Interest
JF-Expert Member
- Apr 11, 2015
- 3,434
- 7,055
Bado napambania maslahi ya Mama Tanzania!
Wizara ya Mambo ya Nje ilikuja na taarifa kuhusu Tanzania kutambua ushoga. Yaani, inaheshimu mikataba ya Umoja wa Mataifa ambayo inataka Haki za Binadamu zitambuliwe na kutekelezwa. Taarifa hiyo iliambatana na kusema haiitambui operesheni ya Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda dhidi ya mashoga. Kwamba ni mawazo yake binafsi na sio msimamo wa Serikali!
Nimejipa muda kufuatilia. Sijaona mkataba wowote wa UN/Kimataifa unaotambua Ushoga kuwa ni sehemu ya Haki za Binadamu. Sasa huku kuufyata kuhusu ushoga kunatoka wapi?
Badala yake, nimeona Mikataba 2 ambayo inazungumza tofauti na hivyo.
1. Mkataba wa Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni (the International Covenant on Economic, Social and Cultural Rights):
Kifungu cha kwanza cha makataba huu kinatambua haki ya kila jamii kujiamulia yenyewe bila kuingiliwa mambo yao ya kiuchumi, kijamii na kiutamaduni (Article 1: All peoples have the right of self-determination. By virtue of that right they freely determine their political status and freely pursue their economic, social and cultural development.). Ndivyo mkataba huu unavyosema. Sio maneno yangu!
Sasa iweje leo nchi yetu ilazimishwe kufuata mifumo ya uchumi ya wengine? Iweje leo tulazimishwe tuishi kwa mila za wengine? Kwanini leo tulazimishwe tuige utamaduni wa wengine? Kwanini huu mkataba hauheshimiwi?
Kwa kuzingatia mkataba huu tunayo kila sababu kama wanachama wa UN kukataa mashinikizo yote yanayoingilia uhuru wetu wa kujiamulia tuishije kiuchumi, kijamii na kiutamaduni. Wale wenye dhamana wawakumbushe hawa jamaa kuwa kuna mkataba wa UN unatupa haki yetu ya kuamua tuishije kiuchumi, kijamii na kiutamaduni. Ni mpaka hapo mkataba huu utakapofutwa ndio watakuwa na uwezo huo.
2. Mkataba wa haki za kiraia na kisiasa (the International Covenant on Civil and Political Rights).
Mkataba huu umetoa haki kwa mtu au binadamu mmoja mmoja. Hakuna kipengele hata kimoja kimempa mtu au binadamu uhuru wa kuingiliana kinyume na maumbile. Kama kipo naomba nionyeshwe. Hakipo! Na hakipo kwa kuwa mwaka 1966 mkataba huu uliporidhiwa watu hawakuitambui hii kama haki ya kijamii na ya kisiasa ya binadamu! Hata kwenye kifungu 23 haki hii haikutambuliwa.
Mkataba huu bado uko hai. Haukutambua ushoga, usagaji, kujibadili viungo kama moja ya haki za kiraia na kisiasa za mwanadamu. Mkataba huu umetambua ndoa ya watu wanaoweza kupata watoto. Mkataba huu umetambua familia kama muungano wa mwanamke na mwanaume wanaoweza kuzaa. Na hakuna mkataba wowote wa umoja wa mataifa ulioridhiwa ambao umehalalisha ushoga na hayo mengine. Hawa wanaodai ushoga, usagaji na uchafu mwingine ni haki ya binadamu wanatoa hoja yao kwenye mkataba upi wa UN?
Nijuavyo mimi, baadhi ya nchi zimehalalisha mambo hayo kwenye sheria za nchi zao. Tunalazimikaje kufuata maagizo yatokanayo na sheria ya nchi nyingine? Ni vyema wenye dhamana wawakumbushe kuhusu uhai wa huu mkataba. Wakitaka waufute kwanza. La sivyo wanakiuka mkataba wa UN kutulazimisha mambo ambayo hayapo kwenye huu mkataba!
Nimalizie kwa kuwahimiza vijana na wanadiplomasia wetu wajenge utamaduni wa kusoma kwa umakini mikataba ya UN ambayo ndiyo kila mara wapiga debe wanaitumia kutaka tufuate uovu.
Hakuna mkataba wa UN umehalalisha ushoga, usagaji na hayo mengine, yaani LGBT kwa ujumla.
NB: Bernard Membe alipokuwa Waziri wa Mambo ya Nje, aliwahi kusema walivyoenda kwenye Mikutano ya Umoja wa Mataifa, walijadiliana kuhusu Haki za Binadamu na kukubaliana mambo kadhaa. Suala la Ushoga halikuwepo kwenye ajenda na hata viongozi wa mataifa flani walipojaribu kuwashawishi (pembeni) wakubali kuitambua LGBT, waligoma.
Yaani nimeshangaa sana leo hii Serikali ya Tanzania kuingia kingi kizembe kwenye mtego huu!
======
UPDATE:
Hiki ndicho tulichokubali kutoka UN
Wizara ya Mambo ya Nje ilikuja na taarifa kuhusu Tanzania kutambua ushoga. Yaani, inaheshimu mikataba ya Umoja wa Mataifa ambayo inataka Haki za Binadamu zitambuliwe na kutekelezwa. Taarifa hiyo iliambatana na kusema haiitambui operesheni ya Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda dhidi ya mashoga. Kwamba ni mawazo yake binafsi na sio msimamo wa Serikali!
Nimejipa muda kufuatilia. Sijaona mkataba wowote wa UN/Kimataifa unaotambua Ushoga kuwa ni sehemu ya Haki za Binadamu. Sasa huku kuufyata kuhusu ushoga kunatoka wapi?
Badala yake, nimeona Mikataba 2 ambayo inazungumza tofauti na hivyo.
1. Mkataba wa Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni (the International Covenant on Economic, Social and Cultural Rights):
Kifungu cha kwanza cha makataba huu kinatambua haki ya kila jamii kujiamulia yenyewe bila kuingiliwa mambo yao ya kiuchumi, kijamii na kiutamaduni (Article 1: All peoples have the right of self-determination. By virtue of that right they freely determine their political status and freely pursue their economic, social and cultural development.). Ndivyo mkataba huu unavyosema. Sio maneno yangu!
Sasa iweje leo nchi yetu ilazimishwe kufuata mifumo ya uchumi ya wengine? Iweje leo tulazimishwe tuishi kwa mila za wengine? Kwanini leo tulazimishwe tuige utamaduni wa wengine? Kwanini huu mkataba hauheshimiwi?
Kwa kuzingatia mkataba huu tunayo kila sababu kama wanachama wa UN kukataa mashinikizo yote yanayoingilia uhuru wetu wa kujiamulia tuishije kiuchumi, kijamii na kiutamaduni. Wale wenye dhamana wawakumbushe hawa jamaa kuwa kuna mkataba wa UN unatupa haki yetu ya kuamua tuishije kiuchumi, kijamii na kiutamaduni. Ni mpaka hapo mkataba huu utakapofutwa ndio watakuwa na uwezo huo.
2. Mkataba wa haki za kiraia na kisiasa (the International Covenant on Civil and Political Rights).
Mkataba huu umetoa haki kwa mtu au binadamu mmoja mmoja. Hakuna kipengele hata kimoja kimempa mtu au binadamu uhuru wa kuingiliana kinyume na maumbile. Kama kipo naomba nionyeshwe. Hakipo! Na hakipo kwa kuwa mwaka 1966 mkataba huu uliporidhiwa watu hawakuitambui hii kama haki ya kijamii na ya kisiasa ya binadamu! Hata kwenye kifungu 23 haki hii haikutambuliwa.
Mkataba huu bado uko hai. Haukutambua ushoga, usagaji, kujibadili viungo kama moja ya haki za kiraia na kisiasa za mwanadamu. Mkataba huu umetambua ndoa ya watu wanaoweza kupata watoto. Mkataba huu umetambua familia kama muungano wa mwanamke na mwanaume wanaoweza kuzaa. Na hakuna mkataba wowote wa umoja wa mataifa ulioridhiwa ambao umehalalisha ushoga na hayo mengine. Hawa wanaodai ushoga, usagaji na uchafu mwingine ni haki ya binadamu wanatoa hoja yao kwenye mkataba upi wa UN?
Nijuavyo mimi, baadhi ya nchi zimehalalisha mambo hayo kwenye sheria za nchi zao. Tunalazimikaje kufuata maagizo yatokanayo na sheria ya nchi nyingine? Ni vyema wenye dhamana wawakumbushe kuhusu uhai wa huu mkataba. Wakitaka waufute kwanza. La sivyo wanakiuka mkataba wa UN kutulazimisha mambo ambayo hayapo kwenye huu mkataba!
Nimalizie kwa kuwahimiza vijana na wanadiplomasia wetu wajenge utamaduni wa kusoma kwa umakini mikataba ya UN ambayo ndiyo kila mara wapiga debe wanaitumia kutaka tufuate uovu.
Hakuna mkataba wa UN umehalalisha ushoga, usagaji na hayo mengine, yaani LGBT kwa ujumla.
NB: Bernard Membe alipokuwa Waziri wa Mambo ya Nje, aliwahi kusema walivyoenda kwenye Mikutano ya Umoja wa Mataifa, walijadiliana kuhusu Haki za Binadamu na kukubaliana mambo kadhaa. Suala la Ushoga halikuwepo kwenye ajenda na hata viongozi wa mataifa flani walipojaribu kuwashawishi (pembeni) wakubali kuitambua LGBT, waligoma.
Yaani nimeshangaa sana leo hii Serikali ya Tanzania kuingia kingi kizembe kwenye mtego huu!
======
UPDATE:
Hiki ndicho tulichokubali kutoka UN