Mkataba wa TRL hauvunjwi ng'o!

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Mkataba wa TRL hauvunjwi ng'o !

17 September 2009
Majira

kawambwa1.jpg


Waziri wa Miundombinu Dkt. Shukuru Kawambwa akisisitiza jambo mbele ya waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kuhusu azma ya Serikali kuboresha vipengere vya mkataba wa Kampuni ya RITES na Serikali ili kuepuka kuuvunja mkataba huo. (Picha na Charles Lucas)

*Waziri asema lengo ni kulinda mazingira ya uwekezaji
*Adai serikali inahofia fidia kubwa inayoweza kutozwa
*Pia inaogopa kuchafuliwa na mwekezaji nje ya nchi
*Hata hivyo akiri upungufu mkubwa wa mwekezaji


Imeandikwa na Benjamin Masese na Gladness Theonest

SERIKALI imesema kamwe haiwezi kuvunja mkataba wake na Kampuni ya Reli Tanzania (TRL) ili kulinda mazingira ya uwekezaji nchini na kuhofia gharama kubwa inazoweza kutozwa endapo itachukua uamuzi huo.

Hatua hiyo imekuja siku chache baada ya Chama Cha Wafanyakazi wa Kampuni ya Reli Tanzania (TRAWU) na wadau wengine kutaka mkataba TRL uvunjwe kutokana na kusuasua kwa mwekezaji kampuni ya RITES kutoka India kuendesha reli hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Waziri wa Miundombinu, Dkt. Shukuru Kawambwa alisema kuvunjwa mkataba huo kunaweza kusababisha mwekezaji atakayefukuzwa, kuitangaza Tanzania vibaya nje ya nchi.

"Kuvunjwa mkataba wa TRL kutasababisha Watanzania kuingia gharama kubwa kulipa fidia wawekezaji hao. Serikali haiwezi kuvunja mkataba kirahisi kama wengi wanavyofikiria kwa sababu mkataba huu ni wa kimataifa unaohusisha nchi tatu, ambazo ni Tanzania, India na Msumbiji, hivyo badala yake ina uharaka wa kutenga fedha nyingi za kuboresha reli, hata kama mwekezaji ataendelea kuwepo.

"Umoja wa Mataifa una orodha ya nchi zinazovunja mikataba iliyosainiwa kihalali, tukivunja huu tutashtakiwa baadaye. Kama itahitajika kuuvunja, utakuwepo utaratibu maalum wenye maridhiano baina ya pande zote mbili. Huu ni mkataba wa kimataifa hautavunjwa kamwe!" Alisema Dkt. Kawambwa.

Huku waandishi wa habari wakionekana kuwa na hamasa kuuliza maswali juu ya kile kinachoonekana kuwa utendaji mbovu wa TRL, Waziri Kawambwa, alikiri kudorora huduma za reli hiyo tangu TRL ilipokabidhiwa jukumu hilo.

Alitaja kasoro zinazosababisha kudorora huduma hizo kuwa ni pamoja na matatizo ya kiuendeshaji na uwezo mdogo alinao mwekezaji huyo.

Pia alikiri kuwepo upungufu ya mtaji katika utekelezaji wa mkataba wa ukodishaji ambapo alisema hali hiyo imesababisha uhaba wa pesa ambazo zingetumika kufanyia matengenezo njia ya reli na kukarabati vyombo vya uendeshaji.

Akizungumzia uhalali wa ukodishwaji wa lililokuwa Shirika la Reli ya Tanzania (TRC), uliozaa wa sasa wa TRL, alisema Waraka wa Baraza la Mawaziri Na. 29/2006 uliruhusu utumike utaratibu wa ubia katika kuendesha na kugharamia TRL, kati ya Serikali ya Tanzania na kampuni ya RITES kutoka India.

Dkt. Kawambwa alikiri kuwa mkataba huo una matatizo ambayo ni; TRL kutozingatia mkataba wa ukodishaji, uongozi wa TRL kutotekeleza makubaliano ya nyongeza ya mshahara wa kima cha chini kati yake na TRAWU.

Kuhusu uhalali wa RITES kuidai TRL injini na mabehewa na kuamua kusitisha matumizi ya vifaa hivyo, mpaka itakapolipwa dola za Marekani milioni 13.42, Dkt. Kawambwa alisema serikali haina habari na deni hilo kwani mkataba huo ni kati ya TRL na RITES.

Alisema serikali itaendelea kuikopesha TRL vipuli na vitendea kazi vingine. Alitoa rai kwa wafanyakazi na kuendelea kuchapa kazi kwa mujibu wa kanuni za ajira na kuacha kuingilia majukumu ya serikali ambayo ndiyo ilisaini mkataba.

"Nchi ni yetu sote lazima tufuate kanuni na utaratibu wa utawala bora, hivyo wasifanye maamuzi yoyote ya kuiondoa manejimenti ya TRL, wafanye kazi walizopangiwa.


"Wananchi wawe wavumilivu kwa kuwa hali ya sasa ya TRL ni ya mpito ambayo itarekebishwa na kupatiwa ufumbuzi wa kudumu," alisema Bw. Kawambwa.
 
Huu ni usanii wa hali ya juu na udhaifu mkubwa wa kiutendaji. Mbona Lowassa alivunja mkataba na wale wasanii wa Dar City waliowekeza kwenye huduma za maji na walifungua mashtaka UK kutaka kulipwa fidia kwa kuvunja mkataba na Tanzania ilishinda kesi ile!? Kwanini leo Serikali iogope kuvunja huu mkataba na hawa matapele wa RITES ambao kuna ushahidi wa kutosha kwamba kazi ya kuendesha TRL imewashinda kabisa? Hii Serikali inasikitisha na kuudhi mno!
 
Hapa kuna namna ya docs ya kuunganisha ili kupata picha halisi,. inahuzunisha kuwa TRL matatizo, ATC matatizo, TTCL Matatizo, sasa hivi sisi Watanzania tuna Nini??
 
Huu ni usanii wa hali ya juu na udhaifu mkubwa wa kiutendaji. Mbona Lowassa alivunja mkataba na wale wasanii wa Dar City waliowekeza kwenye huduma za maji na walifungua mashtaka UK kutaka kulipwa fidia kwa kuvunja mkataba na Tanzania ilishinda kesi ile!? Kwanini leo Serikali iogope kuvunja huu mkataba na hawa matapele wa RITES ambao kuna ushahidi wa kutosha kwamba kazi ya kuendesha TRL imewashinda kabisa? Hii Serikali inasikitisha na kuudhi mno!
Bubu,
Tatizo ni kwamba hatuna tena viongozi wanaothubutu. They have no guts!
 
Huu ni usanii wa hali ya juu na udhaifu mkubwa wa kiutendaji. Mbona Lowassa alivunja mkataba na wale wasanii wa Dar City waliowekeza kwenye huduma za maji na walifungua mashtaka UK kutaka kulipwa fidia kwa kuvunja mkataba na Tanzania ilishinda kesi ile!? Kwanini leo Serikali iogope kuvunja huu mkataba na hawa matapele wa RITES ambao kuna ushahidi wa kutosha kwamba kazi ya kuendesha TRL imewashinda kabisa? Hii Serikali inasikitisha na kuudhi mno!

trust me, huu mkataba....from day one ulikuwa "FYONGO" kwa upande wetu.......
........when it come to serious issues to takle na NIA IKO......Lowassa is very good at that..........
 
Haya madhara ya % yanatupeleka kuwa watumwa wa nchi yetu huku tukitambua.
Huyu jamaa nilimsikia jana akiongea dah nilitamani kummeza sijui tunaelekea wapi bora arudi mkoloni mweupe ieleweke kuliko kuwa na mkoloni mweusi.
Walisha ambiwa jamaa mchovu lakini wao wamemkumbatia dah au mnataka Reli ya kati ife alafu mataruma yale mgeuze scraper?
 
Mnakumbuka walisema watareta vichwa vya treni vitakuwa vinakimbia kama Bajaj.
 
trust me, huu mkataba....from day one ulikuwa "FYONGO" kwa upande wetu.......
........when it come to serious issues to takle na NIA IKO......Lowassa is very good at that..........
Indeed Lowasa is very good at that
Eti matatizo ya kuvunja mikataba anayajua kipindi alipokuwa waziri wa maji....huu ni upuuzi.Hivi kweli huyu ni mbunge wa jimbo gani kweli? Naombeni kujua ili mashambulizi tuyahamishie jimboni kwake.
 
Hapa kuna namna ya docs ya kuunganisha ili kupata picha halisi,. inahuzunisha kuwa TRL matatizo, ATC matatizo, TTCL Matatizo, sasa hivi sisi Watanzania tuna Nini??
Tumelogwa na aliyetuloga keshakufa, there is no way tunaweza kuamka usingizini.
 
Indeed Lowasa is very good at that
Eti matatizo ya kuvunja mikataba anayajua kipindi alipokuwa waziri wa maji....huu ni upuuzi.Hivi kweli huyu ni mbunge wa jimbo gani kweli? Naombeni kujua ili mashambulizi tuyahamishie jimboni kwake.

Leo ndo mnakumbuka EL teh teh teh
Huyu mbunge wa Bwagamoyo kama sijakosea.
 
Yaani bora hata ilivyokuwa TRC.Yaani hawa wawekezaji wana lao jambo.YAANI USOMI WA KAWAMBWA ndo analea ufyongo namna hii?hatari kweli kweli
 
Yaani bora hata ilivyokuwa TRC.Yaani hawa wawekezaji wana lao jambo.YAANI USOMI WA KAWAMBWA ndo analea ufyongo namna hii?hatari kweli kweli
Usomi wa mtu hausaidii lolote hapa ni wisdom and knowledge na falsafa ya kuelewa mambo ndio vinatumika. Hakuitaji Maths kwenye hili.
 
"Wananchi wawe wavumilivu kwa kuwa hali ya sasa ya TRL ni ya mpito ambayo itarekebishwa na kupatiwa ufumbuzi wa kudumu," alisema Bw. Kawambwa.
Kawambwa siamini kama ndo wewe hebu jiweke katika viatu vya wananchi then upime hayo maneno uliyotamka hapo
 
It doesn't click well in my mind hearing Dr Kawambwa talk crap like this.
 
Kawambwa siamini kama ndo wewe hebu jiweke katika viatu vya wananchi then upime hayo maneno uliyotamka hapo

Kahongwa na wahindi huyo ndo maana analinda ulaji wake.
Mtu mwenye akili timamu huwezi fumbia macho mkataba bomu kama huo
 
Waziri mzima anakiri uwezo wa mwekezaji ni mdogo, sasa kwa nini bado mnamuita mwekezaji? Kwa nini mliingia naye mkataba ?
 
trust me, huu mkataba....from day one ulikuwa "FYONGO" kwa upande wetu.......
........when it come to serious issues to takle na NIA IKO......Lowassa is very good at that..........

May be we should bring him back, looking at the way things are going now, i am not ashamed to say that !!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom