Mkasa wa jamaa yangu kuhusu mtoto

Mkasa wa jamaa yangu kuhusu mtoto

co fm

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2016
Posts
1,569
Reaction score
2,584
Habarini wadau, ningependa kushare na nyinyi humu jf kuhusiana na mkasa wa rafiki yangu ambaye sasa hivi yupo kama haelewi.Alikuwa na mahusiano na binti mmoja hivi kwa miaka kama miwili iliyopita, baadae mahusiano yakawa yameisha. Amekaa baada ya miezi 8 ya mahusiano yao kuisha, yule mwanamke akamwambia amezaa na mtoto ni wake, jamaa alivyoambiwa hivyo akakataa sio kwamba anamkana bali alisema yaani upate mimba hadi kujifungua hujaniambia halafu leo unasema una mtoto wangu hiyo haiwezekani.

Basi wamekaa kama mwaka hivyi jamaa nakuja kugundua yule mwanamke ameolewa na jamaa(mume) ila yule jamaa(mume) anadai yule sio mtofo wake amesingiziwa ila tu kuficha aibu ya yule mwanamke, na yule mwanamke amerudi kwa jamaa(mshikaji wangu) na kumwambia tena huyu mtoto ni wako na baba mlezi hamtaki ni kama ameumbuka. Hebu wadau tushauriane
 
Huyo anayesema haiwezekani kisa kachelewa kuambiwa anataka mtoto wake au anamtaka mwanamke?
Yeye anasema kama ni wake apewe, sio kwamba huwezo hana
 
Habarini wadau, ningependa kushare na nyinyi humu jf kuhusiana na mkasa wa rafiki yangu ambaye sasa hivi yupo kama haelewi.Alikuwa na mahusiano na binti mmoja hivi kwa miaka kama miwili iliyopita, baadae mahusiano yakawa yameisha. Amekaa baada ya miezi 8 ya mahusiano yao kuisha, yule mwanamke akamwambia amezaa na mtoto ni wake, jamaa alivyoambiwa hivyo akakataa sio kwamba anamkana bali alisema yaani upate mimba hadi kujifungua hujaniambia halafu leo unasema una mtoto wangu hiyo haiwezekani.

Basi wamekaa kama mwaka hivyi jamaa nakuja kugundua yule mwanamke ameolewa na jamaa(mume) ila yule jamaa(mume) anadai yule sio mtofo wake amesingiziwa ila tu kuficha aibu ya yule mwanamke, na yule mwanamke amerudi kwa jamaa(mshikaji wangu) na kumwambia tena huyu mtoto ni wako na baba mlezi hamtaki ni kama ameumbuka. Hebu wadau tushauriane
Mwambie jamaa yako amchukuwe huyo mtoto kwa moyo mmoja ndugu, Mtoto hana shida yoyote bali walio mleta Duniani ndio wana shida zao binafsi. Amchukuwe amlelee vyema na Mungu atambariki.
 
Mwambie jamaa yako amchukuwe huyo mtoto kwa moyo mmoja ndugu, Mtoto hana shida yoyote bali walio mleta Duniani ndio wana shida zao binafsi. Amchukuwe amlelee vyema na Mungu atambariki.
Tatizo ni kwann sasa hivi ndo aonekane ni wake?
 
Tatizo ni kwann sasa hivi ndo aonekane ni wake?
Sijakataa kumbuka wanadamu hatuja kamilika, sasa tunapotaka kutafuta mchawi wakati wote wanamakosa anaeumia ni Mtoto na wazazi ndio wana makosa kwanini mtoto ateseke bure? Hekima na busara itumike hapo amani na haki ya msingi matunzo mtoto apate, mengine ni kusameheana na kusonga mbele kwa ustawi wa mtoto.
 
Nitafuteni twende tukapime DNA, usije ukabeba mzigo kulea mtoto asiye wako na usije ukakataa kulea kumbe ni damu yako.
 
Sijakataa kumbuka wanadamu hatuja kamilika, sasa tunapotaka kutafuta mchawi wakati wote wanamakosa anaeumia ni Mtoto na wazazi ndio wana makosa kwanini mtoto ateseke bure? Hekima na busara itumike hapo amani na haki ya msingi matunzo mtoto apate, mengine ni kusameheana na kusonga mbele kwa ustawi wa mtoto.
Ok.
 
Nitafuteni twende tukapime DNA, usije ukabeba mzigo kulea mtoto asiye wako na usije ukakataa kulea kumbe ni damu yako.
DNA utaratibu wake umekaaje na bei je?
 
Mwambie azingatie Msemo "Kwenye Ndoa zenu kuna Watoto wetu!"
 
Ona wapumbavu wanavyomnyanyasa huyo mtoto ,kuna mambo ni kumdhalilisha mtoto kwa namna yoyote ile hata wakienda kumpima DNA kwa jicho la pili ni kumdhalilisha huyo Mtoto.

Hapo mambo ya kutupiana mzigo mwishoe ni kumuharibu kiasaikolojia huyo mtoto ,baba na mama wote vichaa hapo
 
Habarini wadau, ningependa kushare na nyinyi humu jf kuhusiana na mkasa wa rafiki yangu ambaye sasa hivi yupo kama haelewi.Alikuwa na mahusiano na binti mmoja hivi kwa miaka kama miwili iliyopita, baadae mahusiano yakawa yameisha. Amekaa baada ya miezi 8 ya mahusiano yao kuisha, yule mwanamke akamwambia amezaa na mtoto ni wake, jamaa alivyoambiwa hivyo akakataa sio kwamba anamkana bali alisema yaani upate mimba hadi kujifungua hujaniambia halafu leo unasema una mtoto wangu hiyo haiwezekani.

Basi wamekaa kama mwaka hivyi jamaa nakuja kugundua yule mwanamke ameolewa na jamaa(mume) ila yule jamaa(mume) anadai yule sio mtofo wake amesingiziwa ila tu kuficha aibu ya yule mwanamke, na yule mwanamke amerudi kwa jamaa(mshikaji wangu) na kumwambia tena huyu mtoto ni wako na baba mlezi hamtaki ni kama ameumbuka. Hebu wadau tushauriane
[/QUOT vijana acheni kukwepa majukumu kuna laana mnajitakia huwez toboa katika maisha
 
Kama huyo mtoto ni wa kike lete nimkuze mwenyewe
 
Ona wapumbavu wanavyomnyanyasa huyo mtoto ,kuna mambo ni kumdhalilisha mtoto kwa namna yoyote ile hata wakienda kumpima DNA kwa jicho la pili ni kumdhalilisha huyo Mtoto.

Hapo mambo ya kutupiana mzigo mwishoe ni kumuharibu kiasaikolojia huyo mtoto ,baba na mama wote vichaa hapo
Mkuu si ni bora kufanya hivyo ila kuwa na uhakika, kama ni wake au lah
 
Ona wapumbavu wanavyomnyanyasa huyo mtoto ,kuna mambo ni kumdhalilisha mtoto kwa namna yoyote ile hata wakienda kumpima DNA kwa jicho la pili ni kumdhalilisha huyo Mtoto.

Hapo mambo ya kutupiana mzigo mwishoe ni kumuharibu kiasaikolojia huyo mtoto ,baba na mama wote vichaa hapo
Mtoto kulelewa na baba asiye wake ni kumnyima haki yake (mtoto) kumfahamu baba yake na kufurahi nae.
 
Ona wapumbavu wanavyomnyanyasa huyo mtoto ,kuna mambo ni kumdhalilisha mtoto kwa namna yoyote ile hata wakienda kumpima DNA kwa jicho la pili ni kumdhalilisha huyo Mtoto.

Hapo mambo ya kutupiana mzigo mwishoe ni kumuharibu kiasaikolojia huyo mtoto ,baba na mama wote vichaa hapo

hawakujua maana ya uzazi wa mpango
 
Back
Top Bottom