Mkanganyiko wa Katiba ya Sasa

Wakati wa kusainiwa mkataba wa Muungano, yalikuwa mambo 17. Baadaye yakaongezwa mpaka kufikia 24.

Misaada na mikopo ya nje, ni kweli ni jambo la Muungano. Zanzibar inastahili kupewa asilimia fulani (sina uhakika, lakini nadhani ni asilimia 4). Lakini pesa hiyo hukabidhiwa kwa Serikali ya Zanzibar kwaajili ya kugharamia mambo yasiyo ya Muungano, afya ni mojawapo. Pesa hiyo ikipelekwa Zanzibar, inatumika kwa kadiri ya maamuzi ya Serikali ya Zanzibar na Baraza la wawakilishi. Kwenye hilo msemaji haiwezi kuwa serikali ya JMT wala Rais wa serikali ya JMT. Hili la CT scan, kwa nini maamuzi na msemaji awe serikali ya JMT?
Unapaswa kufahamu kwamba utendaji wote kwa Serikali upo chini ya Rais. Mawaziri, kwa mujibu wa katiba,wanafanya kazi kwa niaba ya Rais, hivyo Rais anaweza, kama alivyofanya, kuelekeza
 
Wakati wa kusainiwa mkataba wa Muungano, yalikuwa mambo 17. Baadaye yakaongezwa mpaka kufikia 24.

Misaada na mikopo ya nje, ni kweli ni jambo la Muungano. Zanzibar inastahili kupewa asilimia fulani (sina uhakika, lakini nadhani ni asilimia 4). Lakini pesa hiyo hukabidhiwa kwa Serikali ya Zanzibar kwaajili ya kugharamia mambo yasiyo ya Muungano, afya ni mojawapo. Pesa hiyo ikipelekwa Zanzibar, inatumika kwa kadiri ya maamuzi ya Serikali ya Zanzibar na Baraza la wawakilishi. Kwenye hilo msemaji haiwezi kuwa serikali ya JMT wala Rais wa serikali ya JMT. Hili la CT scan, kwa nini maamuzi na msemaji awe serikali ya JMT?
Orodha ya asili ilikuwa na mambo 11 tu kwa orodha
 
Ukiingalia katiba ya Tanzania, ni kama vile ilifikiriwa kuwa wakati wote Rais atakuwa Mtanganyika.

Tanganyika iliungana na Zanzibar kwenye mambo machache, nadhani wakati ule yalikuwa 17 tu.

Hayo mambo 17 pekee ndiyo yalikuwa chini ya Serikali ya JMT. Mambo hayo yalikuwa ni pamoja na Ulinzi, Mambo ya ndani, Uhusiano wa Kimataifa, Sarafu, Elimu ya juu, n.k.

Mambo yaliyobakia kama vile Afya, Elimu, Utamaduni, Kilimo, Biashara, yalibakia kuwa chini serikali za maeneo (Tanganyika na Zanzibar). Mambo haya kwa upande wa Zanzibar yangesimamiwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar chini ya Rais wa Zanzibar. Na kwa upande wa Tanganyika, yangesimamiwa na Serikali ya JMT chini ya Rais wa JMT. Kwa mantiki hiyo, ni kwamba kuna wakati Rais wa JMT anakuwa Rais wa nchi ya Tanzania (anaposimamia utekelezaji wa yale mambo ya Muungano), na kuna wakati anakuwa Rais wa Tanganyika (anapotekeleza mambo yale ya Tanganyika yasiyo chini ya Muungano).

Mambo ya Kufikirisha:

1) Kila raia wa Zanzibar ni raia wa Tanzania

2) Siyo kila raia wa Tanzania ni raia wa Zanzibar.

3) Kila raia wa Zanzibar na Tanganyika ana haki ya kushika uongozi au kuwa mtumishi kwenye taasisi zinazosimamia mambo yale ya Muungano.

?? Jana nimesikia kuwa eti Rais wa JMT ameagiza serikali ya JMT inunue CT scan machines kwaajili ya hospitali zote za mikoa ya bara na visiwani. Ina maana suala la Afya, nalo limeingizwa kwenye mambo ya muungano? Au mkanganyiko wa katiba unamfanya Rais akose kutambua mipaka ya mamlaka ya Rais wa JMT kwenye mambo yasiyo ya muungano?

JUMUISHO
Kuna wakati Rais wa JMT anafanya kazi kama Mkuu wa nchi ya JMT (wakati huo anasimamia yale mambo ya Muungano tu) na kuna wakati anafanya kazi kama Rais wa Tanganyika (anasimamia mambo yale yasiyo ya Muungano).

SWALI
Raia wa Zanzibar, ambaye siyo raia wa Tanganyika, anakuwa na uhalali gani kuwa Rais wa Tanganyika (ili kusimamia mambo yale yasiyo ya muungano)? Au Mwalimu Nyerere alidhani wakati wote, Rais wa JMT atatoka bara tu?

Waliosema katiba ina mkanganyiko, naona wapo sahihi sana. Na aliyesema Tanganyika imejivika koti la muungano, naye yupo sahihi.

KATIBA MPYA YENYE UFAFANUZI SAHIHI NA WENYE MANTIKI HAIIEPUKIKI.
@Pascal Mayalla mtaalam wananzengo wanakusubiri kwenye numbaga uwafafanulie tafadhali

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Afya haimaanishi CT scan pekee yake. Zanzibar wangeweza kupewa sehemu yao, na kuambiwa kuwa dhumuni la mkopo huu (ambalo najua kuwa wanajua) ni kwenye afya. Huko kwenye afya watafanya nini, niaamuzi yao na wala siyo jukumu la Samia.
Unafahamu mahitaji ya hizo mashine kwa hospital kuu za Zanzibar?
 
Wakati wa kusainiwa mkataba wa Muungano, yalikuwa mambo 17. Baadaye yakaongezwa mpaka kufikia 24.

Misaada na mikopo ya nje, ni kweli ni jambo la Muungano. Zanzibar inastahili kupewa asilimia fulani (sina uhakika, lakini nadhani ni asilimia 4). Lakini pesa hiyo hukabidhiwa kwa Serikali ya Zanzibar kwaajili ya kugharamia mambo yasiyo ya Muungano, afya ni mojawapo. Pesa hiyo ikipelekwa Zanzibar, inatumika kwa kadiri ya maamuzi ya Serikali ya Zanzibar na Baraza la wawakilishi. Kwenye hilo msemaji haiwezi kuwa serikali ya JMT wala Rais wa serikali ya JMT. Hili la CT scan, kwa nini maamuzi na msemaji awe serikali ya JMT?
Hapo ndipo utata ulipo, which means Mh. Rais ata set precedence mbaya kwa Zanzibar, kesho akiwa siyo mzanzibar naye ataamua awape kingine kwa utashi wake bila kujali Zanzibar ina maamuzi yake inapokuja kwenye maswala yake ya ndani
Asante kwa kujadili vema. Ila, Zanzibar inaheshimiwa sana na sisi sote ni Watanzania.

Pili,maelekezo ya hizo mashine si hisani ni sehemu ya kudumisha Muungano wetu.

3. Zingatia malengo ya hizo fedha. Ni afya. Pia hadi Rais anaelekeza anajua hali ya Zanzibar. Rais ni taasisi.
Ahsante kwa mjadala wa kiustaarabu.

Nami niongezee hili, kweli u Rais ni taasisi lakini inyoongoza watu na kwa mujibu wa sheria, siyo inayojisimamia yenyewe zipo na zingine nisiende huko kwa maslahi mapana ya nchi yetu.

Mfano, mdau amesema Katiba inasema mambo hayo yalitakiwa yajadiliwe na Baraza la Wawakilishi na kisha anayewajibika kulisemea ni Rais wa Zanzibar na siyo wa Tanzania kwakua ni mambo ya ndani ya Zanzibar, je hapo taasisi ya u Rais wa Tanzania inaingiaje?

Lengo liwe ni kukubali kuongozwa na sheria, kanuni na taratibu na iwe consistent isiwe inabadilika badilka kila anapoingia mtu wa tofauti kwenye hizo taasisi.
 
Kila siku nasema ujinga ulifanywa na viongozi wetu wa Tanganyika wakati huo wa kuungana kukubali kuwaachia Zanzibar mambo yao halafu wao ndio wakajiona wajanja kwa kuigeuza Tanganyika kuwa ndio Tanzania matokeo yake ndio haya sasa.
 
Ndio maana tulipounga Kuna Mambo yalifanywa kuhusu muungano na mengine siyo ya muungano, afya sio swala la muungano. Mara nyingi Zanzibar amekopa kupitia serikali ya muungano na sio hisani kikatiba Zanzibar anaruhusiwa kupata asilimia 4 ya misaada na mikopo leo iweje pesa za tanganyika ziende Zanzibar
Siyo hisani ya fedha za Tanganyika ni haki ya Zanzibar.

Lakini pia, kuna ubaya gani kwa mfano,Zanzibar kuwasaidia ndugu zao wa Bara na Bara kuwassidia Wazanzibari? Kwa nini vitu vizuri tunataka kuviingizia fikra hasi?
 
Siyo hisani ya fedha za Tanganyika ni haki ya Zanzibar.

Lakini pia, kuna ubaya gani kwa mfano,Zanzibar kuwasaidia ndugu zao wa Bara na Bara kuwassidia Wazanzibari? Kwa nini vitu vizuri tunataka kuviingizia fikra hasi?
Wangekuwa na nia ya kusaidiana tusingesikia malalamiko yao ndio maana tunaitaka Tanganyika yetu
 
1) Kila raia wa Zanzibar ni raia wa Tanzania

2) Siyo kila raia wa Tanzania ni raia wa Zanzibar.
hiyo number 2 ina sura ya ubaguzi....

Mwalimu alipoulizwa hili alisema eti wazazibar ni wachache na ardhi yao si kubwa, kwa hili ni lazima katiba iwalinde....

Je haya tuliyajadili kwa pamoja au wachache ndiyo walituamulia wakati wa kutungwa katiba hii? mliokuwepo mwaka 1977 tujuzeni mchakato ulifanyikaje?
 
?? Jana nimesikia kuwa eti Rais wa JMT ameagiza serikali ya JMT inunue CT scan machines kwaajili ya hospitali zote za mikoa ya bara na visiwani. Ina maana suala la Afya, nalo limeingizwa kwenye mambo ya muungano? Au mkanganyiko wa katiba unamfanya Rais akose kutambua mipaka ya mamlaka ya Rais wa JMT kwenye mambo yasiyo ya muungano?
Tatizo kubwa hapa ni Tanganyika kukosa mtetezi wa kweli.. Imegeuka Shamba la bibi
 
Pili, rejea hizo fedha Rais alizoagiza ziende Zanzibar. Kama ni za IMF huo ni mkopo wa Kimataifa kwa Tanzania. Zanzibar haikopi ktk taasisi za Breton woods kama IMF na WB. Hivyo mkopo huo ni wa nchi yetu na Zanzibar ni sehemu ya Tanzania, ina haki ya kunufaika.
Lkn kuna kanuni ya mgawo wa hizo fedha . Siyo kama anavyonya rais. Ndege zimeletwa mbili, moja inaenda Zanzibar, fedha zimekuja anagawanya bila formula. Mwambieni huyu mama kwamba awakwaza watanganyika.
 
Afya sio suala la muungano, Zanzibar wao wenyewe wanawajibika kupanga na kuamua kuhusu mambo ya afya na sio kuamuliwa na serikali ya muungano. CT scan ni jambo la afya kwa 100% halikupaswa kufanyiwa maamuzi na Rais Samia, ni makosa makubwa. Ni kujipendekeza kulikovuka mipaka.

Samia alikosea, huenda hajui sheria au hajui mipaka ya maamuzi yake kikatiba, nahisi bado anawaza kijinsia (kike) na Kikanda (mzanzibar) hatambui kama yeye ni Rais wa Tz.
Muungano huu ufe tu, una manufaa kwa watu wachache sana wenye maslahi binafsi.
 
Unapaswa kufahamu kwamba utendaji wote kwa Serikali upo chini ya Rais. Mawaziri, kwa mujibu wa katiba,wanafanya kazi kwa niaba ya Rais, hivyo Rais anaweza, kama alivyofanya, kuelekeza
Nadhani huelewi hoja iliyopo. Waziri wa afya aliye chini ya Rais wa JMT ni Waziri wa Afya wa huku bara na siyo Waziri wa afya wa Zanzibar.

Kwenye suala la afya, Rais wa JMT hana mamlaka juu ya Zanzibar. Na wala waziri wa afya wa huju bara, hana mamlaka juu ya Zanzibar, isipokuwa linapokuwa kwenye kiwango cha kimataifa.
 
Orodha ya asili ilikuwa na mambo 11 tu kwa orodha
Asante kwa kunirekebisha. Nadhani upo sahihi. Mwanzoni yalikuwa 11, baadaye 17.

Sasa kama Rais Samia na mwenzie Mwinyi wameamua kuongeza na Afya liwe suala la Muungano, wapeleke kwenye bunge la JMT na Baraza la Wawakilishi, ili ikapitishwe kikatiba.
 
Back
Top Bottom