaa hataki kumpa mkewe talaka akidai kwamba bado anampenda.

Kabla hawajagombana jamaa alikuwaga na kawaida ya kwenda Dar kusalimia familia yake basi ikawa kila jamaa akija home kwake mwanamke anaondoka halali home na mshikaji akiondoka kurudi kazini mwanamke anarudi kiufupi mwanamke hataki kukaa pamoja na mumewe.

Bas visa vimeendelea mara achelewe kurudi Mara asije kabisa nyumbani yaani ili mradi ni shida tu. Mume alipoamua kumfuatilia mke wake akagundua anatoka na mwanajeshi. Jamaa kwa sasa ameamua kutoenda Dar mwezi wa pili huu wakati mwanzoni ilikuwa kila week yupo Dar home kwake kisa tu anahofia kuuawa kwa juju na mke wake.

Jamaa kwa sasa huku alipo anatangatanga kwa waganga tu ambao mimi naona wammalizia pesa na huko Dar, mwanamke naye anashirikiana na mama yake nao wanamuwinda jamaa kwa juju wammalize (maneno ya mume). Mpaka sasa hivi kuna mashindano ya nguvu ya giza kati ya mwanamke akishirikiana na mama yake dhidi ya jamaa.

Mimi nilimshauri jamaa amwache tu huyo mkewe ila ndio hivyo jamaa bado anashikilia akiamini waganga wanaweza okoa ndoa yake.

Sijui ungekuwa wewe ungemshauri vipi huyu jamaa maana nikimwangaliaga anatia huruma kwakweli na mwili wote umeisha maskini.
 
Nguzu za giza hazizimwi/kumalizwa kwa nguvu za giza. Zaidi anaenda tu kujiongezea maagano hapo ambayo baadaye yatamsumbua tu. And asije akapoteza tu maisha yake kisa ndoa, watoto wakamkosa baba yao na akawaachia uchungu wazazi wake bure. Mtu hakutaki, unataka hadi utolewe roho khaa
 
Kama mkewe anatumia "dawa" Basi dawa za mke zipo juu. Vingenevyo angekuwa ametoa TALAKA.

SISI WAAFRIKA tuna mila zetu, hata tukuzikana na kuzipuuza haziwezi kutoweka.
 
mberf zake si limwanamkevaliache tu aendelee na maisha yake? yaan anapoteza hela kisa hilo limalaya? kasharogwa huyo, mwambie apige kimya aanze maombi aavhane na huyo make, atakufa kwa ukimwi,
Bora ukimwi mkuu....ninachokiona hapa kuna hatar jamaa hata akawa kichaa kama sio kuwekewa sumu kwenye chakula
 
Kuna jamaa tunafanya nae kazi nje ya mkoa wa Dar Ameoa (ndoa ya kikristo) NA ana watoto wa3 mke ni mfanya kazi ktk taasis moja ya kibenki ..Huyu mke jamaa ndio kamsomesha kuanzia degree mpaka post grad

Wamekuwa NA ugomvi NA mke wake siku nyingi tu ila kama miezi 5 iliyopita ugomvi wao umepitiliza mke akawa anahitaji taraka NA jamaa hatak kumpa dem taraka akidai kwamba bado anampenda....,

Kabla hawajagombana jamaa alikuwaga NA kawaida ya kwenda Dar kusalimia familia yake bas ikawa kila jamaa akija home kwake Demu anaondoka halali home NA mshikaji akiondoka kurud kazin demu anarud kiufupi demu hataki kukaa pamoja NA mumewe,bas visa vimeendelea mara achelewe kurudi Mara asije kabisa nyumban yaan ili mrad ni shida tu....Mume alipoamua kumfuatilia mke wake akagundua anatoka NA mwanajeshi ....Jamaa kwa sasa ameamua kutoenda Dar mwezi wa pili huu wakat mwanzon ilikuwa kila week yupo Dar home kwake kisa tu anahofia kuuwawana kwa juju na mke wake ....

Jamaa kwa sasa huku alipo anatanga tanga kwa waganga tu ambao mm naona wammalizia pesa NA huko Dar demu naye akishirikiana NA mama yake nao wanamuwinda jamaa kwa juju wammalize(maneno ya mume)...Mpaka sasa hiv kuna mashindano ya nguvu ya Giza kati ya demu akishirikiana NA mama yake dhidi ya jamaa....

Mm nilimshaur jamaa amwache tu huyo demu ila ndio hivyo jamaa bado anashikilia akiamin waganga wanaweza okoa ndoa yake....

Sijui ungekuwa ww ungemshaur vp huyu jamaa maana nikimwangaliaga anatia huruma kwakwel NA mwili wote umeisha maskini
Ada za vyuo zina muuma kuliko mapenz someshen sana
 
Mbona kuna wengi tu wamesomesha na mwisho wa siku demu anaolewa na kidume mwingine!? Mwambie ampige chini fasta maana wazuri hawajazaliwa bado!
 
Hivi wakati huu bado kuna watu wanawategemea waganga jamani....Anyway,Mshauri kwa utulivu akawaone viongozi wa dini...na asiache kuwashirikisha wazazi wake pia. Atajikuta anakosa vyote...ajifunze ku-let go.

Huyo mwanamke pengine alikubali aolewe nae kulipa fadhila tu za kusomeshwa, but hakuwa na hisia nae tangia mwanzo.Pole sana kwake
 
Back
Top Bottom