Licking Wounds
JF-Expert Member
- Nov 28, 2014
- 3,800
- 4,850
Mkuu katika ubora wako! Asante sanaHii michezo ya Mind-Control ipo sana, kuna mashirika ya kijasusi kama C.I.A, MI6, MOSSAD na SVR yamefuka mbali sana kwenye suala zima la ujasusi. Huu ujasusi wa kudukua simu, kuteka watu na kung'oa kucha kwao ni vitu vya kizamani mno. Wakati Urusi ya Kisovieti imeanzisha shirika la kijasusi The Cheka, mkurugenzi wao wa kipindi hicho Myahudi Felix Dzerzhinsky alikuwa anatumia huu mchezo.
Inasemekana SLEEPING-DEPRIVATION ni moja ya mbinu ambayo humfanya mwanadamu apoteze mamlaka ya ubongo wake wa hiyari (Conscious Mind) na ubongo usiyo wa hiyari (Subconscious Mind) ndiyo unafanya kazi. Ubongo usiyo wa hiyari ndiyo unatunza kumbukumbu zako zote na ndiyo unatengeneza tabia zako (Characters) na lugha ya mwili (Body Language).
Akiyafahamu haya, Felix aliwaambia majasusi wake waanza kufanya mahojiano (Interrogations) usiku wa manane na watumie njia ya SLEEPING-DEPRIVATION ili kupata taarifa. Alifanikiwa kwa kiwango kikubwa mno katika hili. Hili lilitokea tena kule Ujerumani ya wanazi, ambapo inasemekana wenyewe walikuwa wanafanya majaribio ya kutengeneza The Superman ( Übermensch) hivyo walifanya haya majaribio ya kucheza na ubongo wa binadamu.
Kinachosikitisha sana sisi watanzania na dunia haya mambo ndiyo tumeanza kuyafahamu leo, lakini wana saikolojia kama Sigmund Freud waliaandikia haya mnamo karne za 19 na 20. Freud yeye akiwa ndiye The Father of Modern Psychology ameandika mambo ya ajabu mno na ya kuogopesha kuhusu ubongo wa mwanadamu na tabia zake. Sasa hawa wenzetu wameanza kucheza navyo hivi vitu miaka hiyo.
Jambo ambalo linaogopesha zaidi na nadhani wanadamu huwa tunalisahau ni kwamba wanazi hawakuishia kule The Nuremberg Tribunal ila walipelekwa Marekani na The Dulles Brothers. Wanasayansi wote wakubwa wa Ujerumani waliohusika na tafiti za ubongo wa binadamu, anga la juu, nyuklia, mwili wa binadamu na mambo ya kiroho walipelekwa Marekani kupitia The Operation Paper Clip na Urusi ya Kisovieti.
Tafiti nyingi za kisayansi za Ujerumani ya kinazi ndizo zilitumika kwa sana na pande mbili hasimu kupambana wakati wa vita baridi. Ukifuatilia vizuri Operation Mocking-Bird na kulinganisha alichokuwa anakisema Joseph Goebbels (Nazi Minister of Propaganda) utaona hakuna utofauti wowote ule. MK-ULTRA was the worse, maana inasemekana walianza na wanyama na baadae wakaja binadamu.
Mnazi Kurt Friedrich Plötner aliyekuwa mwanasayansi wa The SS ya Ujerumani aliajiriwa na CIA ya Marekani na akaendeleza biashara yake ya tafiti (Mind-Control) huku akiletewa binadamu ambao alikuwa anawafanyia hizi tafiti kama panya wa maabara. Wameanza miaka ya 1930's sijui leo hii 2021 watakuwa wamefika wapi, kuna mambo ukiyafikilia na kuyawaza kama una akili timamu ni lazima uyaogope sana mataifa kama Marekani, Urusi, uchina, Israeli na Uingereza.
Mataifa haya ni hatari sana kwa usalama wa dunia......
Hata maraisi wa Marekani waliodhani nchi yao ni dola takatifu baada ya kufahamu nini kinaendelea nyuma ya pazia na kwamba demokrasia ile ambayo wanaaminishwa kiuhalisia haipo waling'aka sana. Raisi Harry S. Truman kwenye baadhi ya Memoirs zake anakiri kabisa kwamba CIA aliyoianzisha imebadilika tofauti kabisa na matarajio yake na imekuwa ni taasisi ambayo ngazi zake za juu zimeshikiliwa na watoto wa familia kubwa za Marekani ambao wamesoma Harvard, Princeton, Oxford na Yale wakilinda maslahi mapana ya makundi husika.
Haikuishia hapo, Raisi Dwight Eisenhower anavyoondoka madarakani baada ya kufahamu kinachoendelea kule AREA 51 na sehemu nyingine alionya wamarekani na kuwaambia "Beware of the Military Industrial Complex".
Raisi John F.Kennedy baada ya kufahamu kwamba CIA ndiyo inaendesha nchi na siyo yeye alimfukuza kazi Allan Dulles lakini bahati mbaya bado akawa anaendelea kuendesha CIA kupitia mlango wa nyuma. Kennedy alipigiwa simu na Raisi wa Ufaransa Charles De Gaulle akiulizwa ni kwanini CIA inafanya operation dhidi ya Ufaransa, Kennedy akabaki anashangaa tu maana alikuwa hajuia chochote. Akaapa akisema "I splinter the CIA into 1000 pieces and scatter it into the wind" lakini CIA ndiyo ikaikata vipande 1000 familia ya Kennedy na kuitupa kwenye upepo.
Mind-Control is very real........
Truth-Serums are very real.........
Mass-Control of populations are very real.......(The color revolutions + Arab Spring+ Active Measures)
Tena siku hizi pamoja na huu utandawazi ndiyo balaa kabisa, wamefika hadi sebuleni kwako. Hivi hujiulizi kwanini Marekani ndiyo nchi inayoongoza kwa kutoa asilimia 60% ya huduma ya filamu za ngono na utupu mitandaoni ??? Tena nyingi ni bure kabisa. Jiulize ni watu wangapi tunaangalia hizo tovuti, unadhani wamezitoa bure tu kukufurahisha wewe ????
AU unadhani hizi filamu za Hollywood pamoja na miziki ambazo zimewatajirisha sana wahusika wake, unadhani lengo lake ni kukufurahisha wewe tu (Entertainment Purposes Only) na wao kupata faida za kiuchumi ????
Moja kati ya wasomi nguli kwenye karne yetu hii ya 21 ni Noam Chomsky (Among the most cited scholar) alisema haya "Democratic societies can't force people. Therefore they have to control what they think."
Siku hizi CIA hawafanyi kama ambavyo tunaaminishwa kuhusu MK-ULTRA ya zamani, au kama ambavyo George Orwell alisema kwenye kitabu chake 1984 kuhusu "The Thought Police". Ila siku hizi kinachofanyika ni kile ambacho Aldous Huxley alikiandika kwenye kitabu chake cha "A Brave New World" akisema kwamba moja ya njia ya kuongoza akili ya mtu ni kucheza na "Hedonistic Pleasures" zake.
Mfumo wa utandawazi na maisha yake ya leo hii ni njia tosha kabisa ya Mind-Control, ambayo ni silaha kubwa na yenye nguvu ya mataifa kama Marekani. Leo hii anaweza kusimama Biden akaongea kitu na vijana wa Hong-Kong wakaamua kuingia mtaani na kuanza kuchoma vitu. Unadhani hii ni kawaida ???? IT'S NOT NORMAL