Mjini shule

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Feb 4, 2009
74,457
154,323
PaDri mmoja aliyekuwa na tabia ya kutembea na mke wa mtu kila mumewe alipokuwa kazini, siku moja siri ya uzinzi ilimfikia mwenye mali na kutakiwa arudi nyumbani ghafla. Jamaa alifanya hivyo na kukuta mlango umefungwa kwa ndani. Aligonga mkewe kwa woga wa kufumaniwa akachanganyikiwa, lakini Padri kwa kujiamini alivaa nguo na kujining’iniza dalini huku miguu ikionekana kwa chini.
Jamaa alipoingia alianza kumshutumu mkewe;
Jamaa: Nasikia unatembea na Padri?”
Mke: Watu waongo mume wangu, huyo Padri yupo wapi?”
Jamaa alianza kumtafuta kila kona lakini hakumuona alisahau kuangalia juu zaidi ya uvunguni na ndani ya kabati. Baada ya kuridhika kweli hakukuwa na mtu ndani, walikaa kitandani huku mkewe akiomba asiangalie juu.
Padri aliyekuwa akining’inia juu ya kenchi mikono yake ilichoka na kujikuta akidondoka toka na kuanguka mbele ya yule mwanaume na mkewe. Wote walishtuka kumuona Padri, jamaa aliuliza;
“Si huyu?”
Padri: “Huyu nani, nimesikia mkiniteta kuwa natembea na mkeo, lakini kwa uwezo wa roho mtakatifu amenileta ndani mwako ili unithibitishie kuwa mimi natembea na mke wako”
Jamaa alipoangalia juu hakuona sehemu yenye tundu alipopitia padri.
Jamaa: “Umepitia wapi?”
Padri: “Ni uwezo waroho mtakatifu aliyeniingiza kwa uwezo wake bila kuharibu bati wala kitu chochote”
Jamaa: “Samahani baba Padri”
Padri: “Nimekusamehe wewe na mkeo kwa kuwa hamkujua mtendalo”
Jamaa: “Asante baba Padri walimwengu ni wagombanishi”
Baada ya kusema hayo Padri alimfungulia mlango na kutoka huku mume akiamini kuwa ni kweli Padri kaletwa na roho mtakatifu. Kweli mjini shule.
 
janja ya njyani kula indi mbichi
PaDri mmoja aliyekuwa na tabia ya kutembea na mke wa mtu kila mumewe alipokuwa kazini, siku moja siri ya uzinzi ilimfikia mwenye mali na kutakiwa arudi nyumbani ghafla. Jamaa alifanya hivyo na kukuta mlango umefungwa kwa ndani. Aligonga mkewe kwa woga wa kufumaniwa akachanganyikiwa, lakini Padri kwa kujiamini alivaa nguo na kujining’iniza dalini huku miguu ikionekana kwa chini.
Jamaa alipoingia alianza kumshutumu mkewe;
Jamaa: Nasikia unatembea na Padri?”
Mke: Watu waongo mume wangu, huyo Padri yupo wapi?”
Jamaa alianza kumtafuta kila kona lakini hakumuona alisahau kuangalia juu zaidi ya uvunguni na ndani ya kabati. Baada ya kuridhika kweli hakukuwa na mtu ndani, walikaa kitandani huku mkewe akiomba asiangalie juu.
Padri aliyekuwa akining’inia juu ya kenchi mikono yake ilichoka na kujikuta akidondoka toka na kuanguka mbele ya yule mwanaume na mkewe. Wote walishtuka kumuona Padri, jamaa aliuliza;
“Si huyu?”
Padri: “Huyu nani, nimesikia mkiniteta kuwa natembea na mkeo, lakini kwa uwezo wa roho mtakatifu amenileta ndani mwako ili unithibitishie kuwa mimi natembea na mke wako”
Jamaa alipoangalia juu hakuona sehemu yenye tundu alipopitia padri.
Jamaa: “Umepitia wapi?”
Padri: “Ni uwezo waroho mtakatifu aliyeniingiza kwa uwezo wake bila kuharibu bati wala kitu chochote”
Jamaa: “Samahani baba Padri”
Padri: “Nimekusamehe wewe na mkeo kwa kuwa hamkujua mtendalo”
Jamaa: “Asante baba Padri walimwengu ni wagombanishi”
Baada ya kusema hayo Padri alimfungulia mlango na kutoka huku mume akiamini kuwa ni kweli Padri kaletwa na roho mtakatifu. Kweli mjini shule.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom