Mjukuu wa Mandela: Babu angekuwapo angewaunga mkono HAMAS na Wapalestina dhidi ya Israel!

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
28,180
36,174
1. Huu ndiyo ulio ukweli mchungu wenye kuakisiwa vyema nyuma ya jitihada zote za Afrika Kusini hadi ICJ huko dhidi ya Israel.

2. Kwamba kuna mpenda haki wapi kwetu aliyebakia CCM, CHADEMA, ACT, UDSM au wapi wa aina ya mjukuu huyu wa Mandela?

IMG_20240511_170104.jpg


3. Kwamba nani anaweza kuthubutu kwa na hakika kusema Nyerere angesema nini? Kwani haijulikani au ni unafiki, umbumbumbu, ujuha, ushabiki, uchawa, na vya namna hiyo tu, uliowajaa watu hadi kina makongorosi huko kiasi cha kutokuwa na dira wala mwelekeo?

IMG_20240511_170153.jpg


4. Kwani Nyerere, Mandela, Castro, Tutu, Che Guevara, Mtikila, Maalim Seif, Chavez, Gaddafi nk au wa namna hiyo walikuwa na nini spesheli ambacho wengine wameshindwa kujitanabaisha navyo? Si kuwa walikuwa wenye kuendeshwa kwa nguvu za hoja?

IMG_20240511_170229.jpg


5. Kwamba mambo sisi, si ni ushabiki na mihemko tu? Hivi hadi aseme nani ndipo tugutuke ya kuwa kwa hakika tumepotea njia; na kuwa tuliko na tuendako si kwenyewe?

IMG_20240511_170303.jpg


6. Kwamba hata nyomi tuzionazo duniani kote nyuma ya HAMAS na Palestina si sauti za Mungu tena? Kwamba aje malaika kutokea wapi kutugatua wapi tutoke usingizini? Hivi hata tunajihurumia japo kidogo kuwa ndani ya umbumbumbu huu uliopitiliza mno, tuliomo?

7. Kwamba tumefeli wapi sisi Yarabi? Hivi sisi leo hata tunajuq kama Nyerere angekuwapo hata angesema nini? Ya kwamba hatukumsoma Wala kumwelewa? Ya kwamba aliondoka na yake yote? Na inakuwa jioni inakuwa asubuhi, tuko vizuri; maisha yanaendelea? "No wonder huwa tuko vizuri kugombea mali alizoacha marehemu!"

9. Kwamba mjukuu wa Mandela anajua Babu yake angesema nini, hata leo? Vipi contemporary, watoto, vijana, mabinti, wafuasi; wake, nk? "No wonder Afrika Kusini wanawakilisha wa aina ya kina Shivji, Ulimwengu na wachache mno wenye akili zao waliobakia hapa nchini, ambao pia nao wanaendelea kutoweka!"

9. Bila shaka baada ya kizazi cha kina Shivji na kina Ulimwengu, tutakuwa na "taifa la hovyo proper," kwa tunavyoshindana kuzidiana kuwa hovyo zaidi ya mwingine!

10. Alisema Prof. Chachage: "Babu zetu wakiwamo kina Kinjekitile, Mkwawa, Nyerere, Milambo, Sina, Isike, nk wangefufuka wakatukuta leo tulivyo komaa kuwashadadia mabeberu na wakoloni (wazungu kwa waarabu), watatukataa kuwa sisi si wajukuu zao!"

10. Kwamba wao katika uhai wao walipigana na kutupigania sisi wakipinga kutawaliwa na kwa nguvu zao wakiukataa ukoloni na utumwa? wengi wao hadi kupoteza maisha? Ya kuwa sisi leo ndiyo Hawa?

a) mkoloni na mlowezi ni wawekezaji, wafadhili au wahisani?!
b) Baina yetu tuna Arsenal, Chelsea, Man U, City, Real, Barca, nk; damu?!
c) Tunalazimishwa kwenda Rwanda tukipatikana kutaka hifadhi Uingereza ambako nako haturudi katu, kwa ridhaa zetu?!
d) tumekuwa wafuasi wa dini zao kuliko wao?!
e) Tunagombea kwenda ulaya na arabuni kwenda kuwa hata watumwa; wengine wakifia kwa maelfu baharini?
f) kwamba tumekuwa mabalozi wao hadi wanatushangaa?
g) kwamba tunaona heri tukawe magerezani kwao kuliko kuwa huru nchini?
h) kwamba tunatamani mkoloni angeendelea kuwapo kuliko yaliyotukuta baada ya uhuru?
i) Nk.

11. Kwa hakika washupavu hao (#10) wangesema: "katu sisi siyo wajukuu zao!"
 
1. Huu ndiyo ulio ukweli mchungu wenye kuakisiwa vyema nyuma ya jitihada zote za Afrika Kusini hadi ICJ huko dhidi ya Israel.

2. Kwamba kuna mpenda haki wapi kwetu aliyebakia CCM, CHADEMA, ACT, UDSM au wapi wa aina ya mjukuu huyu wa Mandela?

View attachment 2988004

3. Kwamba nani anaweza kuthubutu kwa na hakika kusema Nyerere angesema nini? Kwani haijulikani au ni unafiki, umbumbumbu, ujuha, ushabiki, uchawa, na vya namna hiyo tu, uliowajaa watu hadi kina makongorosi huko kiasi cha kutokuwa na dira wala mwelekeo?

View attachment 2988012

4. Kwani Nyerere, Mandela, Castro, Tutu, Che Guevara, Mtikila, Maalim Seif, Chavez, Gaddafi nk au wa namna hiyo walikuwa na nini spesheli ambacho wengine wameshindwa kujitanabaisha navyo? Si kuwa walikuwa wenye kuendeshwa kwa nguvu za hoja?

View attachment 2988028

5. Kwamba mambo sisi si ni ushabiki na mihemko hadi aseme nani ndipo tugutuke ya kuwa kwa hakika tumepotea njia; na kuwa tuliko na tuendako si kwenyewe?

View attachment 2988030

6. Kwamba hata nyomi tuzionazo duniani kote nyuma ya HAMAS na Palestina si sauti za Mungu tena? Kwamba aje malaika kutokea wapi kutugatua wapi tutoke usingizini? Hata tunajihurumia kweli japo kidogo kuwa ndani ya umbumbumbu huu uliopitiliza tuliomo?

7. Kwamba tumefeli wapi sisi Yarabi? Hivi sisi leo haya hatujui kama Nyerere angekuwapo hata angesema nini? Ya kwamba hatukumsoma Wala kumwelewa? Ya kwamba aliondoka na yake yote? Na inakuwa jioni inakuwa asubuhi, tuko vizuri maisha yanaendelea? No wonder huwa tuko vizuri kugombea mali alizoacha marehemu!

9. Kwamba mjukuu wa Mandela anajua Babu yake angesema nini hata leo? Vipi contemporary, watoto, vijana, mabinti, wafuasi; wake, nk? No wonder Afrika Kusini wanawakilisha wa aina ya kina Shivji, Ulimwengu na wachache mno wenye akili zao waliobakia hapa nchini, ambao pia nao wanaendelea kutoweka.

9. Bila shaka baada ya kizazi cha kina Shivji na kina Ulimwengu kitakapo kuwa hakipo, tutakuwa na "taifa la hovyo proper," kwa tunavyoshindana kuzidiana kuwa hovyo zaidi ya mwingine!

10. Alisema Prof. Chachage Babu zetu wakiwamo kina Kinjekitile, Mkwawa, Nyerere, Milambo, Sina, Isike, nk wangefufuka wakatukuta leo tulivyo komaa kuwashadadia mabeberu na wakoloni (wazungu kwa waarabu) watatukataa kuwa sisi si wajukuu zao!

10. Kwamba wao katika uhai wao walipigana na kutupigania wakipinga kutawaliwa na kwa nguvu zao wakiukataa ukoloni na utumwa; na wengi wao hadi kupoteza maisha; ya kuwa sisi leo:

a) mkoloni na mlowezi ni wawekezaji, wafadhili au wahisani?!
b) Baina yetu tuna Arsenal, Chelsea, Man U, City, Real, Barca, nk; damu?!
c) Tunalazimishwa kwenda Rwanda tukipatikana kutaka hifadhi Uingereza ambako haturudi katu, kwa ridhaa zetu?!
d) tumekuwa wafuasi wa dini zao kuliko wao?!
e) Tunagombea kwenda ulaya na arabuni kwenda kuwa hata watumwa wengine wakifia kwa maelfu bahati ya kati?
f) kwamba tumekuwa mabalozi wao hadi wanatushangaa?
g) kwamba tunaona heri tukawe magerezani kwao kuliko kuwa huru nchini?
h) kwamba tunatamani mkoloni angeendelea kuwapo kuliko yaliyotukuta baada ya uhuru?
i) Nk.

11. Kwa hakika washupavu hao (#10) wangesema: "katu sisi siyo wajukuu zao!"
Ni sawa kama walimuunga mkono Bashir watashindwa kuiunga mkono Palestine
 
1. Dedan Kimathi angefufuka angekukana MK254!

2. Zipo tofati za baina ya mbuzi na wajukuu wa Kimathi!
 
Suala siyo kuandamana, suala ni Israel na Palestinians wakubali kuishi pamoja , makabila 2 yanashindwa je kuishi pamoja? Au nyuma ya pazia kuna ajenda za siri? Pro Israel hawaoni athari za vita ambavyo vimeua watoto na wanawake wa kipalestina, pro hamas wanatamani kuona Israel inaangamia na kufutika kwenye uso wa dunia . Bila Palestinians leaders na Israel leaders kukaa pamoja na kuukubali ukweli kubwa wote tunahitajiana kuleta amani ya wayahudi na wapalestina, amani haitapatikana, pale ni dini ndio zinasababisha vita kati ya msimamo ya kiislamu na misimamo ya kiyahudi.
 
Bro hizi nguvu tungezitumia hata kupinga wamasai kufukuzwa loliondo....

1. Hata huko loliondo hatupoi.

2. Hapo #1, ni kama ilivyo kuwahusu kina Ben, Lijenje, Azory, Mawazo, Lissu au waliokuwa kwenye viroba na wasiojulikana.

3. Bro, hapo #2 kuna unayemkumbuka au hata kutafakari na dhulma iliyowakuta au kokote iliko?

4. Huyu mwamba Hapa chini ana maana yoyote kwako?

Shivji: Chimbuko la wasiokuwa na Hoja au uthubutu wa Kuhoji, linalo ligharimu Taifa (Part 1)

5. Au ubora wako uko wapi ndugu ambako wewe umeelekeza nguvu zako zaidi?

6. Zingatia, Hapo #5: hata kwenye magoma hatukuoni kama Vicky tu wa jabali la muziki?!
 
Suala siyo kuandamana, suala ni Israel na Palestinians wakubali kuishi pamoja , makabila 2 yanashindwa je kuishi pamoja? Au nyuma ya pazia kuna ajenda za siri? Pro Israel hawaoni athari za vita ambavyo vimeua watoto na wanawake wa kipalestina, pro hamas wanatamani kuona Israel inaangamia na kufutika kwenye uso wa dunia . Bila Palestinians leaders na Israel leaders kukaa pamoja na kuukubali ukweli kubwa wote tunahitajiana kuleta amani ya wayahudi na wapalestina, amani haitapatikana, pale ni dini ndio zinasababisha vita kati ya msimamo ya kiislamu na misimamo ya kiyahudi.

1. Suala la Palestina na Israel siyo la kidini:

IMG_1567.jpg


2. Suala la Palestina na Israel ni suala la mtu na mkoloni wake.

3. Hapo #2 ni sawa na Tanganyika na ujerumani kabla ya 1945 na Uingereza na Tanganyika 1945 - 1961.

4. Suala la ukoloni halikubaliki!
 
1. Suala la Palestina na Israel siyo la kidini:

View attachment 2988198

2. Suala la Palestina na Israel ni suala la mtu na mkoloni wake.

3. Hapo #2 ni sawa na Tanganyika na ujerumani kabla ya 1945 na Uingereza na Tanganyika 1945 - 1961.

4. Suala la ukoloni halikubaliki!
Kama ni hivo tuanze na Sahara
1. Suala la Palestina na Israel siyo la kidini:

View attachment 2988198

2. Suala la Palestina na Israel ni suala la mtu na mkoloni wake.

3. Hapo #2 ni sawa na Tanganyika na ujerumani kabla ya 1945 na Uingereza na Tanganyika 1945 - 1961.

4. Suala la ukoloni halikubaliki!
Basi sisi Africa tuanze na ukombozi wa nchi ya Sahara Magharibi inayokaliwa na Morocco kabla ya kwenda mbali kupambania wayahudi na wapalestina, hilo suala ni la dini kati ya dini ya kiyahudi na kiislam, ndo maana kila siku ni vurugu pale Jerusalem kwenye msikiti wa Al aquisa
 
Kama ni hivo tuanze na Sahara
1. Sasa mkuu unajua je kama wengine tunapiga miguu yote?

2. Kwamba tunayo mapafunya kokamaa kote Kwa wakati mmoja hadi Ukraine huko?

3. Si tulikubaliana kutokupangiana na kila mtu kushinda mechi zake kama anavyoona inafaa?

4. Tukianza kupangiana huoni mwingine atakuuliza kwanini tuanze Saharaw, wakati hatujamalizana na wasiojulikana wa kwetu?

5. Kwani ulishawapata kina Lijenje Azory Ben Mawazo au Hata kuwatambua waliokuwa kwenye viroba? Au nani walitaka kumwua Lissu? Wauaji Hawa wangalipo?

6. Mwuaji ni mwuaji tu!

Basi sisi Africa tuanze na ukombozi wa nchi ya Sahara Magharibi inayokaliwa na Morocco kabla ya kwenda mbali kupambania wayahudi na wapalestina, hilo suala ni la dini kati ya dini ya kiyahudi na kiislam, ndo maana kila siku ni vurugu pale Jerusalem kwenye msikiti wa Al aquisa

7. Kwani mbali ni wapi Ndugu?

8. Kwa mwendo huu huoni su muda mrefu utaona uanze East Africa, baadaye utagundua uande Tanzania, labda Tanganyika?

9. Kama haitoshi ukawa MLA nyama ya mtu kuwa kumbe uanze Mbeya, Chunya Nk?

10. Itatosha vipi kumbe itakuwa ni Kijiji mwisho utaona familia baadaye wewe mwenyewe hatimaye kumbe hata wewe utaona too much kumbe ujikite na Abdallah kichwa wazi tu?

11. Pengine hata hapo #10 ukaona Bado haitoshi?

12. Atatosheka na nini binadamu?!
 
Mambo yao waachiwe wenyewe...


Cc: Mahondaw

1. Kila mtu akishika lake, tutatoboa kweli?

F3k78Z8a0AAldWM.jpeg


2. Kwa mtaji huu waKo, hata katiba mpya itapatikana kweli?

3. Kwa mtaji huu pia, hata mtu itabidi kujiangalia mwenyewe na mtu mmoja mmoja itafikia kuwa ni too much labda kila kiungo kijijue kivyake vyake?
 
Back
Top Bottom