MKASA: Ulaaniwe marehemu kaka. Alaaniwe Bibi Harusi wako pia

Storika Tz

Member
Dec 18, 2023
17
47
Ep 01
Sikuwahi kufikiria wala kuwaza kama kuna siku nitakuja kumchukia kwango cha kumlaani marehemu kaka yangu na Mkewe. Kiufupi, nawachukia sana, yeye marehemu kaka na bibi harusi wake, nawachukia sana, tena sana. Popotea ulipo marehemu Kaka Fred, iwe motoni au peponi, naomba ujue nakuchukia sana, wewe na bibi harusi wako.Wote wawili nawachukia sana, na mlaaniniwe ile laana ya nguruwe .

Naomba ungana nami kwenye hii simulizi kujua lipi ni lipi.

SEHEMU YA KWANZA.

Sikuwa tayari kuona Kaka yangu, Fred , akizikwa kwenye lile kaburi. Nilimfata baba na kumnongoneza. Baba aliniangalia kama mtu niliyechanganyikiwa. Aliyashangaa maneno yangu.

“ Hutaki azikwe kwenye hili kaburi?” Aliniuliza. Bila kupepesa macho nilimjibu. “ Ndio baba , sitaki.”

“ Kwahiyo ulitaka azikwe wapi?” Aliniuliza.

“ Tuchimbe kaburi lingine tumzike” Nilimwambia.

“ Ach masihara, naomba usiongee tena hilo jambo. Watu wakikusikia hapa wanaweza kukuhisi vibaya.:”

“ Lakini baba……..”

“ Hakuna cha lakini, naomba fanya kama nilivyokuambia. Sitaki uongee kuhusu hilo jambo.Tena kaa kimya kabisa.” Aliniambia Baba.

Nikiwa nawaza nifanye nini, Padre alimaliza kulibaliki kaburi, aliwaruhusu watu washushe mwili wa kaka Fred kaburini. Vijana waliweka kamba vizuri kwenye jeneza na kuanza kulishusha.

“ Yaani naruhusu huu upumbavu ufanyike mbele yangu! Hapana, kaka hawezi kuzikwa kwenye hili kaburi.” Nilijiambia moyoni. Niliwasogelea wale vijana na kuwasimamisha. “ Kaka yangu hawezi kuzikwa kwenye hili kaburi. Naomba msiendelee kushusha jeneza.” Niliwaambia.

“ Eeeeh!” Watu wote walishangaa. Vijana waliokuwa wanashusha jeneza waliangaliana kwa mshangao. Sura zao zilijaa maswali yasiyokuwa na majibu.

“ Mnashangaaa nini! Naomba toeni hilo jeneza humo, tutachimba kaburi lingine hapa pembeni.” Niliwaambia. Walinitii na kuanza kulivuta juu, lakini Kabla hawajamalizia kulitoa, Ndugu zangu waliwaambia waendelee, walinisogelea na kunishika mkono.

“ Kwanini unataka kuharibu msiba wa kaka yako?” Aliniuliza Baba.

“ Siwezi kukubali azikwe kwenye hili kaburi.Kamwe siwezi kukubali hilo.” Nilimwambia.

“ Tunashindwa kukuelewa John, hili kaburi lina nini?” Aliniuliza Mjomba Chriss.

“ Aaaah! Nyie hamuoni? Yaani hamuoni kabisaaa, eeeh! Hamuonii….”

“ Hatuoni ndio mana tunakuuliza, kama kuna lolote la ajabu tuambie. Usilete vurugu bila sababu.” Aliongea Baba.

Nikiwa najibizana na ndugu zangu, Jeneza lilishushwa kaburini.Kitendo cha kuniongelesha huku jeneza linashushwa kaburini kilinikera, niliona ndugu wananifanyia mchezo, wananizonga kwa maswali hili watu wazike. Niliamua kuwapita ili niende kuzuia tena.

“ Niliwaambia msishushe Jeneza! Nani aliyewaruhusu?” Niliwauliza wale vijana huku nikiwasogelea. Jeneza lilikuwa kaburi tayari. Akili yangu iliniambia niingie nikalitoe. Nilishika nguzo ya kaburi na kutaka kuingia.

Kabla sijaingia, nilivamiwa na ndugu na kutolewa pale msobe msobe.

“ Niacheni…niacheni…..” Niliwaambia huku nikijaribu kujinasua kwenye miili yao.

“ Msimuache, mpelekeni nyumbani….” Aliongea baba.

Walinifunga kamba na kunibeba msobe msobe mpaka nyumbani. Walinifungia chumbani na wao wakarudi makaburini kuendelea na mazishi. Nilijaribu kuvunja mlango nilishindwa, nilijaribu kukunja nondo za dirishani ili nitoke, nilishindwa pia.

“ Nafanyaje?” Nilijiuliza.

“ aaha…aha..aha…….aaaaaaaaaa….aaaaa……” Nilipiga kelele kuomba msaada. Hakuna aliyefika kunifungulia mlango.Nilikata tamaaa.

“ Nisamehe Kaka Fred, nimeshindwa kukusaidia.Nisamehe sana kaka.” Nilijisemea moyoni.

“ Lakini bado, vita haijaisha. Nitafanya jambo kukuokoa. Niamini mimi Fred, nitafanya jambo kukuokoa.” Nilijisemea moyoni tena.

…………………

Baada ya masaa kadhaa kupita, nilisikia sauti za watu wakija kutoka makaburini. Kuridi kwao kulimaanisha kaka yangu Fred amezikwa kwenye lile kaburi. Hii ilimaanisha nimeshindwa kumtetea.

Mlango wa chumba nilichofungiwa ulifunguliwa, aliingia baba akiwa na ndugu wengine. Walinikarisha chini na kunisema. Kwa muda wa masaa karibu matatu walinisema bila kunipa nafasi ya kujieleza. Walinieleza jinsi gani nilivyowadharilisha.

Sikutaka kubishana nao wala kuwaambia sababu ya kile nilichofanya.

Baada ya kisemo cha muda mrefu sana, waliondoka na kuniacha. Giza lilikuwa limeingia. Niliendelea kukaa mle ndani bila kutoka nje. Dakika ziliyoyoma, masaa yalikatika.

……………………

Majira ya saa nane usiku, nilitoka mle ndani. Watu wote walikuwa wamelala.

Niliingia store na kuchukua chepe, bila kuonwa na mtu yeyote nilikimbia kuelekea makaburini.

“ Ni lazima nimuhamishe kaka, siwezi kukubali azikwe kwenye lile kaburi.” Niliwaza huku nikielekea makaburini.

Dakika kadhaa mbele nilifika, niliyatoa mataji yote na kuyaweka pembeni. Nilianza kulifukua kaburi. Kwakuwa walizika siku ile ile kazi ya kufukua haikuwa ngumu, nilifukua mpaka mwisho, lakini Ajabu,Jeneza halikuwepo ,Kaburi lilikuwa tupu.

“ Eeeeeh!” Nilistaajabu.

Nakuja
 
ULAANIWE MAREHEMU KAKA- ALAANIWE BIBI HARUSI WAKO PIA- 02

“Eeeeh!” Nilistaaajabu.

Kwa dakika kadhaa ubongo wangu uliganda. Nilisimama bila kujua nifanye nini, nililiangalia kaburi mara tatu tatu, halikuwa na kitu ndani.

“ Inawezekana vipi?” Nilijiuliza. Nilingata tochi mdomoni, nilishika kuta za kaburi na kutoka nje.

“ Au nimechanganya ? au nimefukua kaburi tofauti na lile walilomzika ?” Nilijiuliza. Niliangaza kushoto na kulia kutafuta kaburi lingine, nililikosa. Hakukuwa na kaburi mpya zaidi ya lile nililolifukua.

“ Hapana, ni hili hili, alama ni huu mti.” Nilijiambia.

Pamoja na kupata mshtuko wa kutoona jeneza, wala sikuwa na hofu kubwa. Sifahamu ujasiri ulitoka wapi. Maisha yangu yote nilikuwa nayaogopa sana makaburi.Haikuwa sehemu rafiki kwangu, lakini ajabu, kwa mara ya kwanza , saa nane usiku nilikuwa makaburini lakini wala sikuogopa. Kiasi Fulani hadi mwenyewe nilijishangaa.

Nilikata shauri, niliamua kulifukia lile kaburi.

Nikiwa nimelifukia nusu, gafla, paka wawili weusi walitoka kaburini. Nilitupa chepe chini na kurudi nyuma kwa woga. Kwa mara ya kwanza hofu iliniingia, mapigo ya moyo yalienda kasi. Paka wale walitembea kwa madahaa kunisogelea.

Nilirudi nyuma kwa woga, “ Uuu….uuuuu…..uuuu….” Nilihema huku nikirudi nyuma. Mwanga mkali wa macho yao ulinifanya nijizibe macho na mikono yangu.

“ ahahahah…ahahaha..ahahah…..” Kilisikika kicheko kikubwa baada ya kujiziba macho. Nilitoa mikono haraka, mbele yangu wale paka hawakuwepo , na kile kicheko kiliacha kusikika.

“ Mmmmmh!” Niliguna, Sikushangaa tena, pale pale nilitimua mbio. Nikiwa sijafika popote nilijikwaa na kuanguka chini kama mzigo.

“ Ooooooh!” Niligumia kwa maumivu.

“ John…” Mtu aliniita na kunishika mkono. Niligeuza kichwa kumtazama, alikuwa Shemeji yangu, mke wa marehemu kaka yangu.

“ Eeeeeh!” Nilistaajabu.

“ Usishtuke, najua kila kitu. Kama ilivyokuwa kwako, na mimi marehemu alinipa maagizo. Hivyo tupo pamoja, naomba tushirikiane.” Aliniambia.

“ Usiku huu wa manane ulikuwa unaenda wapi?” Nilimuuliza.

“ Naenda ulikotoka wewe. Naenda kaburini kutimiza agizo la mume wangu.” Alinijibu.

“ Hakuna usalama kule, usiende. Jeneza la marehemu kwenye kaburi halipo, pia kuna mambo ya kutisha ndio mana unaona nakimbia.” Nilimwambia.

“ Ulienda kitoto ndio mana imekuwa hivyo. Twende , hakuna baya lolote litakalotokea.” Aliniambia . Alinishika mkono na kuninyanyua. Nafsi yangu ilisita , pamoja na kusita nilitamani kujua nini kitatokea. Niliongozana naye kuelekea makaburini.

Njia nzima nilikuwa namuangalia Shemeji bila kummaliza. Nilijiuliza manane yale ya Usiku iweje asiogope. Tukiwa tunakaribia nilimshika mkono na kumsimamisha.

“ Hujaniambia maagizo aliyokupa kaka ni yepi?”

“ Utajua tukifika, saizi hupaswi kujua.” Aliniambia.

“Kwanini usiniambie hapahapa.” Nilimwambia huku nikisimama vizuri.

“ Unanichelewesha John, hebu twende.” Aliniambia. Nilipiga hatua kwenda. Zikiwa zimebaki mita chache kufika kaburini, Mwili wangu ulisisimka sana, damu ilichemka. Nilihisi nyuma yangu kuna kitu kisicho cha kawaida, Haraka , nilitaka kugueza shingo ili nitazame, kabla sijafanikiwa kugeuka , Shemeji aliniwahi.

“ Usigeuke nyuma, ni hatari.” Aliniambia.

“ Eeeeeh!”

“ Ni hatari, kwa muda wote tutakao kuwa hapa hautakiwi kugeuka nyuma. Ukigeuka nyuma habari yako imeisha.” Aliniambia.

Maneno yake yalinizidishia hofu, mikono ilitetemeka, miguu iliishiwa nguvu kabisa, nilijikaza nisianguke. Damu yangu ilichemka, moyo ulipiga kwa kasi ya ajabu, nilihisi unataka kutoka, niliweka mikono kifuani.

“ Mbona mara ya kwanza nilipofika haikuwa hivi?” Nilijiuliza.

Shemeji baada ya kuona hali yangu mbaya, alinishika mkono na kunivuta, nikawa natembea kuelekea makaburi kwa msaada wake. Sijui kwanini, baada ya kunishika mkono hofu yangu ilipungua. Sikutetemeka wala mapigo ya moyo hayakwenda kasi sana. Tulifika, alinisisitiza nisigeuke nyuma.

“ Ulikuwa unataka kujua maagizo aliyonipa kaka yako ni yepi?” Aliniuliza .

“ Ndio, nataka kujua hayo maagizo ya kuja kuyatekeleza saa nane usiku?” Nilimwambia .

“ Ahahah..ahahah….” Alicheka Shemeji. Sura yake haikuonesha hofu yoyote, ilikuwa ni kama yupo sehemu salama kupita zote.

“ Kabla sijakuambia, kwanza naomba niambie maagizo aliyokupa wewe? Kwanini ulikuwa hutaki azikwe kwenye hili kaburi? Na kwanini umefika usiku wa manane kwenye kaburi lake” Aliniuliza.

“ Aaaaah…aaaaaaa…..” Nilijiuma uma. Sikuwa tayari kumwambia. Nikiwa najiuma uma, macho yangu yalitua kwenye lile kaburi, lilikuwa vile vile kama nilivyoliacha.

“ Eeeeh! Halafu wewe ndiye uliolifukua? Mbona umeacha hivi?” Aliniuliza.

“ Kabla sijafukia vilitokea vitu vya ajabu. Sikuwa na jinsi niliamua kukimbia.” Nilimwambia.

“ Halafu umesema jeneza alipo?”

“ Ndio , halipo,”

“ Mmmmh! Sidhani,” Aliongea shemeji huku akiingia kaburini. Alichukua chepe na kuanza kutoa mchanga.

“ Mbona lipo, jeneza si hili hapa.” Aliniambia. Nilisogea haraka kutazama, ni kweli lilikuwepo.

“ Lakini inawezekana likawa halina kitu, maana dunia ya sasa sio kabisa.” Aliongeza shemeji na kunipa ishara ya kwenda kumsaidia kulifungua. Niliingia ndani ya kaburi na kwa pamoja tukaanza kulifungua ili kuhakikisha kama mwili wa marehemu upo.

Tulifanikiwa kulifungua, ajabu, kama alivyoongea, jeneza halikuwa na kitu ndani. Jeneza lilikuwa tupu. Nilimwangalia shemeji kwa mshangao, Yeye hakuonesha kushangaa, alikuwa anatabasamu tu. Nikiwa nashangaa waliingia watu wawili kaburini ambao sifahamu walitoka wapi. Walinishika kwa nguvu na kuniingiza kwenye lile jeneza.

Wakati yanatendeka hayo, shemeji alinipungia mkono. “ Byeeeeee…byeeeeeeeee….” Aliniambia.

Leo nime waunga watu 300 kwenye group la whatpp bure kama sijakuunga emb nitext now whatpp 0768315707
 
ULAANIWE MAREHEMU KAKA- ALAANIWE BIBI HARUSI WAKO PIA -03

Wakati yanatendeka hayo, shemeji alinipungia mkono.

“ Byeeeeee…byeeeeeeeee….” Aliniambia.

Nilijitutumua kujitoa nilishindwa, waliniingiza kwenye jeneza na kulifunika. Nililipiga mangumi kwa ndani, nilihangaika kujitoa nilishindwa.

Baada ya kuniingiza kwenye jeneza, wao walitoka nje. Nilisikia kishindo cha kifusi kikitua juu ya jeneza. Pumzii iliniishia taratibu macho yangu yalianza kuona vitu visivyoeleweka, Gafla, nilitulia tuli, sikusikia, sikuhisi, wala sikuona chochote.

………………………..

SIKU YA PILI YAKE.

Asubuhi na mapema nilitoka chumbani kwangu na kusimama uwanjani. Kichwa kilikuwa kikiniuma kupita maelezo, nilichukua maji na kujimwagia. Nikiwa najimwagia maji, alikuja baba.

“ John jana usiku ulikuwa wapi?” Aliniuliza.

“ Eeeeh! Kweli, jana usiku sikuwa hapa.” Nilijiambia. Nilijaribu kuwaza nilikokuwepo sikupata jibu.

“ Mmmmh! Nilienda wapi usiku wa jana?” Nilijiuliza. Sikuwa na kumbukumbu ya lolote lile.

“ Umeondoka hapa saa nane usiku, kunamtu alikuona na chepe. Kuanzia saa nane mpaka saa kumi tumekutafauta bila mafanikio, na chumbani kwako haukuwepo. Ulienda wapi?” Aliniuliza Baba.

Niliwaza na kuwazua , sikupata majibu ya sehemu niliyokuwa.

“ Ulikuwa wapi! Na umerudi saa ngapi? Maana toka saa nane tuliyokutafuta mpaka asubuhi hii watu hawakulala, si unawaona wale uwanjani, waliwasha moto na kuota, na hakuna aliyekuona ukirudi? Inakuwaje unatokea ndani?’ Aliniuliza Baba.

“ Mbona sikumbuki kitu baba.” Nilimwambia.

“ Eeeeh! Hukumbuki kabisa.”

“ Ndio” Nilimjibu.

Nikiwa namjibu baba, kijana mmoja aliyekuwa anaota moto pale uwanjani alikuwa akiniangalia kwa jicho ambalo sikulielewa, nilipomuangalia alikwepesha macho. Aliangalia chini.

“ Atakuwa anajua kitu” Nilijiambia. Nilimwacha baba akiwa kasimama. Nilimfata yule kijana. Alipoona namfata, haraka, alisimama na kutimua mbio.

“ Eeeeh!” Nilishangaa. Niliamua kumkimbiza.

“ John…john….john…..” Baba na ndugu zangu wengine waliniita, waliniambia nimuache yule kijana. Sikuwajali, niliendelea kumfukuza. Nikiwa namkaribia, alijikwaaa na kuanguka chini. Nilimshika shati na kumuinua.

“ Kwanini ulikuwa unaniangalia vile?” Nilimuuliza.

“ Aaaa…..aaaaa……..” Alishikwa na kigugumizi. Alishindwa kuongea.

“ Niambie kwanini ulikuwa unaniangalia vile? Unajua nilipoenda jana? Unajua nilivyorudi?” Nilimuuliza. Alitikisa kichwa ishara ya kutojua kitu.

“ Kama hujui kwanini ulikuwa unakimbia?”

“ aaaa…ee……ooooo…aaaa…..” Alitamka kwa kigugumizi maneno yasiyoeleweka.

Baba na ndugu zangu walifika.

“ Amefanya nini kijana wa watu?” Aliniuliza baba.

“ Nazani anajua sehemu niliyoenda jana, nataka aniambie ili nikumbuke.” Nilimwambia.

“ Ni bubu huyo, hawezi kuongea . Halafu usitufanye sisi wapumbavu tuambie ulikoenda na umerudi saa ngapi ? . Kujifanya kwako umesahau hakuwezi kukusaidia kitu.” Aliongea baba.

“ Kwahiyo baba huniamini? Kwanza nidanganye ili iweje. Sikumbuki kitu kabisa. Kila nikijaribu kukumbuka kichwa changu kinawaka moto.” Niliwaambia. Na ilikuwa kweli, sikukumbuka lolote lile.

“ Mmmmmh!” Aliguna baba. Nilimwacha yule kijana, niliongozana na ndugu zangu kurudi nyumbani. Moja kwa moja tulipitiliza barazani. Baada ya kuketi, baba alinitazama kisha akaniuliza.

“ Unakumbuka ulichokifanya makaburini wakati wa kuzika?” Aliniuliza.

“ Makaburini…makaburini…..makaburini….” Nilijaribu kuvuta kumbukumbu. Ilikuwa bure, sikukumbuka chochote kile.

“ Mbona sikumbuki kitu.”

“ Mmmmmmh! Umerogwa sio bure” Aliongea Mjomba Chriss.

“ Ni kweli, mwanangu atakuwa amechezewa sio bure. Anawezaje kusahau tukio kama lile?” Aliuliza baba.

“ Hayo yameshatokea, tuachane nayo, nazani baada ya muda kumbukumbu zake zitarudi zenyewe. Kwasasa ni vyema tukaongea jambo la msingi ambalo linamkabili mbele yake.” Aliongea mama. Baba na wajomba zangu walitikisa vichwa kukubaliana na mama.

“ Jambo gani linalonikabili ?” Niliwauliza.

“ Kabla ya kuongea naomba muiteni muhusika mwenyewe.” Aliongea baba. Mama alitoka nje, sekunde kadhaa mbele alikuja akiwa kaongozana na shemeji, mke wa marehemu kaka.Nilipomuona tu, mapigo yangu ya moyo yalienda kasi, mwili wangu wote ulisisimka. Nywele zilisimama.

“ Mbona nimekuwa hivi? “ Nilijiuliza. Nilimuangalia shemeji huku nikijaribu kukumbuka kama kuna lolote linalonifanya niwe vile, nilikosa. Kila nilipojaribu kukumbuka, kumbukumbu nzuri zilinijia. Nilikumbuka jinsi alivyokuwa anampenda kaka, nilikumbuka jinsi alivyokuwa mkarimu kwetu tulipoenda kuwatembelea.

Baada ya kukumbuka wema wake, mapigo yangu yalitulia, mwili ulipoa. Nilimuangalia macho yetu yakagongana, kwa aibu nikakwepesha.

“ John…” Aliniita baba.

“ Naaam….” Niliitika.

“ Unamuona shemeji yako? Mke wa marehemu kaka yako?” Aliniuliza.

“ Ndio namuona” Nilimjibu.

“ Sasa…………………………..


Leo nime waunga watu 300 kwenye group la whatpp bure kama sijakuunga emb nitext now whatpp 0768315707
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom