MKataba Tanzania na China Katika uendeshaji makaa ya mawe Mchuchuma na Liganga

G. Activist

JF-Expert Member
Nov 3, 2010
482
125
Hellow wana JF,

Leo tumeshuhudia utiliwaji wa saini wa uendeshaji wa miradi ya makaa ya mawe Liganga na Mchuchuma katika uzalishaji wa Umeme kati ya TANZANIA na CHINA. Nimefarijika kidogo na shughuli hii ya leo kama itasimamiwa sawasawa na ilivowekwa kwenye makaratasi, naamini kiasi fulani tutapunguza hili tatizo la Umeme linalotukabili.., Positive gain ya pekee ambayo watanzania tunatarajia ndo hiyo ya Nishati tu, otherwise ni loses tu ndizo tutakazopata.

Kinachoonekana hapa kikubwa ni wimbi la raia wa China kujaa hapa nchini, maana kila tunapoona viongozi wa Uchina wamezulu nchini, huwa kuna wimbi kubwa sana la Raia wa China kuhamia nchini, nasema kuhamia sababu sioni harakati zao za kuondoka. Hawa viongozi wajapo nchini huwa hawaangalii mambo mengi sana ikiwemo na fursa kwa raia wake, tofauti na viongozi wakwetu wakizulu huko ni misaada tu na kula goodtime..

Katika zoezi zima la utiliwaji wa saini nilitegemea kumuona Mheshimiwa Ngeleja akisimamia suala na vijana wake wa wizara, lakini hajaonekana zaidi ameonekana waziri wa Viwanda na Biashara na Mh. Makamu wa Rais cjui anaitwa nani maana mi hata cmjuagi jina lake. Sasa Je Ngeleja keshaona mkataba ni cheche ndo maana kakaa pembeni kupisha lawama za baadaye au ndo kasusa na kuacha mambo mazito kama haya kusimaamiwa na Makamu wa Rais? Cjaelewa vizuri hili.

Naomba kuwasilisha
.
 
China is starting to rule the world bro na hawa ni macapitalist wapya bado siamini kuwa miradi mikubwa kama hii tunahitaji msaada wa nchi nyingine yeyote ile duniani hii nchi tukiyabana tu vizuri makampuni yalipe kodi kama inavyotakiwa na kuziba ile mirija ya Kule TRA na Mafisadi wote na tukawa na mfumo mzuri wa ukusanyaji kodi tunaweza kutekeleza miradi kama hii kwa pesa zetu wenyewe.Usishangae mradi ukaisha na mgao ukaendelea kwa kasi zaidi na ari zaidi
 
China is starting to rule the world bro na hawa ni macapitalist wapya bado siamini kuwa miradi mikubwa kama hii tunahitaji msaada wa nchi nyingine yeyote ile duniani hii nchi tukiyabana tu vizuri makampuni yalipe kodi kama inavyotakiwa na kuziba ile mirija ya Kule TRA na Mafisadi wote na tukawa na mfumo mzuri wa ukusanyaji kodi tunaweza kutekeleza miradi kama hii kwa pesa zetu wenyewe.Usishangae mradi ukaisha na mgao ukaendelea kwa kasi zaidi na ari zaidi
Tuseme hatuna hizo fedha,ule mradi unaweza kujikopesha na kujiendesha.mimi sisemi tu kuwa tutapata mgao mdogo(20% inavyosemekana) bali tulipaswa kuuendesha wenyewe.jamani mimi nachoka hata kufikiri,hv tumechoka kupiga kelele? Wakati wanasiasa wote akili zipo igunga(which is very wrong maana hapa ni kupigania nyongeza za ruzuku tu).kuna mambo mengi mabovu sasa pengine kuliko wakati wowote,kasi ya swala la katiba nani analizungumzia sasa? Au ndo tunaishi kwa matukio kama ya babu wa loliondo.tumefika mahali wananchi wamechanganyikiwa nao wamegeuka mashabiki wa matukio kama ya ufisadi na hawana tena uchungu na kinachoendelea maana wamezoea! Wanasiasa na wanaharakati lazima washirikiane na kuainisha yapi yasimamiwe vizuri sasa kubadili mfumo uliopo.nimesikitishwa na taarifa za mkataba wa mchuchuma huku tukiwa kimya.umeme tulipofikia ni aibu lakini tumeishia kulalamika bila kuchukua hatua za kuishinikiza serikali ichukue hatua za dharura,tumeamua kusubiri ahadi ya umeme mwezi dec tena kutoka kwa watu waliokwisha prove failure! Tutahaidiwa na wabunge wetu kuwa bunge la mwezi Jan patachimbika kama umeme utakuwa bado ni tatizo.hizi ni sawa na ahadi za wachezaji wa taifa stars kuwa tutafia uwanjani lakini wanafungwa huku hakuna juhudi za kurekebisha makosa.lazima tujipange kimkakati kama wanasiasa,wanaharakati na wananchi wote tukiongozwa na viongozi wa upinzani ili tujue tunataka matokeo gani na si kutoa "tamko zito" tumeshayachoka haya.
 
Chinese mining firms in the earlier stages of the campaign of creating slave labour conditions with scant regard for safety or the local culture.

We shoulb be careful... they have becoming blood suckers... not Communists...
 
Nakumbuka wakati wanajenga TAZARA mwalimu aliwamanage kuwarudisha baada ya ujenzi sasa hawa wakija ndugu zangu Ludewa kazi ipo ila najua Wapangwa wako fiti.
Na hii serikali legelege watajaa apo kama nzi.
Vile vijembe vya Mzindakaya vilikuwa vya Ngeleja nini maana alisema naona kuna watu hawataki tudhubutu lakini sisi tunasonga mbele.
Yetu macho na masikio
 
Back
Top Bottom